Maporomoko

Bobi Wine amtaka Jaji Mkuu kutosikiliza shauri lake

And we'll keep you signed in.

Sign in orRegister

Why sign in to the BBC?

Got a TV Licence?

You need one to watch live TV on any channel or device, and BBC programmes on iPlayer. It’s the law.

Find out more
I don’t have a TV Licence.

Muhtasari

  1. Mahakama ya Rwanda kuanza kusikiliza kesi ya Paul Rusesabagina
  2. Bobi Wine amtaka Jaji Mkuu kutosikiliza shauri lake

Habari za moja kwa moja

Na Lizzy Masinga

time_stated_uk

  1. Mahakama ya Rwanda kuanza kusikiliza kesi ya Paul Rusesabagina

    Paul Rusesabagina
    Copyright: BBC
    Image caption: Paul Rusesabagina

    Mahakama ya Rwanda hii leo inaanza kusikiliza kesi dhidi ya Paul Rusesabagina nawengine 20 ambao wanakabiliwa na mashtaka ya ugaidi.

    Rusesabagina,mkosoaji wa Rais Paul Kagame, anatuhumiwa kuunga mkono shughuli za kikosiNational Liberation (FLN), ambaco ni mrengo wa wanamgambo wa chama chake chaRwandan Movement for Democratic Change (MRCD).

    Paul Rusesabagina
    Copyright: BBC
    Image caption: Paul Rusesabagina akiwa Mahakamani

    Alikamatwa mnamo Agosti 2020 akiwa katika nchi ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na kurudishwa nchini Rwanda kukabiliana na mashtaka ya ugaidi, utekaji nyara na mauaji.

    Mwezi Julai mwaka 2018, FLN ilidai kuhusika na mashambulio katika mkoa wa kusini wa Rwanda.

    Paul Rusesabagina
    Copyright: BBC

    Rusesabagina alifahamika kufuatia filamu ya Hotel Rwanda ikielezea jinsi alivyookoa maisha ya watutsi waliokuwa wamekimbilia katika hoteli moja mjini Kigali aliyokuwa meneja wake mwaka 1994.

    Rais Paul Kagame amesema kikubwa sio ushujaa wa Bwana Rusesabagina au vitendo vyake wakati wa mauaji ya kimbari akisema kinachoangaliwa kwa sasa ni yeye.

    Bwana Kagame amesema kwamba hajali kuhusu hadithi ya Bwana Rusesabagina kwamba yeye ni shujaa wa mauaji ya kimbari na kwamba ''hilo si jambo ambalo litakalomkabili mahakamani''.

    "Kuna maswali ambayo lazima atayajibu.kuna wanaomsaidia wakiwa Ulaya,Marekani na kwIngineko na ambao walimpandisha cheo na kumpa majina ya ushujaa.awe shujaa au la ,mimi sina wasi wasi na hilo.

    Paul Rusesabagina
    Copyright: BBC
    Image caption: Balozi wa Marekani nchini Rwanda akiingia mahakamani kusikiliza kesi hiyo
  2. Bobi Wine amtaka Jaji Mkuu kutosikiliza shauri lake

    Bobi Wine aliibuka mshindi wa pili katika uchaguzi wa mwezi Januari
    Copyright: Getty Images

    Kiongozi wa upinzani RobertKyagulanyi maarufu Bobi Wine , amemtaka jaji Mkuukujiondoa katika kusikiliza shauri la kupingakuchaguliwa tena Rais Yoweri Museveni.

    Bobi Wine amemshutumujaji Alfonse Owiny- Dollo kwa upendeleo kwa sababu ya ushirika wake na rais.

    Mwanasiasa wa upinzanipia anataka majaji wengine wawili wa mahakama ya juu kujiondoa kusikilizashauri hilo kwa misingi hiyo hiyo.

    Majaji watatuhawajajibu chochote kuhusu shutuma dhidi yao.

    Jaji Mkuu Owiny-Dolloalikuwa mwanasheria wa Rais Museveni mwaka 2006, kwa mujibu wa tovuti ya NilePost.

    Jaji Mike Chibitaalikuwa msaidizi wa Museveni katika masuala ya sheria, wakati Jaji EzekielMuhanguzi ni ndugu wa Waziri wa Ulinzi Elly Tumwine kwa mujibu wa vyombo vyahabari vya nchini humo.

    Bobi Wine amedai kuwawatatu hao hawataweza kutenda haki iwapo watasikiliza shauri hilo.

  3. Habari! karibu katika matangazo ya moja kwa moja ya taarifa zetu