Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Yemen

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
الجمهورية اليمنية
Al-Jumhūriyyah al-Yamaniyyah

Jamhuri ya Yemen
Bendera ya YemenNembo ya Yemen
BenderaNembo
Kaulimbiu ya taifa:Allah, al-Watan, at-Thawra, al-Wehda
(Mungu, taifa, mapinduzi, umoja)
Wimbo wa taifa:Jamhuri ya Maungano
Lokeshen ya Yemen
Mji mkuuSana'a
15°21 N 12°24 E
Mji mkubwa nchiniSana'a
Lugha rasmiKiarabu
SerikaliJamhuri
Abd Rabbuh Mansur Hadi
Khaled Bahah
Establishment
Maungano ya Yemen Kaskazini
na Kusini

22 Mei1990
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
527,970 km² (50)
kidogo sana
Idadi ya watu
 -Julai 2018 kadirio
 -2004 sensa
 - Msongamano wa watu
 
28,498,683 (48)
19,685,000
44.7/km² (160)
FedhaYemeni rial $1 = 198.13 Rials (YER)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+3)
(UTC)
Intaneti TLD.ye
Kodi ya simu+967

-


Yemen (kwaKiarabu: ٱلْيَمَن‎, al-Yaman), rasmiJamhuri ya Yemen, ninchi iliyoko kwenye ncha ya kusini-magharibi yaRasi ya Uarabuni baraniAsia. Inapakana naSaudi Arabia kaskazini,Oman mashariki, na imepakana naGhuba ya Aden naBahari ya Shamu kusini na magharibi. Yemen ina eneo la takriban kilomita za mraba 555,000 na idadi ya watu inayokadiriwa kuwa zaidi ya milioni 34. Mji wake mkuu niSana'a, ingawaserikali kwa sasa inaendesha shughuli nyingi kutoka mji wa muda wa Aden kutokana na hali yakisiasa. Yemen ni mojawapo ya nchi zenye historia ndefu yaustaarabu katika eneo laKiarabu, ikiwa ni nyumbani kwa falme za kale kama Saba na Himyar.

Hata hivyo, katika karne ya sasa, nchi hii imekumbwa na migogoro ya kisiasa na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodhoofisha uchumi na hali ya kibinadamu.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Hadi mwaka1990 palikuwa na nchi mbili za Yemen ya Kaskazini na Yemen ya Kusini.

Ile yakaskazini ilikuwaUfalme wa Yemen baada yaImamu Yahya Muhamad wa kundi laZaidiya kuvamiavelayat ya Yemen ya milki yaWaturukiWaosmani (1 Novemba1918). Baadaye ikawaJamhuri kwa njia yamapinduzi (1962).

Ile yakusini ilikuwa sehemukoloni (Aden) na sehemunchi lindwa (Hadramaut) yaWaingereza. Baada yaukoloni kwisha ikawa mara moja Jamhuri (30 Novemba1967).

Nchi hizo mbili ziliungana tarehe22 Mei1990, lakiniuongozi ulizidishaufisadi, na tangu mwaka2011 hali yasiasa ni tata.Vita vya wenyewe kwa wenyewe vinaendelea kwa misaada kutoka nchi za nje, hasa kutokana na uwepo wa makundi makubwa adui yaWasuni naWashia.

Matokeo yake ni njaa kwa wakazi 17,000,000 kiasi kwamba Yemen imehesabika kuwa nchi inayohitaji zaidi misaada ya kibinadamu.

Watu

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi wengi ni Waarabu wa makabila mbalimbali; wengine ni machotara wa Kiarabu-Kiafrika,Waajemi naWazungu.

Lugha rasmi na ya kawaida niKiarabu.

Upande wadini, wananchi karibu wote (99%) niWaislamu, wakiwemoWasuni (60–65%) naWashia (35-40%). Waliobaki niWakristo,Wayahudi,Wahindu au hawana dini yote.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo yaAsia

Afghanistan |Armenia2 |Azerbaijan |Bahrain |Bangladesh |Bhutan |Brunei |China |Falme za Kiarabu |Georgia2 |Hong Kong3 |Indonesia |Iran |Iraq |Israel |Jamhuri ya China (Taiwan) |Japani |Kamboja |Kazakhstan |Kirgizia |Korea Kaskazini |Korea Kusini |Kupro2 |Kuwait |Laos |Lebanoni |Macau3 |Malaysia |Maldivi |Mongolia |Myanmar |Nepal |Omani |Pakistan |Palestina |Qatar |Saudia |Singapuri |Sri Lanka |Syria |Tajikistan |Timor ya Mashariki |Turkmenistan |Ufilipino |Uhindi |Urusi1 |Uthai |Uturuki1 |Uzbekistan |Vietnam |Yemen |Yordani

1. Nchi ina maeneo katikaAsia naUlaya. 2. Nchi ikoAsia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi zaUlaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.
Makala hii kuhusu maeneo yaYemen bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuYemen kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Yemen&oldid=1425950"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp