Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Yangtze (mto)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutokaYangtse)
Mto Yangtze ( Changjiang)
Beseni ya Yangtze
ChanzoTibet (China)
MdomoBahari ya Mashariki ya China karibu naShanghai
NchiChina
Urefu6,380 km
Kimo chachanzo5,405 m
Mkondo31,900 m³/s
Eneo labeseni1,800,000 km²
Miji mikubwa kando lakeChongqing,Wuhan,Nanjing,Shanghai
Mto Yangtze, ambayo ni mto mrefu Asia na huesabika kama mto watatu mkubwa dunia nzima
Pinde la kwanza la Yangtze katika jimbo laYunnan ambako mto hugeukia 180° kutoka mwelekeo wa kusini kuelekea kaskazini

Mto Yangtze (pia:Changjiang) ni mto mkubwa nchiniChina na pia mto mrefu waAsia yote. Duniani huhesabiwa kama mto mrefu wa tatu baada yaAmazonas naNaili).

Mwendo wake wote wa kilomita 6,300 pamoja na kilomita 2,800 zinazotumiwa na meli uko ndani ya China.

Chanzo chake iko katika nyanda za juu za Tibet. Inafuata mwelekeo wa kusini-mashariki hadi kilomita 1,500 baada ya chanzo. Hapa inasimamishwa na milima yenye mawe magumu na kugeuka ikuelekea sasa kwenda kaskazini-mashariki.

Katikati ya mwendo wake mto hupita kwenye mabode makali. Hapa serikali ya China iliamua kujengalambo la magenge matatu linalo umbara zake zimeonakana kwa sababu watu milioni 1.5 walipaswa kuhamishwa na tayari tatizo la matope kujaza ziwa nyuma ya lambo limeshaanza.

Kuna miji mingi mikubwa inayotegemea mto huu na machafuko kutoka ya viwanda vyao yamekuwa tatizo.

Katika historia mwendo wa Yangtze ilikuwa mpaka kati ya China ya kaskazini na China ya kusini.

Makala hii kuhusu maeneo yaChina bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuYangtze (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Yangtze_(mto)&oldid=1178951"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp