Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Washington, D.C.

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wilaya ya Columbia
Washington, D.C.
Jimbo
Kauli Mbiu
"Justitia Omnibus" (Haki kwa Wote)
Ramani ya
Ramani ya
Mahali pa Washington, D.C. katika Marekani
NchiMarekani
Lugha rasmiKiingereza
Lugha zinazozungumzwa87%Kiingereza
6.6%Kihispania
Kabila
UtaifaMkaazi wa D.C.
Serikali
MeyaMuriel Bowser
Eneo
Jumla177 km²
Ardhi158 km²
Maji19 (10.73%)
Idadi ya Watu
Kadirio 713,549
Pato la Taifa(2023)
Jumla $176.502 bilioni (ya 15)
Kwa kila mtu $135,100
HDI (2021)0.947(ya 7)
Maendeleo ya Juu Sana
Mapato ya Kati
ya Kaya (2023)
$108,200 (ya 1 kati ya majimbo na DC)
Majira ya saaUTC−5 (EST), UTC−4 (EDT)
Tovuti
🔗dc.gov
Nguzo ya Washington na Nyumba Nyeupe (White House)

Washington, D.C., rasmi inajulikana kamaWilaya ya Columbia na kwa kawaida huitwaWashington auD.C., ni mji mkuu na wilaya ya shirikisho yaMarekani. Jiji hili liko kwenye Mto Potomac, mkabala naVirginia, na linapakana naMaryland upande wa kaskazini na mashariki. Lilipewa jina laGeorge Washington, rais wa kwanza waMarekani. Wilaya hiyo imepewa jina laColumbia, mfano wa kike wa taifa.

Jina la mji mkuu limechaguliwa kwa heshima ya kiongozi wa uhuru na rais wa kwanzaGeorge Washington. Jina la "District of Colombia" likachaguliwa kwa heshima yaKristoforo Kolumbus mpelelezi wa Amerika.

Mji wa Washington uko kando lamto Potomac kati ya majimbo yaMaryland naVirginia. Uko karibu na pwani la mashariki la Marekani.Hori ya Chesapeake ya Atlantiki iko 35 km kutoka mji.Anwani ya kijiografia ni 38°53'42"N na 77°2'12"W.

Washington D.C. ni tofauti najimbo la Washington lililopo upande wa magahribi wa Marekani.

Hapa ni makao rasmi ya Bunge la Marekani, ya Rais pamoja na serikali yake na makao ya mahakama kuu. Kuna pia majengo ya kihistoria hata kama Marekani haina historia ndefu pamoja na makumbusho mazuri.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Makao ya kwanza ya serikali ya Marekani ilikuwa New York. Rais George Washington mwenyewe alichagua eneo la mji mpya kando la mto Potomac mwaka 1790. Ujenzi wa ikulu la Nyumba Nyeupe ulianza 1792. Mpango wa mji ulifuata mfano wa mji waKarlsruhe (Ujerumani).

11. Juni 1800 Washington ikawa mji mkuu wa Marekani. Wakati wavita ya Uingereza na Marekani ya 1814 mji ulivamiwa na kuchomwa na Waingereza.

Hadivita ya wenyewe kwa wenyewe ya Marekani Washington ilikuwa mji mdogo usiozidi wakazi 75,000 lakini ilikua baada ya vita kwa sababu serikali iliongezeka idara na wafanyakazi.

Tangu 1878 mji wa Washington na mkoa wa shirikisho ("D.C.") viliunganishwa. Mji kama mkoa ulitawaliwa moja kwa moja na bunge. Tangu 1973 mji umempata meya na serikali ya kimanisipaa. Kwenye bunge lenyewe hakuna mbunge wa wakazi wa Washington. Kuna mwakilishi wao mle lakini hana kura.

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]


Majimbo na maeneo yaMarekani
Majimbo ya Marekani
AlabamaAlaskaArizonaArkansasCaliforniaColoradoConnecticutDelawareFloridaGeorgiaHawaiiIdahoIllinoisIndianaIowaKansasKentuckyLouisianaMaineMarylandMassachusettsMichiganMinnesotaMississippiMissouriMontanaNebraskaNevadaNew HampshireNew JerseyNew MexicoNew YorkNorth CarolinaNorth DakotaOhioOklahomaOregonPennsylvaniaRhode IslandSouth CarolinaSouth DakotaTennesseeTexasUtahVermontVirginiaWashingtonWest VirginiaWisconsinWyoming
Mkoa wa Mji Mkuu
Mkoa wa Columbia (Washington D.C.)
Visiwa vya ng'ambo
KatikaPasifiki:Samoa ya MarekaniVisiwa vya Mariana ya KaskaziniGuamKatikaKaribi:Puerto RicoVisiwa vya Virgin vya MarekaniVisiwa vidogo sana vyaPasifiki:Kisiwa cha HowlandKisiwa cha JarvisAtolli ya JohnstonKingman ReefAtolli ya MidwayKisiwa cha BakerAtolli ya PalmyraKisiwa cha WakeKisiwa kidogo cha Karibi:Kisiwa cha Navassa
Makala hii kuhusu maeneo yaMarekani bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuWashington, D.C. kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Washington,_D.C.&oldid=1433713"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp