Ukoloni ni mfumo wataifa moja kuvuka mipaka yake na kutawala maeneo ya mbali yanayokaliwa na watu wengine kwa nyanja zauchumi,utamaduni najamii. Maeneo hayo yanaweza kuitwa makoloni ya kawaida au maeneo lindwa tu.
Neno hilo la Kilatini lilitumiwa baadaye kwa ajili ya kutaja makazi mapya ya watu kutoka eneo moja katika eneo la mbali. Ilhali hatua hii ilimaanisha mara nyingi pia upanuzi wautawala wa eneo mama, neno likataja baadaye pia eneo linalotawaliwa na nchi ya mbali.
Lakini kulikuwa na vipindi vya ukoloni pia zamani katikahistoria kama vile ukoloni waRoma ya Kale, ukoloni waWaarabu na wengine. Ukoloni kwa maana hii unaweza kuwa tofauti na kuundwa kwakoloni katika vipindi mbalimbali vya historia ambapo maeneo bila wakazi au yenye wakazi wachache sana yaliingiliwa na watu kutoka sehemu nyingine.
Ukoloni mamboleo ni aina ya nchi au kundi la nchi fulani kutawala nchi nyingine kinyemela kwa kuweka vikwazo na masharti yatakayowafanya watawaliwa waendelee kuwa nauchumi tegemezi ili watajirishe zaidi hao wanaowatawala kinyemela.
Utawala huo ulitegemea hali yataifa husika pamoja na hali yajamii zilizokuwa zinatawaliwa.
Baada ya kuanzisha utawala huo wakoloni walibadilishautawala wa jadi na kuufanya utawale kwamasilahi ya wakoloni; pia utawala huo uliharibuhadhi ya utawala wa jadi na misingi yajadi.