Katika vita kuna pande mbili au zaidi. Husababisha mateso, vifo na kuharibika kwamali ya watu pamoja namazingiraasilia.
Mwanamgambo wa Kipalestina akiwa ameshika silaha aina yaM16 rifle, mwaka 2009.
Asili ya vita ilikuwa mapambano kwa silaha kati ya makabila au vijiji mbalimbali. Baada ya kutokea kwamadola ilikuwa zaidi serikali au watawala wa madola walioamua juu ya vita.
Mlipuko wa silaha ya nyuklia mwaka 1951.
Aina za vita
Kuna aina tofauti za vita:
vita kati yanchi mbili au zaidi kwa niaba yaserikali zao
vita ya uhuru ambako watu wa eneo fulani wanapambania dola ya pekee, kwa mfano
vita ya wenyeji wa koloni au nchi lindwa dhidi ya serikali ya kikoloni au nchi inayotawala
vita ya watu wa sehemu moja ya nchi dhidi ya serikali ya nchi nzima
Watekelezaji wa vita
Watekelezaji wa vita huitwaaskari auwanajeshi.Historia imejua vipindi ambapowanaume wote wa nchi fulani walitakiwa kushika silaha na kushiriki katika mapigano. Palikuwa pia na vipindi nautamaduni ambapo wapiganaji walikuwa watu wa pekee wenyejukumu hilo ama kwa sababu walipaswa kuwa askari kufuatana nasheria za nchi au kwa sababu walikodiwa kwakazi hii.
Wanajeshi rasmi huwa chini yakanuni za vita lakini sehemu kubwa na vita inashirikisha watu wasiofuata kanuni hizo kamawanamgambo hasa katika vita za wenyewe kwa wenyewe.
Silaha
Wanadamu wametumiaakili nyingi kuboresha vifaa vya vita, yaanisilaha, na mbinu za vita.Maendeleo ya silaha yamesababisha kupungua kwaidadi ya askari wanaopigana moja kwa moja lakini uharibifu wa silaha umeongezeka.
Silaha za kale zilitegemeanguvu yamkono wa mtu zikifikiaumbali mdogo. Silaha zimebadilika kulenga mahali ambapo ni mbali zaidi na zaidi. Silaha kali za kisasa zina uwezo wa kuharibu nchi yote; jumla yasilaha za nyuklia inatosha kuuauhai woteduniani.
Jitihada za kuepa au kupunguza athari za vita
Kutokana na uharibifu mkubwa unaosababishwa na vita palikuwa tena na tena na makubaliano juu ya kanuni za vita. Kanuni hizo hulenga kupunguza hasara inayosababishwa na mapigano. Lakini historia imejaa pia mifano ambapo kanuni hizo zilivunjwa au kupuuzwa.