Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

V

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alfabeti ya Kilatini
AaBbCcDd
EeFfGgHhIiJj
KkLlMmNnOoPp
QqRrSsTtUuVv
WwXxYyZz
(Kwa matumizi ya Kiswahili)
chdhghkh
mbmvndngng'nj
nynzshth

V ni herufi ya 22 katikaalfabeti ya Kilatini ambayo ni pia mwandiko waKiswahili cha kisasa. Asili yake niipsilon katikaalfabeti ya Kigiriki.

Maana za V

[hariri |hariri chanzo]

Historia ya alama V

[hariri |hariri chanzo]

Historia ya V ina asili za pamoja na U, W, Y na F. Historia hii ni ngumu kidogo kwa sababu alama ilipita katika alfabeti za lugha ambazo zilitumia hasa alama hii kwa sauti tofautitofauti. Kwa sababu hii matamshi yalibadilika kati ya lugha na lugha. Pia lugha mpya iliweza kuona haja ya kuunda alama mpya kwa sauti ya pekee.

Kisemiti asilia:
picha ya kingoe
Kifinisia:
Waw
Kigiriki:
ipsilon
Kietruski:
V
Kilatini:
V

Alama ya V kiasili ilimaanisha sauti za "v" na "u" kwa pamoja katika Kilatini cha Kale. Iliandikwa kama V na matamshi yake yalitegemea nafasi yake katika neno pia lahaja mbalimbali. Tofauti ilikubwaliwa tu wakati wa Kilatini Kipya katika karne ya 16 ambako wataalamu wa Ulaya walikubaliana kutumia alama yenye kona V kwa sauti yakonsonanti na alama isiyo na kona U kwavokali.

Waroma walipokea alama hii kutokaalfabeti ya Kigiriki kupitia alfabeti za Kiitalia za awali kamaKietruski. Wagiriki walipokea kutokaWafinisia.

Wafinisia walikuwa na "waw" iliyokuwa kiasili picha iliyorahisishwa ya fimbo la kingoe au kiopoo. Wagiriki wa Kale walichukua alama hiyo na kuitumia kwa namna mbili: kwa umbo moja kamadigamma (tazamaF) na umbo la pili kama "ipsilon" bila kujali maana asilia ilitaja sauti kati ya "u" na "i".

Waitalia ya kwanza wakaendelea kutumia alama kwa aina ya "u" lakini pia "v" kama ilikuwa mwanzoni wa neno. Waroma walipokea vile.

Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=V&oldid=1093997"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp