Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Usanisinuru

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kila jani kina kiwanda cha kikemia ndani yake.

Usanisinuru (piausanidimwanga, ing.photosynthesis) ni mchakato wa kibiolojia na kikemia ambakomimea yakijani inageuzanguvu yanuru yajua kuwanishati ya kikemia. Inatengenezakabohidrati ikitumia nguvu ya nuru ya jua nadioksidi kabonia yahewani pamoja namaji.

Nje ya mimea kuna pia aina kadhaa zabakteria na hasamwani zinazofanya usanisinuru.

Fomula yake ni

6CO2 + 12H2O + nuru →C6H12O6 + 6O2 + 6H2O
dioksidi kabonia +maji + nishati nuru →glukosi +oksijeni +maji

Usanisinuru ni msingi wamaisha yoteduniani. Unajengamada ogania ambayo ni chanzo chalishe katikamtando chakula kwa karibuviumbehai vingine vyote kwa njia moja au nyingine. Kwa njia hii ni chanzo chamtando chakula wauhai wote.

Mchakato wa usanisinuru

[hariri |hariri chanzo]
Picha ya kiwiti (chloroplast)

Usanisinuru unaanza kwenye sehemu za kijani za majani. Rangi ya kijani inatokana na punje ndogo sana zakiwiti ndani ya majani. Wakati nuru ya jua inafikia kiwiti inasababisha kemikali ndani yake kuvunja molekuli za maji. Molekuli ya maji ikivunjwa inatoa oksijeni,hidrojeni na nishati. Protini ndani ya seli inatumia dutu hizi pamoja na dioksidi kabinia ya hewani kujengaglukosi naATP ambayo ni molekuli yafosifati inayotunza nishati nyingi ndani yamuungo kemia wake.

Katika mchakato huu oksijeni inaachishwa na hivyo usanisinuru ni pia chanzo chaoksijeni katikaangahewa ya dunia jinsi ilivyo.

Makala hii kuhusu mambo yabiolojia bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuUsanisinuru kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Usanisinuru&oldid=1151364"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp