Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Umoja wa Mataifa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Umoja wa Mataifa
United Nations
منظمة الأمم المتحدة
联合国
Organisation des Nations unies
Организация Объединённых Наций
Organización de las Naciones Unidas
Nchi wanachamaNchi wanachama
Mji mkuu
na mkubwa
760 United Nations Plaza, Manhattan, New York City (eneo la kimataifa)
Lugha rasmiKiarabu
Kichina
Kiingereza
Kifaransa
Kirusi
Kihispania
  Katibu Mkuu
António Guterres
  Naibu Katibu Mkuu
Amina J. Mohammed
  Rais wa Baraza Kuu
Philemon Yang
  Rais wa Baraza la Kiuchumi na Kijamii
Bob Rae
Wanachama193 mataifa wanachama
2 mataifa waangalizi
Historia
  Kusainiwa kwa mkataba wa UM
26 Juni 1945
  Mkataba ulifanyishwa kazi
24 Oktoba 1945
Jina la kikoa.un

Umoja wa Mataifa (UM) (Kiingereza:United Nations, UN) nishirika lakiserikali ambalo malengo yake ni kudumishaamani nausalama wa kimataifa, kuendeleza uhusiano wa kirafiki kati ya mataifa, kufikia ushirikiano wa kimataifa, na kuwa kituo cha kuoanisha matendo ya mataifa. Niumoja wanchi zoteduniani isipokuwa zile zisizotambuliwa kuwadola huru.

Umoja huo ulianzishwa na nchi washindi waVita Kuu ya Pili ya Dunia kuchukua nafasi yaShirikisho la Mataifa (1919 -1946). Makubaliano yalifikiwatarehe24 Oktoba1945 hukoSan Francisco,California.

Mwanzoni nchi zilikuwa 51 lakini kufikia mwaka2017 kulikuwa na nchi wanachama 193, mbali yaUkulu mtakatifu (Vatikani) naPalestina ambazo zinashiriki kamawatazamaji wa kudumu, zikiwa nahaki karibu zote isipokuwa kupigakura.

Dhumuni la umoja huu ni kuratibu mahusiano ya kimataifa kupitiasheria na mikataba ya kimataifa kwenye maeneo kamausalama,amani,maendeleo ya jamii na yauchumi,haki za binadamu,uhuru,demokrasia n.k.

Toka mwanzomakao makuu ya Umoja wa Mataifa yakoManhattan,New York City,New York nchiniMarekani na hayako chini yamamlaka ya nchi hiyo.Ofisi nyingine zikoGeneva (Uswisi),Nairobi (Kenya) naVienna (Austria).

Lugha rasmi za UM nisita:Kiarabu,Kichina,Kifaransa,Kihispania,Kiingereza naKirusi.

Katibu Mkuu wa UM anachaguliwa kwa miaka mitano; kwa sasa niAntónio Guterres kutokaUreno, aliyechaguliwa kuwa Katibu Mkuu mwaka2016 akichukua nafasi yaBan Ki-moon.

Muundo

Ukumbi wa UM.

UM una vyombo vitano:

Cha sita kilikuwaBaraza la Wafadhili la UM (Trusteeship Council), ambacho kimesimama mwaka1994.

Baraza la Usalama linaamua kutumawalinzi wa amani wa UM penye maeneo ya ugomvi.

Mashirika ya pekee

  • UNICEF (United Nations Children's Fund) - Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa
  • WHO (World Health Organization) Taasisi ya Afya ya Ulimwengu
  • FAO (Food and Agriculture Organization) - Taasisi ya Chakula na Kilimo
  • UNESCO (United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization) - Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi, na Utamaduni
  • ILO (International Labour Organization) Taasisi ya Kimataifa ya Kazi
  • IMF (International Monetary Fund) - Mfuko wa Fedha wa Kimataifa
  • UNCTAD (United Nations Conference on Trade and Development) - Mkutano wa Kimataifa kuhusu Biashara na Maendeleo
  • ITC (International Trade Centre (UNCTAD/WTO) -
  • UNDCP (United Nations Drug Control Programme) - Taasisi ya Kimataifa ya Mpango wa Kusimamia Madawa
  • UNDP (United Nations Development Programme) - Mpango wa Kimataifa wa Maendeleo
  • UNIFEM (United Nations Development Fund for Women) Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Wanawake
  • UNV (United Nations Volunteers)
  • UNEP (United Nations Environment Programme) Mpango wa Kimataifa wa Mazingira
  • UNFPA (United Nations Fund for Population Activities)
  • UNHCR (Office of the United Nations High Commissioner for Refugees)
  • UN-HABITAT (United Nations Human Settlements Programme)
  • UNRWA (United Nations Relief and Works Agency for Palestine Refugees in the Near East)
  • IAEA (Shirika la Kimataifa la Nishati ya Nyuklia) inashirikiana na UM na kutoa taarifa kwa Baraza la Usalama hata kama si chini ya katiba ya UM
  • UNDIO ( United Nations Data and Information Organization)

Viungo vya nje

Tovuti rasmi

Tanbihi

    Makala hii kuhusu mambo yasiasa bado nimbegu.
    Je, unajua kitu kuhusuUmoja wa Mataifa Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari
    Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
    Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
    Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Umoja_wa_Mataifa&oldid=1434013"
    Jamii:
    Jamii iliofichwa:

    [8]ページ先頭

    ©2009-2026 Movatter.jp