Habari kuu za kipindi cha kwanza, kama ile yasiku yaPentekosteRoho Mtakatifu kuwashukia wafuasi waYesu, zinapatikana hasa katikaMatendo ya Mitume,kitabu kilichoandikwa namwinjili Luka kwenyemiaka ya 80. Humo unasimuliwa hasauenezi waUkristo katika maeneo ya upande wakaskazini waBahari ya Kati.
Tukio lingine muhimu linalosimuliwa na Luka niuongofu waMtume Paulo, mwenezi mkuu wa Ukristo namfafanuzi bora waimani hiyo mpya.[1]
Pamoja na uenezi, linajitokeza badiliko kubwa laWakristo: awali walikuwa woteWayahudi ama kwa kuzaliwa ama kwa kuongoka,[2] nao wanaitwaWakristo wa Kiyahudi. Lakini katikakarne ya 1 tayariidadi yao ilizidiwa na ile ya Wakristo wamataifa mengine.
Sambamba na hilolughaya kimataifa yaKigiriki ilizidi kutumika badala yaKiaramu,lugha mama ya Yesu na mitume wake.[3] Ndiyo sababuAgano Jipya limeandikwa lote kwa Kigiriki. Vitabu 27 vinavyoliunda vilianza kulinganishwa na vile vyaAgano la Kale kama vitakatifu.
TenaYerusalemu, uliokuwamji mkuu waWayahudi na waWakristo wa kwanza, ulizidi kukosa umuhimu, hasa baada yaMtume Petro na wenzake kuuhama au kuuawa. Wakati wavita vya kwanza vya Kiyahudi hata waumini wa kawaida walihama, na waliporudi hakukuwa tena nahekalu, kwa kuwa lilibomolewa mwaka70. Mbali ya hayo, uhusiano na Wayahudi ulizidi kuharibika, na hatimaye Wakristo walikatazwa wasishiriki tena ibadasinagogini.
Jumuia yaRoma,makao makuu yadola, ilizidi kuwa muhimu, hasa baada ya kufikiwa na Petro na Paulo, ambao walimalizia hukokazi yao kwakufia dini katikadhuluma ambayo ilianzishwa naKaisari Nero mwaka64 na kuendelea kwakwikwi hadi mwaka313.