Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Ukanamungu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Uatheisti
Atheism (en)

ukubwa_wa_picha
Alama ya Uatheisti, inayowakilisha ukosefu wa imani kwa miungu

UainishajiKifalsafa
TeolojiaHakuna imani katika miungu au uungu
EneoDuniani kote, hasaUlaya,Amerika ya Kaskazini,Asia ya Mashariki
MwaasisiMatthias Knutzen (anayejulikana wa kwanza)
AsiliKarne ya 17,Ulaya
WafuasiTakriban milioni 450 - 500
ProfesaRichard Dawkins ni mwatheisti mashuhuri wa karne ya 21.

Ukanamungu (pia:Uatheisti kutokaneno laKiyunani cha kale,atheos, likiwa na maana ya "bila miungu") kijumla ni msimamo wa kutokuwa naimani juu wa uwepo wamiungu, ama kukataa imani kuwa kuna miungu, yaani ni dhana kuwa hakunaMungu wala miungu. Hivyo ni kinyume cha Utheisti, imani kuwa angalau kuna Mungu mmoja.

Asili ya neno Uatheisti, limechipuka hata kabla yakarne ya 5, lilitumika kuwakilisha wale wasioamini uwepo wa miungu inayoabudiwa najamii kubwa yawatu, wale waliovunjwa mioyo na miungu, au wale wasioona sababu yoyote ya msingi ya kuamini uwepo wa miungu.

Neno lenyewe uatheisti lilianza kutumika hasa mnamokarne ya 16, baada ya kusambaa kwa fikra huru dhidi yadini.

Watu wa kwanza kujitambulisha kama waatheisti, waliishikarne ya 18 wakati waZama za Mwangaza;mapinduzi ya Ufaransa yalishuhudia vuguvugu kubwa la kisiasa kuwahi kutokea kwenyehistoria, lililotetea ukuu wa fikra za binadamu.

Hoja zinazotetea uatheisti, zimegawanyika kwenye makundi mbalimbali yakiwemo ya kifalsafa, kijamii na kihistoria.

Mantiki ya kutoamini uwepo wa miungu inajumuisha, tatizo lauovu, hoja yafunuo zinazokinzana, na kukataadhana isiyoweza kupingika.

Wasioamini wanadai kuwa uatheisti ndio dhana asili ya binadamu kuliko Utheisti, kwa sababu kila mtu anazaliwa bila kuwa na imani ya Mungu au miungu; kwa maana hiyo basi, nijukumu la anayeamini uwepo wa miungu au Mungu kuthibitisha madai yake na si jukumu la atheisti kuthibitisha kuwa hakuna Mungu au miungu.

Tafiti za zamani kutoka shirika la habari la Uingereza (BBC), zilionyesha kuwa 8% ya watu woteduniani ni waatheisti, huku zile za zamani zaidi zikionyesha kuwa ni 2% pekee, na wale wasiokuwa na dini yoyote wakiunda 12% ya watu wote duniani.

Mwaka2015, tafiti zimeonyesha 61% ya watu waChina walikuwa waatheisti, huku tafiti za mwaka 2010 zikionyesha kuwa 20% ya watu waUmoja wa Ulaya hawaamini uwepo waroho ya aina yoyote wala miungu, hukuUfaransa naUswidi zikiongoza kwaidadi kubwa ya waatheisti, zikiunda 40% na 34% kila mmoja.

Tafsiri na Aina

[hariri |hariri chanzo]

Uatheisti ni dhana inayokanusha uwepo wa miungu. Mara nyingi aina mbili za ukanamungu hutofautishwa ambazo ni:

  • ukanaji unaosema hakuna sababu ya kuamini kuwepo kwa Mungu kwa sababuakili ausayansi zinaweza kueleza kila kitu.
  • ukanaji mkali unaodai ya kwamba kuwepo kwa Mungu hakuwezekani.

Wakanaji mashuhuri wakarne ya 19 walikuwaLudwig Feuerbach,Karl Marx,Friedrich Engels,Arthur Schopenhauer naFriedrich Nietzsche. Wakanaji muhimu katikakarne ya 20 walikuwa kwa mfanoStephen Hawking,Siegmund Freud,Bertrand Russell,Albert Camus,Simone de Beauvoir,Louis de Broglie,Erwin Schrödinger,David Kellogg Lewis,Vladimir Lenin,Paul Dirac,Marlene Dietrich,Albert Einstein,Jean Baptiste Perrin,Mao Zedong,Auguste Comte,Noam Chomsky,Isaac Asimov,James Chadwick,John Lennon,David Attenborough,Michel Foucault,Richard Feynman,Niels Bohr,Douglas Adams,Christopher Hitchens,Daniel Dennett,Richard Dawkins,Sam Harris, naUmberto Eco.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mambo ya dini bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Ukanamungu&oldid=1409472"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp