Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Ufini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Ufini
Suomen tasavalta (Kifini)
Republiken Finland
(Kiswidi)
Wimbo wa taifa: "Maamme" (Kifini)
"Vårt land" (Kiswidi)
("Nchi yetu"Kiswahili)
Eneo la Ufini kati Umoja wa UlayaEneo la Ufini kati Umoja wa Ulaya
Ufini katika duniaUfini katika dunia
Mji mkuu
na mkubwa
Helsinki
Lugha rasmiKifini (84.1%)
Kiswidi (5.1%)
SerikaliBunge laJamhuri
 Rais
Alexander Stubb
Petteri Orpo
  Uhuru
6 Desemba 1917
  Utambuzi wa uhuru
3 Januari 1918
Eneo
  Jumlakm2 338,145(ya ya 64)
  Maji (asilimia)9.4%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2024 5,635,560[1]
  Msongamano18.4/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
  Jumla $351.5 bilioni[2](ya 50)
  Kwa kila mtu $64,660[3] (ya 23)
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
  Jumla $306.08 bilioni (ya 49)[3]
  Kwa kila mtu $54,770[3] (ya 15)
HDI (2022)0.942juu sana
SarafuEuro (€)
Majira ya saaUTC+2 EET
Upande wa magariKulia
Msimbo wa simu+358
Jina la kikoa.fi
Pielinen

Ufini (kwaKifini:Suomi;jina rasmi:Jamhuri ya Ufini) ni nchi yaSkandinavia iliyokoUlaya ya Kaskazini. Imepakana naNorwei upande wakaskazini,Urusi upande wamashariki naUswidi upande wamagharibi. Ng'ambo yaBaltiki ikoEstonia ambayo watu wake hutumialugha iliyo karibu sana naKifini. Inaonekana ya kwamba mababu wa Wafini na Waestonia walihama pamoja wakiwa na lugha ileile zamani, lakini sasa ni lugha mbili kwa sababu hawakuwa namawasiliano kati yao kwa muda mrefu.

Ufini ina idadi ya watu takriban milioni 5.6 namji mkuu wake niHelsinki, ambao pia nimji mkubwa zaidi nchini. Nchi hii inamazingira ya kuvutia yenyemaziwa mengi (takriban 188,000) namisitu mikubwa inayochukua sehemu kubwa ya ardhi yake. Ufini pia hujulikana kwa kuwa namajira ya baridi kali na mchana mfupi wakati wa majira ya baridi kaskazini, huku maeneo yaAktiki yakipata kipindi cha usiku mrefu wa majira ya baridi na mwanga wa saa 24 wakati wamajira ya joto.

Kiutawala, Ufini nijamhuri yakidemokrasia yenye mfumo waserikali yabunge.Rais ni mkuu wa nchi, wakatiwaziri mkuu ndiye mkuu waserikali. Ufini ni mwanachama waUmoja wa Ulaya,Umoja wa Mataifa, Baraza la Nordic, na kuanzia 2023, mwanachama waNATO. Nchi imepata sifa duniani kwa viwango vyake vya juu vyaelimu,haki za binadamu,usawa wakijamii, na ustawi wa wananchi. Ufini pia huchukuliwa kuwa moja ya nchi zenye viwango vya juu vya furaha duniani.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Historia ya awali

[hariri |hariri chanzo]

Ufini ulikaliwa na watu tangu ilipokwishaenzi ya barafu ya mwisho, miaka9000 KK hivi.[4] Wakazi wa kwanza walikuwawawindaji-wakusanyaji ambao walitumia vifaa vyamawe vinavyofanana na vile vyaEstonia,Russia naNorway.

Labdakilimo kilianza miaka3000 KK -2500 KK.[5]

Mwishoni mwakarne ya 13 Ufini ukawa sehemu yaSweden hadimwaka1809, ilipomezwa naUrusi kamaufalme mdogo wenye kujitawala kwa kiasi fulani.

Karne ya 20

[hariri |hariri chanzo]
Carl Gustaf Emil Mannerheim

Mwaka1906, Ufini ulikuwa nchi ya kwanzaduniani kuwapa wananchi wote wenyeumri wautu uzima haki ya kugombeavyeo vyaserikali.[6][7]

Mwaka1917, baada yaMapinduzi ya Russia, Ufini ulijitangaza huru na mwaka uliofuata ukawa jamhuri baada yavita vya wenyewe kwa wenyewe.

Wakati wavita vikuu vya pili,Muungano wa Kisovyeti ulijitahidi kuteka Ufini wote, ukaishia kutwaaKarelia,Salla,Kuusamo,Petsamo navisiwa kadhaa tu.

Baada yavita Ufini uliacha kutegemea kilimo ukajitosa katikauchumi waviwanda[8] hata kufikia kuwa kati yanchi zilizoendelea zaidi[9][10][11][12][13][14][15].

Mwaka1955 Ufini ulijiunga naUmoja wa Mataifa ukichaguasiasa ya kutoambatana na upande wowote.

Mwaka1995 ulijiunga naUmoja wa Ulaya na mwaka1999 ulikubali kutumiaeuro.

Demografia

[hariri |hariri chanzo]
Ufini inajulikana kama "Nchi ya Maziwa Maelfu".[16]

Kuna jumuiya tatu katika Ufini:

  • Wafini wenyewe ambao ni 88.9% ya wakazi wote.
  • Waswidi wako hasa upande wa kusini mwa nchi, kwa jumla ni takriban 5.1% ya wakazi; hasavisiwa vya Aland kuna Waswidi watupu walio na hali ya kujitawala ndani ya Ufini.
  • Wakazi asilia niWasami ambao wako kaskazini tu. Maisha yao yanategemeauwindaji naufugaji; wako wachache, jumla yao haifikii 0.2% ya wakazi wote.

Mbali na hao, kunawahamiaji (11.1%), hasa kutokaRussia, Estonia, Asia (3.8%) naAfrika (1.4%).

Lugha rasmi niKifini naKiswidi. Lugha ya Kifini ina asili yaAsia ya Kati, hivyo haina uhusiano nalugha za Kihindi-Kiulaya.

Wakazi wenye lugha ya Kiswidi wako upande wa kusini mwa nchi kwa sababu Ufini ilitawaliwa na Uswidi kwakarne nyingi. Katika karne hizo walikuwepo Waswidi waliohamia Ufini lakini kuna pia Wafini walioanza kutumia Kiswidi pekee. Hasa kwenye visiwa vya Aland Kiswidi ni lugha pekee. Lakini Waswidi wa Ufini wanajisikia Wafini.

Upande wadini, 62.2% niWalutheri, 1%Waorthodoksi na 1% Wakristo wengine.Madhehebu makuu mawili yaUkristo yanatambulika na kupewa nafasi katika matukio mbalimbali nashuleni. 2% wanafuata dini au madhehebu mengine, wakati 34.9% hawana dini yoyote.

Watu maarufu

[hariri |hariri chanzo]

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. "Finland population 2024". 2024.
  2. IMF."Plt ya Ufini" (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo2025-02-20.
  3. 123Hitilafu ya kutaja: Invalid<ref> tag; no text was provided for refs namedauto1
  4. Georg Haggren, Petri Halinen, Mika Lavento, Sami Raninen and Anna Wessman (2015).Muinaisuutemme jäljet. Helsinki: Gaudeamus. uk. 23.ISBN 978-952-495-363-4.{{cite book}}: CS1 maint: multiple names: authors list (link)
  5. Georg Haggren, Petri Halinen, Mika Lavento, Sami Raninen ja Anna Wessman (2015).Muinaisuutemme jäljet. Helsinki: Gaudeamus. uk. 339.ISBN 9789524953634.{{cite book}}: CS1 maint: multiple names: authors list (link)
  6. Parliament of Finland."History of the Finnish Parliament".eduskunta.fi. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2014-09-26. Iliwekwa mnamo2018-02-20.
  7. Finland was the first nation in the world to give all (adult) citizens full suffrage, in other words the right to vote and to run for office, in 1906. New Zealand was the first country in the world to grant all (adult) citizens the right to vote, in 1893. But women did not get the right to run for the New Zealand legislature, until 1919.
  8. "Finland". International Monetary Fund. Iliwekwa mnamo17 Aprili 2013.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  9. "Finland: World Audit Democracy Profile".WorldAudit.org. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 30 Oktoba 2013.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  10. "Tertiary education graduation rates—Education: Key Tables from OECD". OECD iLibrary. 14 Juni 2010.doi:10.1787/20755120-table1. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2011-04-30. Iliwekwa mnamo6 Machi 2011.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  11. "Her er verdens mest konkurransedyktige land—Makro og politikk". E24.no. 9 Septemba 2010. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 14 Oktoba 2010. Iliwekwa mnamo6 Machi 2011.{{cite web}}:Unknown parameter|deadurl= ignored (|url-status= suggested) (help)
  12. "The 2009 Legatum Prosperity Index". Prosperity.com. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 29 Oktoba 2009. Iliwekwa mnamo4 Februari 2010.{{cite web}}:Unknown parameter|deadurl= ignored (|url-status= suggested) (help)CS1 maint: date auto-translated (link)
  13. "Human Capital Report 2015".World Economic Forum. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2017-12-03. Iliwekwa mnamo15 Mei 2015.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  14. "Fragile States Index 2016". Fundforpeace.org. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 4 Februari 2017. Iliwekwa mnamo27 Novemba 2016.{{cite web}}:Unknown parameter|deadurl= ignored (|url-status= suggested) (help)
  15. Gender Gap Report(PDF). WEF.
  16. Li, Leslie (1989-04-16)."A Land of a Thousand Lakes".The New York Times (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo2021-12-29.

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons


Nchi zaUmoja wa UlayaBendera ya Umoja wa Ulaya
Austria |Bulgaria |Eire |Estonia |Hispania |Hungaria |Italia |Kroatia |Kupro |Latvia |Lituanya |Luxemburg |Malta |Polandi |Slovakia |Slovenia |Romania |Ubelgiji |Ucheki |Udeni |Ufaransa |Ufini |Ugiriki |Uholanzi |Ujerumani |Ureno |Uswidi
Nchi huru
Nchi zisizokubaliwa
na umma wa kimataifa
Maeneo yanayojitawala
chini ya nchi nyingine
1 nchi yaAsia ya Magharibi kijiografia ambayo huhesabiwa kuwa sehemu yaUlaya kiutamaduni2nchi ya kimabara
Makala hii kuhusu maeneo yaUlaya bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuUfini kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Ufini&oldid=1454734"
Jamii:
Jamii zilizofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp