Muhammad Ahmad Al-Mahdi alifaulu kukusanya wafuasi wengi na kushinda Wamisri. Tarehe26 Januari1885 jeshi lake lilitwaa mji mkuuKhartum na kumwua gavanaGordon Pasha.
Al-Mahdi alianzisha mji mkuu mpya ng'ambo ya mto Nile kwa kuundaOmdurman. Wamisri na Waingereza wakatoka nje ya Sudan.
Ugomvi ulitokea kati ya makamu wake hadi1891 wakatiAbdallahi ibn Muhammad mwenye sifa ya kuwa aliongoza jeshi la mahdi wakati wa mashambulio dhidi ya Khartum alikubaliwa wa viongozi wa mahdiyya akajiita "khalifa".
Khalifa Abdullahi aliimarisha utawala wake wa kuwaua wapinzani bila neema, kati yao wanafunzi na ndugu za mahdi mwenyewe. Akajenga jumba mjini Omdurman linalosimama hadi leo.
Khalifa Abdullahi alijaribu kutumia teknolojia mbalimbali. Akanunua meli za mvuke za mtoni alizoziona Waingereza walizitumia pia akajenga kiwanda cha kutengenezea bunduki. Akaanzisha nyaya za mawasilaino kwa simu. Lakini kwa ujumla vita na utawala wa mahdiyya zilikuwa ziliharubu uchumi iliyoendelea kuzorota.
Khalifa alifaulu kupanua utawala wake juu ya maeneo karibu yote ya Sudan ya leo lakini alishindwa kufikiajimbo la Ikweta ambakoEmin Pasha aliendelea kutetea mabaki ya Sudani ya Kimisri.
Jeshi la Mahdiyya
Itikadi ya kupanua utawala wa mahdiyya kwa njia yajihad ilimsababisha khalifa kushambulia nchi jirani yaEthiopia iliyotawaliwa nakaisari wa Kikristo. Mwaka 1887 akaongoza jeshi la askari 60,000 hadiGondar. Waethiopia wakajibu kwa kushambulia Sudan mwaka 1889. Kifo cha KaisariYohane IV katika mapigano yaMetemma tarehe9 Machi 1889 ililazimisha Waethiopia kurudi kwao. Lakini jeshi la mahdiyya lilipoteza wanajeshi wengi pia likadhoofika.
Wakati huohuo jemadari wa khalifa Abd ar-Raħmān an-Nujumī alishambulia Misri lakini alishindwa kwenye mapigano ya Tushkah. Hii ilikuwa mara ya kwanza ya jeshi la mahdiyya kushindwa.
Majaribio ya vita za jihadi dhidi yaWabelgiji katika jimbo la Ikweta na dhidi yaWaitalia katika Eritrea yalishindikana pia.
Mapigano ya Omdurman 2 Septemba 1898
Mwaka1895 mkuu wa jeshi la pamoja la Misri na Uingereza, jeneraliHoratio Kitchener aliamua kulipizakisasi kwa vita ya 1885 akaongoza jeshi kubwa dhidi ya Sudan. Kwa kutumia meli za mvuke kwenye mto Nile na kujenga reli akasongea mbele hadi Omdurman.
Tarehe2 Septemba1898 jeshi la mahdiyya lilishindwa kabisa katika mapigano ya masaa matano. Safari hiyo Waingereza waliandaliwa vizuri zaidi, pia silaha mpya kamabunduki ya mtombo ziliwapa ushindi. Upande wa khalifa walikufaaskari 11,000, upande wa Waingereza na Wamisri watu 400 pekee.
Khalifa mwenyewe alitoroka akajenga jeshi upya na kutawala kusini mwa Sudan, lakini akauawa mwaka1899 katika mapigano yaUmm Diwaykarat.
Hivyo Waingereza walitawala Sudan pamoja na Misri hadi 1956, na Kitchener akawa gavana mkuu wa kwanza.
Baada ya Uhuru
Ramani ya siasa ya Sudan kabla ya Sudan Kusini kujitenga.
Baada yauhuru wa nchi (1956), makabila ya kusini, ambayo hayakukubali kusilimishwa, yalipiganiavita ndefu hadi kupata uhuru wao.
Darfur ni eneo lenye majimbo matatu ambayo imeathiriwa na vita vya kisiasa,vita vya Darfur.
Kutokana na vita nyingiserikali hazikuwa imara na kulikuwa na mabadiliko ya mara kwa mara baada ya uhuru.Mapinduzi ya kijeshi ya kwanza yalitokea mwaka1958, kishajeneraliIbrahim Abboud alitawala hadi1964 wakati alipopaswa kujiuzulu kutokana na upanuzi wa vita katika Sudan Kusini na upinzani wa wananchi kwenye mji mkuu.
Utawala wa Nimeiry
Kilichofuata kilikuwa kipindi cha serikali 3 za kiraia hadi1969. Tarehe25 Mei1969jeshi, chini yakanaliGaafar Nimeiry, lilipindua tena serikali. Nimeiry alikuwawaziri mkuu, wakatibunge na vyama vyote vilipigwa marufuku. Nimeiry alitawala hadi1985, na tangu1971 alikuwa rais. Mwaka1972 alifaulu kumaliza awamu ya kwanza ya vita ya wenyewe kwa wenyewe dhidi ya Sudan Kusini kwamapatano ya Addis Ababa. Sudan Kusini ilipewamamlaka ya kujitawala katika mambo ya ndani chini ya serikali ya kieneo.
Mwanzoni Nimeiry alijaribu kuigasiasa yaGamal Abdel Nasser nchini Misri na kutekeleza sera kadhaa zaujamaa.Utawala wake uliona upinzani kutoka kwaWakomunisti na pia kutokaWaislamu wenyeitikadi kali. Baada ya kupinduliwa kwa siku kadhaa na Wakomunisti alivunja ushirikiano naUrusi na kuanza kupokeawanasiasa wenye mwelekeo wa Uislamu mkali katika serikali yake.
Tangumiaka ya 1980 alisogea zaidi upande wa Uislamu wa kisiasa. Mwaka1983 alitangazasharia kuwamsingi washeria zote na kubadilisha sheria zajinai ipasavyo. Hatua hii ilisababisha upinzani katika sehemu za nchi zisizokaliwa na Waislamu. Alivunja pia serikali ya kieneo kwa Sudan Kusini na hivyo vita ya wenyewe kwa wenywewe ilianza upya.
Nimeiry alitangaza hali ya dharura iliyompa tena mamlaka zakidikteta. Mwaka1985 aliruhusu kunyongwa kwamwanafalsafa MwislamuMahmoud Mohammed Taha kwa kosa la "uasi dhidi ya Uislamu". Miezi minne baadaye Nimeiry alipinduliwa kwenye mwaka huohuo.
Utawala wa Bashir
Sudan ilirudi kwa miaka michache chini yaserikali ya kiraia. Mapinduzi yaliyofuata mwaka1989 yalileta utawala wa jeneraliOmar al-Bashir. Vita ya wenyewe kwa wenye iliendelea hadi mwaka2005 ikamalizika kwaMapatano ya Naivasha baina ya Sudan naSPLA. Sudan Kusini ilipewa miaka hadi2011 kujitawala halafu kuwa na kura ya wananchi wa kusini kuhusu uhuru uliotangazwa mwaka uleule.
Tangu mwaka 2003 Bashir alisimamia pia vita ya jeshi lake nawanamgambo dhidi ya wakazi wasioWaarabu waDarfur waliopinga utawala wake.
Tarehe11 Aprili2019 Bashir alipinduliwa na jeshi lake baada yawiki kadhaa zamaandamano ya wananchi wa Khartum namiji mingine dhidi yake. Kupinduliwa kwake pamoja na kipindi chaserikali ya mpito ya kijeshi vilitangazwa na waziri wa ulinzi, jenerali Awad Mohammed Ibn Auf. Ilhali waandamanaji waliendelea kupinga serikali ya kijeshi, Ibn Auf alijiuzulu tarehe12 Aprili na siku iliyofuata, tarehe 13 Aprili, jeneraliAbdel Fattah Burhan alitangaza wanajeshi wanatafuta ushirikiano wa karibu na wapinzani wa utawala wa awali[1].
Watu na makabila
Kadiri yasensa za mwaka2008, wakazi walihesabiwa kuwa zaidi yamilioni 21.6.
Umma wa miji kama Khartoum (pamoja naOmdurman, na Khartoum ya kaskazini) waongezeka zaidi: umma wa miji hiyo yakadiriwa milioni 6-7 na wengine wahamiaji milioni 2 ambao wamekimbia vita vya kusini, magharibi, mashariki na pia wengine kwa sababu yaukame.
Sudan ina aina mbili zautamaduni —Waafrika walio na Uarabu na Waafrika wasio Waarabu — namaelfu yamakabila na migao ya kabila,lugha tofautitofauti kwa makundi au kabila – migawanyiko hii uleta siasa za utengo naubaguzi.
Majimbo ya Kaskazini hasa ndio makubwa nchini Sudan, na pia miji mikubwa iko katika majimbo haya. Zaidi ya milioni 22 wanaoishi katika majimbo haya ni Waislamu-Waarabu na wanaongeaKiarabu, lakini wengi pia huongealugha 70 za kikabila hasaKinubi,Kibeja,Kifur,Kinuban,Kiingessana, kwa kikundi hiki kuna wale wavutia zaidi kama: Wa-Kababish kutoka Kordofan kaskazini, watu hawa wanaofugangamia; Ga’alin (الجعلين), Rubatab (الرباطاب),Manasir (المناصير) and Shaiqiyah (الشايقيّة); makabila ambao makao yao ni karibu na mito ni kama Baggara waKurdufan naDarfur; WakihamBeja eneo ya bahari ya Shamu na Wanubi wa Nile kaskazini, ambao wengine wamehamishwa karibu na mto Atbara. Eneo la Shokrya kwa Wabutana, Wabataheen wamepakana na Waga’alin na Washorya, upande wa kusini-magharibi eneo ya Butana. Pia kuna Warufaa, Wahalaween na makabila mengine mingi eneo la Gazeera na kwa ufuo wa Bluu Nile na eneo ya Dindir. Hata Wanubi kusini mwa eneo la Kurdufan na Wafur upande wa magharibi.
Makala hii kuhusu maeneo yaAfrika bado nimbegu. Je unajua kitu kuhusuSudan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.