Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Solomoni

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Solomoni namalkia wa Saba (mchoro waKonrad Witz, alias Conradus Sapientis,1434-1435).

Mfalme Solomoni kadiri yaBiblia alikuwa mfalme wa tatu na wa mwisho waIsraeli nzima, akitawala kuanzia970 KK hadi930 KK hivi.

Maisha yake

[hariri |hariri chanzo]
Solomoni katikaikulu yake (kadiri yaIngobertus,880 hivi).

Alikuwa mwana waDaudi na Bath-Sheba (Betsheba), aliyewahi kuwamke waUria Mhiti.

Daudi alimchagua kuwa mrithi wake kwa sababu alikuwa uthibitisho hai wamsamaha aliopewa naMungu kwakuzini na hatimaye kumuua Uria.

Ufalme wake ulitazamwa naWayahudi kuwa na ustawi usio na mfano, kutokana nahekima yake naamani iliyopatikana wakati wote wa utawala wake.

Ufalme wake uliweza kustawi kuliko ule wa baba yake kutokana na msingi imara aliouweka Daudi. Lakini mwenyewe aliudhoofisha na kusababisha mara baada ya kifo chake utokee utengano kati ya makabila ya Kaskazini na yale ya Kusini.

Kati ya kazi muhimu alizozifanya, mojawapo ni kujengahekalu la Yerusalemu na kuliweka wakfu kwa sherehe kubwa ya siku saba, ambapo Mungu alionyesha kibali chake kwa kulijaza kwa sura ya wingu (1Fal 8). Polepolehekalu hilo likaja kuwa la pekee hatapatakatifu pengine pote pakakatazwa chini ya mfalmeYosia.

Ingawa Solomoni anasifiwa kwahekima yake, alishindwa kukwepamajivuno natamaa, akataka kuwapendeza wake zake waliokuwa 700 (mbali na masuria 300), wengi waoWapagani, hata akawajengea mahali pa kuabudia miungu yao akamchukiza Mungu hata akamtabiria mtoto wake atanyang’anywa sehemu kubwa ya ufalme (1Fal 11:1-13) ikawa hivyo.

Hata hivyo mwishoni aliweza kulaumiwa kwa kuzidisha fahari, hasa upande wa wanawake waliomvuta kwenda kinyume chaimani yaMungu pekee.

Sala zake

[hariri |hariri chanzo]

"Nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako,na kupambanua mema na mabaya;maana ni nani awezaye kuwahukumu hawa watu wako walio wengi"? (1Fal 3:9)

"Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe,mbinguni juu wala duniani chini!Ushikaye maagano na rehema kwa watumishi wako,waendao mbele zako kwa mioyo yao yote". (1Fal 8:23)

Baada ya kifo chake

[hariri |hariri chanzo]

Kwa sababu hiyo, ufalme ulivunjika pande mbili mara baada ya kifo chake.

Hata hivyo, Wayahudi waliendelea kumuona kama kielelezo cha hekima, wakaandika vitabu kwa kutumia jina lake au kwa kujifananisha naye.

Yesu alijitangaza kuwa mkuu na mwenye hekima kuliko Solomoni.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Solomoni&oldid=1304390"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp