Mji uko upande wa magharibi wa Bulgaria kando lamto Iskar mbele yamilima ya Vitosha inayofikia kimo cha mita 2286 . Ni kitovu cha kisiasa, kiuchumi na kiutamaduni wa nchi.
Sofia ni mji wa kale mianzo yake ni katikakarne ya 7 KK. Wakati wa Dola la Roma ilijulikana kwa jina "Serdica" au "Sardica".
Tangu mwaka 809 BK ilikuwa sehemu ya milki ya Bulgaria ikaitwa "Sredec". Jina la Sofia limetumiwa tangu 1329. Asili yake ni katika kanisa la Mt. Sofia (yaani: Hekima takatifu ya Mungu).
Mji ulirudi nyuma chini ya utawala wamilki ya Osmani ulipotwaliwa na jeshi la Kirusi mwaka 1878 ulikuwa na wakazi 20,000 pekee.
Bunge la kwanza la Bulgaria tar.22 Machi1879 likatangaza Sofia kuwa mji mkuu wa Bulgaria. Mji ikakua ikafikia lakhi mwaka 1910 na lakhi tatu mwaka 1939.
Baada yavita kuu ya pili ya dunia idadi ya wakazi ikaendelea kupanda hadi kupita milioni mnamo 1975.
Wakazi walio wengi ni Wakristo Waorthodoksi. Kuna pia Waislamu na Wayahudi.
Kanisa la Mt. George limejengwa zamani za Dola la Roma
Nyumba ya maagizo ya taifa
Makala hii kuhusu maeneo yaUlaya bado nimbegu. Je unajua kitu kuhusuSofia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.