Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Siberia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Eneo la Siberia: nyekundu yote; Jimbo la Siberia ndani ya shirikisho la Urusi: nyekundu nyeusi.

Siberia (kwaKirusi: Сиби́рь,Sibir; kwaKitartari: Seber) ni eneo kubwamashariki mwaUrusi. Ni zaidi yanusu ya eneo la Urusi wote. Eneo lake lote nikilomita za mrabamilioni 9.6 ambayo ni karibu sawa naUlaya yote (km² milioni 10.6).

Maana ya Siberia

[hariri |hariri chanzo]

Kuna namna mbalimbali ya kutaja mipaka ya "Siberia".

Mipaka ya Siberia ya kijiografia ni safu yamilima ya Ural upande wamagharibi,bahari ya Aktika kwakaskazini,Pasifiki katika Mashariki na nchi zaKazakhstan,Mongolia naUchina upande wakusini.

Wakazi

[hariri |hariri chanzo]

Idadi ya wakazi ni ndogo: kuna milioni 23 pekee. Walio wengi niWarusi (79%) wanaoishi mjini. Wakazi asilia (21%) ni vikundi vingi vidogo; walio wengi ni wasemaji walugha za Kiturki.Utamaduni wao ulikuwauwindaji naufugaji lakini sasa ni wachache tu wanaoendelea hivyo.

Hali ya hewa

[hariri |hariri chanzo]

Hali ya hewa ya Siberia ni kali sana.Kipindi cha joto kinajoto kali hadi +40°C, lakinikipindi cha baridihalijoto hushuka chini hadi -67 °C.Kijiji chaOymyakon (katika jamhuri yaSakha) ni mahali baridi duniani; -71.2 °C zilipimwa hapa.

Kipindi cha baridi ni kirefu, kipindi cha joto ni kifupi. Sehemu kubwa ya Siberia inafunikwa natheluji kwa muda wa miezi tisa kilamwaka. Hivyokilimo kinawezekana katika kanda nyembamba la kusini. Sehemu kubwa nchi imefunikwa namisitu. Lakini maeneo baridi sana ya kaskazini hapanamiti tena, nimanyasi namajani tu.

Mito na maziwa

[hariri |hariri chanzo]

Siberia inamito mingi mikubwa. Lakini huganda kabisa wakati wa baridi, yaani kwa sehemu kubwa wa mwaka isipokuwa ile katika kusini.

Makala hii kuhusu maeneo yaUrusi bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuSiberia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Siberia&oldid=1091653"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp