Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Raphael

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Raphael alivyojichora.

Raffaello Sanzio (kwaKiitalia huitwa piaRaffaello da Urbino; kwaKiingereza anajulikana kamaRaffael auRaphael) (6 Aprili1483 -6 Aprili1520) alikuwamchoraji namjenzi kutokaItalia.

Pamoja naLeonardo da Vinci naMichelangelo huhesabiwa kati yawasanii muhimu wazama ya mwamko ya Italia.

Maisha

[hariri |hariri chanzo]

Raphael alizaliwamjiniUrbino kamamtoto wa mchorajiGiovanni Santi aliyefanyakazi katikautumishi wamkabailaFederiko III wa Montefeltro.

Katikaumri wa miaka 15 alikuwamwanafunzi katikakarakana ya mchorajiPietro Perugino aliyeshiriki katika kazi za kupambaKikanisa cha Sistina kwenyeVatikano.

Raphael alijifunza haraka na tangu mwaka1500, alipokuwa na umri wa miaka 17, alipewa kazi za kwanza za kujitegemea.

Alianza kuchorapicha katika makanisa yamiji mbalimbali ya Italia.

Alipenda kutembeleaFirenze akitazama michoro yawalimu wa kale.

Tangu alipohamiaRoma, alikoitwa naPapa Julius II, kazi kubwa aliyopewa ilikuwapicha za ukutani kwenye vyumba vyaPapa mwenyewe.

Raphael aliagadunia mapema katika umri wa miaka 37.Hakuoa wala hakunawatoto waliojulikana.

Upande wadini, alikuwaMkristo waKanisa Katoliki, tena mwanachama waUtawa wa Tatu wa Mt. Fransisko.

Michoro yake

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mtu huyo bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuRaphael kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Raphael&oldid=1279378"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp