Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Primata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Primata
Nyani wa kawaida, kima wa Dunia ya Kale
Nyani wa kawaida,kima wa Dunia ya Kale
Uainishaji wa kisayansi
Domeni:Eukaryota
Himaya:Animalia(Wanyama)
Faila:Chordata(Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli:Mamalia(wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda:Primates(Wanyama wanaofanana kiasi na binadamu)
Linnaeus, 1758
Ngazi za chini

Nusuoda 2, oda za chini 4:

Primata nijina la kitaalamu lakundi takribanspishi 400 zamamalia wanaojumlishalemuri,nyani nasokwe wote pamoja nabinadamu.

Wote huwa namikono yenyevidole 5 nakucha na wanafanana na binadamu kwa namna fulani katika mengine kadhaa. Tofauti muhimu nilugha.

Wanahesabiwa kuwa na vikundi aunusuoda 2:

  1. Haplorhini (wenyepua kavu) ni pamoja na nyani, sokwe na binadamu.
  2. Strepsirhini (wenye pua bichi) nilemuri,komba naAye-Aye.

Uenezi

[hariri |hariri chanzo]

Binadamu pekee amesambaa koteduniani.

Primata wengine wanaishi hasa katika maeneo yatropiki nanusutropiki yaAfrika naAsia.Barani Afrika wako kote naidadi kubwa ya spishi wakokusini kwa Sahara. KatikaAmerika wako kati yaMeksiko naArjentina yakaskazini. HawakoUlaya isipokuwa kundi moja hukoGibraltar (kusini mwarasi ya Iberia) lakini inawezekana hao walipelekwa huko na binadamu. Vilevile hawakoAsia ya Kaskazini naya Kati,Australia navisiwa vyaPasifiki wala maeneo karibu nancha za dunia.

Tabia

[hariri |hariri chanzo]

Tabia zifuatazo zinapatikana

  • mikono inafaa kwa kushika
  • kucha ni bapa, ni kucha kali za kuchimba au za kujitetea; huwa na vifinyo kwenye vidole
  • miguu ni muhimu zaidi kwa kutembea
  • uwezo wa kunusa ni mkali sana, na hafifu zaidi kwa primates wanaofanya shughuli zao mchana
  • macho ni makubwa na yote mawili yanatazama mbele, uwezo wa kuona ni wa juu
  • wanazaawatoto wachache kila safari,mimba na kipindi cha kunyonyesha wadogo huchukuamuda mrefu zaidi kuliko mamalia wengine wenye ukubwa sawa
  • ubongo ni mkubwa kulingana na mamalia wengine
  • meno ya magego si zaidi ya matatu, machonge mawili na magego madogo matatu

Ukubwa

[hariri |hariri chanzo]

Wale wa nusuoda Strepsirhini kwa jumla ni wadogo kuliko Haplorhini.

Aina ndogo zaidi kati ya primata niLemuri-panya ya Berthe mwenyeurefu wasentimita 10 pekee nauzito wagramu 38. Aina kubwa ningagi (gorilla) yenyekilogramu hadi 275,

Spishi kadhaa wana tofauti kubwa kati yadume najike; dume wa spishi hizo wanaweza kuwa na uzito mara mbili kuliko jike na pia kuonyesharangi tofauti kama nyani waPapio hamadryas.

Viungo vya mwili

[hariri |hariri chanzo]

Primata wengi hukaliamiti naviungo vyao vinalingana namaisha yao. Kwa spishi nyingi miguu ni mikubwa na yenyenguvu zaidi kuliko mikono, isipokuwaGiboni waAsia Kusini-Mashariki na sokwe wakubwa wasio binadamu.

Katika spishi zinazotembea mtini kwa kuning’inia kwa mikonokidole gumba kimefifia.

Mkia ni muhimu kwa primata wengi wanaoishi mtini lakini spishi nyingine wana mkia mdogo au hawana. Nyani kadhaa waAmerika wana mkia wa kushikilia usio na nywele upande wa chini wenyeneva muhimu.

Manyoya

[hariri |hariri chanzo]

Mwili wa primata wengi umefunikwa nanywele zenye rangi baina yanyeupe,kijivu,kahawia hadinyeusi. Viganja kwa kawaida havina nywele. Spishi kadhaa hazina nyweleusoni. Binadamu ni spishi yenye nywele chache.

Makazi

[hariri |hariri chanzo]

Inaaminiwa kuwa primata kiasili waliishi mtini na hadi leo wengine wana maisha yao mtini pekee ambao hawatembei ardhini. Wengine wanaishi chini na juu pia. Wanaotembea kwenye uso wa ardhi pekee ni wachache pamoja na binadamu.

Primata wanapatikana kwenye aina mbalimbali zamisitu kama vilemsitu wa mvua,mikoko na pia kwenye misitu yamlimani hadikimo chamita 3000juu ya UB.

Spishi nyingine zinaogopamaji lakini kuna pia aina zinazopenda maji zinajua hata kuogelea. Spishi kadhaa zimezoeamazingira ya binadamu zinazoishi kwenyevijiji namiji kama makaka waUhindi.

Kimsingi strepsirhini (wenye pua bichi) wanafanya shughuli zao wakati wausiku na kulalamchana lakini haplorhini (wenye pua kavu) wanafanya shughuli zao machana na kulala usiku. Wale wanaofanya shughuli zao usiku kwa jumla ni wadogo zaidi na wana uwezo mzuri zaidi wa kunusu.

Sawa na mamalia wengine wale wanaokula hasamajani wanapumzika muda mrefu zaidi wakihitaji muda mrefu kumeng'enyachakula chao.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Primata&oldid=1267149"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp