Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Polandi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Polandi
Rzeczpospolita Polska (Kipolandi)
Wimbo wa taifa: "Mazurek Dąbrowskiego" ("Poland Is Not Yet Lost")
Polandi katika duniaPolandi katika dunia
Mji mkuu
na mkubwa
Warsaw
Lugha rasmiKipolandi
Kabila (2021)98.8% Wapoli (2021)
SerikaliJamhuri ya kisemi-urais wa umoja
 Rais
Andrzej Duda
Donald Tusk
  Uduchi wa Polandi
Karne ya 10 (takriban 960)
  Ubatizo wa Polandi
14 Aprili 966
Eneo
  Jumlakm2 312,696(ya 69)
  Maji (asilimia)1.48%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2022 38,036,118
  Msongamano122/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2025
  Jumla $1.992 Trilioni(ya 19)
  Kwa kila mtu $54,498 (ya 37)
PLT (Kawaida)Kadirio la 2025
  Jumla $915 Bilioni
  Kwa kila mtu $25,041 (ya 45)
HDI (2022)0.881juu sana
SarafuZłoty (PLN)
Majira ya saaUTC+1 CET / +2 CEST
Upande wa magariKulia
Msimbo wa simu+48
Jina la kikoa.pl

Polandi (kwaKipolandi:Polska) ni nchi yaUlaya ya Kati. Imepakana naUjerumani upande wamagharibi,Ucheki naSlovakia upande wakusini,Ukraini naBelarusi upande wamashariki naBahari ya Baltiki,Lituanya naUrusi (mkoa waKaliningrad Oblast) upande wakaskazini. Polandi ina watu takriban milioni 38 na kuwa nchi ya 42 kubwa kwa idadi ya watu. Mji mkuu na mkubwa niWarsaw.

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Ardhi ya Polandi ni tupu tu kufikia kiasi chaBahari ya Baltiki katika upande wa kaskazini mwaMilima ya Carpathi kusini mwa nchi. Ndani ya eneo hilo lililo tupu, ardhi inatofautiana kutoka mashariki na magharibi.

Pwani ya Kipolandi ya Bahari ya Baltiki ni murua zaidi, lakini inabandari asilia katikamkoa waTrójmiasto:Gdańsk,Gdynia naSzczecin huko mashariki-magharibi ya mbali. Pwani hiyo inaupepo mzuri na maeneo kadhaa ya pwani za maziwa. Pwani za maziwa na fukwe za zamani ambazo zimekatwa kutokabaharini. Sehemu hizi pia huitwarasi.Rasi ya Szczecin ipo upande wa mashariki mwa mpaka wa nchi yaUjerumani.Rasi ya Vistula ipo upande wa mashariki mwa mpaka wa mji waKaliningrad, ambao ni katika mkoa waUrusi.

Mto mrefu zaidi nchini Polandi niVistula, unaoangukia ndani ya Rasi ya Vistula na pia unakwenda moja kwa moja hadi katika Bahari ya Baltiki. Nikm 1064 kutokachanzo hadimdomo.

Kanda ya kaskazini-mashariki ni miti tu imejaa, inakosa watu wachache narasilimali za kilimo na viwanda. Kanda ya kijografia inawilaya nne za vilima vya moraine na maziwa yaliyotengenezwa na moraine. Haya yalianzishwa baada yaPleistoceneZama za Barafu. Ziwa Masurian ni miongoni mwa maziwa manne ya wilaya yaliyochukua eneo kubwa la kaskazini-mashariki mwa Polandi.

Polandi ina maziwa kibao. KwaUlaya nzima,Finland peke yake ina maziwa mengi zaidi. Maziwa makubwa ni "Śniardwy" na "Mamry". Kwa kuongeza katika wilaya ya ziwa katika kaskazini, kuna idadi kubwa pia ya mlima maziwa katikamilima ya Tatra.

Kusini mwa kanda ya kaskazini-mashariki mwa mikoa yaSilesia naMasovia, ambapo kuna alama za mto na mabonde yazama za barafu. Mkoa wa Silesia una rasilimali nyingi na watu wengi. Kunamakaa ya mawe tele.Silesia ya Chini inamgodi washaba mkubwa kabisa.Tambarare ya Masovian ipo kati ya Polandi. Ipo katika mabonde ya mito mikubwa mitatu: Vistula,Bug naNarew.

Ukiendelea na safari kusini ni mlima ya kanda ya Kipolandi. Milima hiyo ni pamoja naSudetes naMilima ya Carpathi. Sehemu ndefu yaCarpathia ni milima ya Tatra ambayo imekwenda hadi kusini mwa mpaka wa nchi ya Polandi.

Mlima mrefu zaidi nchini Polandi unaitwa "Rysy" wenyem 2,503 (ft 8,210), upo Tatras.

Historia

[hariri |hariri chanzo]
Ramani ya Polandi chini yaMieszko I, mwanzilishi wa taifa (960–992).
Shirikisho la Warsaw katika kilele cha uenezi wake (1635).

Waslavi walienea kati nchi katikanusu ya pili yakarne ya 5BK.

Ukristo waKikatoliki kupokewa namfalmeMieszko I (960-992) na Wapolandi kwa jumla (966) hutazamiwa kama chanzo chataifa lao la pekee katikajamii ya Waslavi.

Nchi ilistawi na kuenea hasa chini yaukoo waJageloni (13861572).

Polandi-Lituanya

[hariri |hariri chanzo]

Katika miaka ya15691795 Polandi iliunganishwa naLituanya katikashirikisho la kifalme. Mfalme wa Polandi alikuwa pia mtawala wa Lithuania, na tangumapatano ya Lublin nchi hizo mbili zilikuwa nabunge la pamoja, lakini kila sehemu iliendelea nasheria zake najeshi la pekee. Bunge la pamoja lililokuwa hasa mkutano wamakabaila wote lilikuwa namamlaka ya kumchagua mfalme likapata ushawishi mkubwa.

Wagombea wa ufalme waliachana na mamlaka za kifalme wakijaribu kupatakura nyingi za wabunge na hivyo nguvu ya dola ilififia.

Ugawaji wa Polandi kati ya nchi jirani

[hariri |hariri chanzo]

Mwaka1764 nchi ilianza kurudi nyuma na zile za jirani, yaani Urusi, Austria na Prussia, ziligawana kwa awamu tatu (1772,1793,1795) eneo lake lote. Yaani kuanzia mwaka1772 majirani hayo matatu ya Polandi yalivamia shirikisho na kugawana maeneo yake. Kufikia mwaka1795 maeneo yote yalikwisha kugawiwa kati ya majirani hao.

Wapolandi walijaribu mara kadhaa kujikomboa, lakini walipatauhuru kwa muda tu (1807-1815 na1918-1939).

Baada yavita vikuu vya pili, Polandi ikawa chini ya utawala waKikomunisti hadi ilipofaulu kujikomboa (1989).

Polandi imekuwa nchi mwanachama waUmoja wa Ulaya tangu tarehe1 Mei2004.

Watu

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi ni 38,483,957, karibu wote wakiwaWapolandi asili (93.52%), wakiongeaKipolandi na wakifuataUkristo katikaKanisa Katoliki (87.5%), tena kwabidii ya pekee.

Kati yalugha nyingine zilizotambulika kisheria, zinaongozaKikashubi naKijerumani, halafuKibelarusi na,Kiukraini. Kati yalugha za kigeni zinaongozaKiingereza naKirusi.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]

    Viungo vya nje

    [hariri |hariri chanzo]

    Kurasa za taasisi za serikali

    [hariri |hariri chanzo]

    Utalii Polandi

    [hariri |hariri chanzo]

    Kurasa mtandaoni juu ya Polandi

    [hariri |hariri chanzo]

    Habari za Polandi kwa Kiingereza

    [hariri |hariri chanzo]
    Nchi huru
    Nchi zisizokubaliwa
    na umma wa kimataifa
    Maeneo yanayojitawala
    chini ya nchi nyingine
    1 nchi yaAsia ya Magharibi kijiografia ambayo huhesabiwa kuwa sehemu yaUlaya kiutamaduni2nchi ya kimabara


    Nchi zaUmoja wa UlayaBendera ya Umoja wa Ulaya
    Austria |Bulgaria |Eire |Estonia |Hispania |Hungaria |Italia |Kroatia |Kupro |Latvia |Lituanya |Luxemburg |Malta |Polandi |Slovakia |Slovenia |Romania |Ubelgiji |Ucheki |Udeni |Ufaransa |Ufini |Ugiriki |Uholanzi |Ujerumani |Ureno |Uswidi
    Makala hii kuhusu maeneo yaPolandi bado nimbegu.
    Je unajua kitu kuhusuPolandi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
    Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
    Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
    Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Polandi&oldid=1454735"
    Jamii:
    Jamii iliofichwa:

    [8]ページ先頭

    ©2009-2025 Movatter.jp