Baada yauvamizi wa Waarabu Ujaemi wkatawaliwa kwa muda kama sehemu yaukhalifa wa Uislamu lakini baada yakarne kadhaa nasaba za kieneo zilichukuautawala kwa jina lakhalifa ila hali halisi kama watawala wa kujitegemea.
Baada ya uvamizi waWamongolia nasaba ya wana waTimur iliunganisha Uajemi pamoja na Afghanistan na Asia ya Kati.
Uhusiano nanchi za magharibi, na hasaMarekani, umekuwa mgumu tangumapinduzi, hasa baada ya wanafunzi Waajemi kushambuliaubalozi wa Marekani mjini Teheran na kuwateka Wamarekani kama makole.Fatwa ya Ayatollah Khomeini kudai kifo chamwandishiSalman Rushdie iliongeza sifa za ukali za Uajemi.
Uajemi ni Jamhuri ya Kiislamu inayoongozwa nakatiba yenye sehemu za kidemokrasia na sehemu za kidini.
Mamlaka kuu ikomikononi mwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi anayesimamiasiasa ya nchi kwa jumla; yeye niamiri jeshi mkuu na msimamizi mkuu wahuduma yausalama; pia anaratibu siasa ya nje. Anateua wakuu wa jeshi,redio natelevisheni, viongozi wasalat wamsikiti mkuu katika kilamji,jaji mkuu namwendesha mashataka mkuu halafu nusu ya wajumbe wa Halmashauri ya Walinzi wa Katiba wanaokubali au kukataa sharia zote zilizopitishwabungeni wakiwa na mamlaka kusimamisha wagombea kwa uchaguzi wa kitaifa. Anaweza kumwachisha rais. Kiongozi mkuu huchaguliwa na Mkutano wa Wataalamu wa Uongozi kwa muda wa maisha yake.Ayatollah Khamenei ni Kiongozi Mkuu wa pili tangu mapinduzi ya Kiislamu.
Serikali inayoongozwa na rais wa Uajemi aliye na nafasi ya pili baada ya Kiongozi Mkuu. Huchaguliwa na wananchi wote kwa kipindi cha miaka 4 na anaweza kuchaguliwa upya. Wagombea wanahitaji kukubaliwa na Halmashauri ya Walinzi wa Katiba. Rais anaongoza serikali na kazi yake. Katika mambo ya siasa ya nje, jeshi na siasa ya nyuklia yuko chini ya mamlaka ya kiongozi mkuu.
Bunge inayoitwa "majlis" inawabunge 290 waliochaguliwa kwa muda wa miaka 4. Wagombea wote wanahitaji kibali cha Halmashauri ya Walinzi wa Katiba. Majlis inatunga sheria za nchi na kukubalimakisio ya serikali na mikataba ya kimataifa. Sheria zote zilizopita bungeni zinahitaji tena kibali cha halmashauri ya walinzi.
Halmashauri ya Walinzi wa Katiba ni chombo muhimu sana kinachohakikisha mamlaka kuu ya kiongozi mkuu. Ina wajumbe 12 ambao niwanasheria. 6 wanateuliwa moja kwa moja na Kiongozi Mkuu. 6 wengine wanachaguliwa nabunge kati ya majina wanaopelekwa mbele na jaji mkuu - anayeteuliwa na Kiongozi Mkuu. Kwa hiyo kiongozi mkuu anaamua juu ya wajumbe wote waliomo katika halmashauri hii, hakuna anayeweza kuwa mjumbe bilakibali chake ama moja kwa moja au kupitia jaji mkuu aliyeteuliwa naye.
Uajemi umegawiwa kwamikoa 31 inayoitwa "ostan" chini yagavana anayeteuliwa na rais. Kila mkoa huwa nawilaya (shahrestan) na ngazi ya chini zaidi nimitaa (bakhsh). Chini ya mitaa kunakata (dehestan) zinazojumlisha vijiji kadhaa.
Leo hii takriban asilimia 90 za wakazi ni Waislamu Washia. Karibu 10% niWasunni, hasa katika maeneo karibu na mipaka; kiutamaduni Wasunni wengi niWakurdi,Wabaluchi auWaturkomani.
Wafuasi wa dini nyingine kwa jumla ni kama 1% ya wakazi wote. Kundi kubwa niBahai lakini dini yao ilipigwa marufuku baada ya mapinduzi ya Kiislamu. Kundi linalofuata ni Wakristoː kati hao kundi kubwa niWaarmenia, halafuWakaldayo.Wayahudi wa Uajemi ni kundi kubwa kati ya nchi zote za Kiislamu wamashariki ya kati (0.01%). Wazoroasta wamebaki pia (0.03%). Kundi dogo sana niWamandayo wanaoitwa pia wafuasi waYohane Mbatizaji.
1. Nchi ina maeneo katikaAsia naUlaya. 2. Nchi ikoAsia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi zaUlaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.
Makala hii kuhusu maeneo yaAsia bado nimbegu. Je unajua kitu kuhusuUajemi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.