Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Nepal

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Shirikisho la Nepal
सङ्घीय लोकतान्त्रिक गणतन्त्र नेपाल (Saṅghīya Lokatāntrika Gaṇatantra Nepāla)
Kaulimbiu: जननी जन्मभूमिश्च स्वर्गादपि गरीयसी – "Mama na Taifa ni kuu kuliko Peponi"
Wimbo wa taifa: सयौँ थुँगा फूलका (Sayaun Thunga Phulka) – "Maua Mamia"
Mahali pa NepalMahali pa Nepal
Mji mkuu
na mkubwa
Kathmandu
Lugha rasmiKinepali
Lugha ya taifaLugha zote za mama
SerikaliJamhuri ya shirikisho ya bunge
 Rais
Ram Chandra Poudel
Sushila Karki (kaimu)
Katiba ya sasa
  Muungano wa Nepal
25 Septemba 1768
  Jamhuri ya Shirikisho
28 Mei 2008
Eneo
  Jumlakm2 147,516 km²
  Maji (asilimia)2.8%
Idadi ya watu
  Kadirio la 202431,122,387
  Msongamano180/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
  Jumla$169.120 bilioni
  Kwa kila mtu$5,348
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
  Jumla$43.673 bilioni
  Kwa kila mtu$1,381
HDI (2023)Ongezeko 0.622
-kati
Gini (2022)30.0
SarafuRupia ya Nepal (NPR)
Majira ya saaUTC+05:45 (Saa ya Nepal)
Msimbo wa simu+977
Jina la kikoa.np
Ramani ya Nepal

Nepal, rasmiJamhuri ya Kidemokrasia ya Shirikisho la Nepal ninchi isiyo na pwani iliyoko katikaAsia ya Kusini, kati yaUchina kusini naIndia kaskazini-mashariki. Ina idadi ya wakazi takriban milioni 31, ikiwa ya 49 duniani kwa idadi ya watu. Mji mkuu na jiji kubwa zaidi niKathmandu. Lugha rasmi niKinepali. Nepal inajulikana kwa kuwa na sehemu kubwa yamilima ya Himalaya ikiwemoMlima Everest ambao ndio mkubwa zaidi duniani, urithi wake wakitamaduni nakidini, hasaUhindu naUbudha, na lenyehistoria tajiri yakifalme na mapambano yakidemokrasia.

Jiografia na hali ya hewa

Nepal inaumbo lamstatili ulioambatanishwa na umbo lapembetatu. Inaurefu wakilomita takribani 800 naupana wa kilomita 200.

Maeneo ya kijiografia ya Nepal yanayojulikana sana ni Himal, Pahad na Terai: Himal ni eneo lenye milima. Terai ni pahala palipo chini na Pahad ni milima isiyo natheluji.

Kwa kawaida nchi ya Nepal huwa namvua ya kutosha japo kunabaridi nyingi zakipupwe.

Misitu ya nchi hii imekuwa ikififia kutokana na ukataji holela wamiti.

Historia

Vyombo vyawatu waliokuwa wakiishi katikazama za mawe zilipatikana katikabonde la Kathmandu kuonyesha kwamba kumekuwa na watu waliokuwa wakiishi katika eneo hili laHimalaya kwa muda wa zaidi ya miakaelfukumi na moja.Maandishi makongwe yaonyesha kwamba Nepal ilikuwepo hata miaka 30kabla ya ujio wa Yesu Kristo.

Viongozi wa kwanza nchini Nepal walikuwa wanaKirati.Historia ya Nepal yaonyesha kwamba kulikuwa na kadri yahimaya 30 za wanaKirati walioongoza nchi hii.

Siasa

Kisiasa Nepal iko katika kipindi chamageuzi. Hadimwaka2006mfalme alitawala peke yake baada ya kuvunjabunge. Mwaka huo alilazimishwa kurudisha bunge, nalo lilitangaza ya kwamba mfalme hanamamlaka tena likamteua Mkuu wa nchi kwa muda. Tena kwamba bunge jipya litakalochaguliwa mnamoJuni2007 litaamua juu yakatiba mpya.

Tarehe28 Mei2008 wananchi waliamua kumalizaufalme Nepal ikatangazwa kuwajamhuri inayofuatademokrasia na kuwa namuundo washirikisho.

Katiba mpya ilipitishwa mwaka2015.

Watu

Wanepali wakicheza ngoma ya asili

Wenyeji wametokana nawahamiaji waliotokeaIndia,Tibet,China naMyanmar.

Hatalugha zinazotumika ni zajamii 4 tofauti. 44.6% wanaongeaKinepali ambacho ndicholugha rasmi. Hicho ni mojawapo yalugha za Kihindi-Kiulaya.

Wakazi wengi (81.3%) hufuatadini yaUhindu.Ubuddha una 9% wa wakazi, ukifuatwa naUislamu (4.4%),Ukirati (3.1%),Ukristo (1.4%) nadini za jadi (0.4%).

Utalii

Utalii ndiouti wa mgongo wauchumi wa Nepal. Nchi hii hupendwa na watalii wanaopenda kuzuru na kuikwea milima yake kama mlima Everest, milima ya Himal na Pahad.

Mengine yanayowapendeza watalii ni kuwatazamandege wa nchi hii na kupaa juuangani kwa kutumiabaluni zilizo nahewa iliyopashwamoto.

Watalii pia hupenda kuzuru nchi hii kwa sababu ya dini ya Kibudha ambayo imejikita mizizi.

Chakula cha Wanepali nidal bhat.Dal nimchuzi uliowekwamaharage, nayobhat nimchele. Wanepali pia hupenda kulamboga zinazoitwatarkari zilizowekwaviungo kwajinachutni.

Picha


  • Nepal
  • Kathmandu
    Kathmandu
  • Kathmandu
    Kathmandu
  • Bhaktapur
    Bhaktapur
  • Patan
    Patan
  • Himalaya
    Himalaya
  • Himalaya
    Himalaya
  • Mustang
    Mustang
  • Changu Narayan
    Changu Narayan

Tazama pia

Viungo vya nje

Nchi na maeneo yaAsia

Afghanistan |Armenia2 |Azerbaijan |Bahrain |Bangladesh |Bhutan |Brunei |China |Falme za Kiarabu |Georgia2 |Hong Kong3 |Indonesia |Iran |Iraq |Israel |Jamhuri ya China (Taiwan) |Japani |Kamboja |Kazakhstan |Kirgizia |Korea Kaskazini |Korea Kusini |Kupro2 |Kuwait |Laos |Lebanoni |Macau3 |Malaysia |Maldivi |Mongolia |Myanmar |Nepal |Omani |Pakistan |Palestina |Qatar |Saudia |Singapuri |Sri Lanka |Syria |Tajikistan |Timor ya Mashariki |Turkmenistan |Ufilipino |Uhindi |Urusi1 |Uthai |Uturuki1 |Uzbekistan |Vietnam |Yemen |Yordani

1. Nchi ina maeneo katikaAsia naUlaya. 2. Nchi ikoAsia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi zaUlaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.
Makala hii kuhusu maeneo yaAsia bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuNepal kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Nepal&oldid=1454082"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp