Mpira wa miguu (piasoka aukandanda) nimchezo unaochezwa na jumla ya wachezaji ishirini na wawili katikatimu mbili, kila timu ikiwa na wachezaji kumi na mmoja.
Lengo hasa la mchezo huu ni wachezaji kuumilikimpira kwa kutumiamiguu na kufunga goli, yaani kuuingiza mpira katikawavu wa wapinzani mara nyingi zaidi.
Matumizi yamikono ni marufuku isipokuwa kwamlinda mlango katika eneo maalumu na wakati wa kurudisha mpira baada ya kutoka nje ya uwanja.
Michezo mbalimbali ya kuchezea mpira inaweza kupatikana katika kila uwanja wajiografia nahistoria.Wachina,Wajapani,Wakorea naWaitalia, wote hao walikuwa wakicheza mpira zamani kabla ya enzi zetu.Wagiriki naWaromania walitumia michezo hiyo kuwaandaa wapiganaji kabla yavita.
Hata hivyo, ni nchiniUingereza ambapo umbo la soka la kisasa lilianza kulipuka.
Ilianza wakati mashirikisho mawili (Shirikisho la Mpira wa miguu na Mpira waRagbi) yalipotawanyika. Shirikisho la kwanza lilibakiaUingereza. MnamoOktoba 1963, Vilabu 11 vyaLondon vilituma wawakilishi katika mkutano waFreemasons ili kujadili na kuweka kanuni zilizokubalika kusimamiamechi zilizochezwa kati yao.
Miongoni mwa kanuni zilizowekwa ni zile za kukataa utumiaji wa mikono kushika mpira na kunyang'anyana kwanguvu. Soka na Ragbi zilifarakana tarehe hiyo.
Miaka minane baada ya kuanzishwa, Shirikisho la Kandanda (FA) lilikuwa na wanachama 50. Shindano la kwanza la kandanda -Kombe la FA - lilianza mwaka huo, likifuatiwa na lile laLigi ya Ubingwa miaka 17 baadaye.
Wachezaji wawili wa Klabu ya Darwin,John Dove naFergus Suter walikuwa wa kwanza kulipwa kwa mchezo wao. Kitendo hiki kilikuwa mwanzo wasoka la kulipwa iliyohalalishwa mwaka wa1885.
Mwamko huu ulipelekea kuanzishwa kwa Mashirikisho ya kitaifa nje ya Uingereza (Great Britain). Baada ya Shirikisho la Kandanda la Uingereza, Mashirikisho yaliyofuatia ni yaUskoti (1873),Wales (1875) naEire (1880).
Kutokana na ushawishi mkuu wa Uingereza katikamataifa yadunia, soka ilisambaa koteduniani.
Mataifa mengine mengi yalianzisha Mashirikisho ya Kandanda kufikia1904 wakatiShirikisho la Soka Duniani (FIFA) lilipoanzishwa. Tangu hapo, kandanda ya kimataifa imekuwa ikikua licha ya vikwazo mbalimbali.
Kufikia1912,FIFA ilikuwa na uanachama wa mashirikisho 21,idadi iliyoongezeka na kufikia 36 mwaka1925.
Kufikia 1930 - mwaka ambapo kwa mara ya kwanza kulikuwa na mashindano yaKombe La Dunia,FIFA ilikuwa na wanachama 41. Idadi hii ilizidi kuongezeka na kufika 51 mnamo1938 na 76 kufikia1950.
Baada ya Kongamano laFIFA la mwaka2000, kulikuwa na wanachama 204 na idadi hii inazidi kukua kila mwaka.
Uwanja una umbo lamstatili. Hakunakipimo kamili, ila kanuni zinasemaurefu ni baina yamita 90 na 120,upana baina ya mita 45 na 90. Kwa michezo ya kimataifa urefu uwe baina ya mita 100 - 110 na upana baina ya mita 64 na 75.
Goli ziko kwenye pande fupi zaidi. Kunaalama yabendera kwenye kona za uwanja. Mwaka2008 IFAB ilijaribu kusanifisha vipimo kuwa mita 105 kwa 68, lakini kanuni hii ilisimamishwa baadaye.
Mstari ni mpaka wa uwanja. Wakati mpira uko kwenye mstari hata kwa kiasi kidogo unahesabiwa bado uko ndani ya uwanja. Kwa goli kukubaliwa sharti mpira uwe umepita mstari wa goli kabisa.
Ni uamuzi wakocha kuhusu idadi ya wachezaji wa kulinda lango, wa kiungo au wa mbele, ikitegemea mfumo uliotumika. Mfumo wa 4-4-2[4] umekuwa maarufu miongoni mwa timu nyingi. Mfumo huu hujumlisha walinzi wanne pamoja na mlinda lango, wachezaji wanne wa kiungo na wawili wa mbele.mshambuluaji lazima akawa mtu mwenye ujuzi mkubwa na mwenye nguvu za kushambulia
Utunukizi wa Alama
Golikipa akiokoa mpira uliopigwa shuti ndani ya eneo la penati
Katikaligi za kitaifa na kimataifa, alama hutunukiwa kwa timu baada ya mchezo. Timu iliyoshinda hupewa alamatatu huku timu zilizotoka sare hupewa alamamoja kila moja.
Ikiwa ni lazima mshindi apatikane, hasa kwenye mechi zafainali, mchezo huwa namuda wa ziada kama timu hizo zikosare. Iwapo sare hiyo huendelea mchezo huamuliwa kwamikwaju yapenalty.
Shirikisho la Kandanda Duniani
[5]Shirikisho la Soka Duniani (FIFA) ndilo shirikisho kuu linalosimamia kandanda duniani. Wanachama wake ni mashirikisho ya kandanda ya nchi mbalimbali. Kufikia mwaka wa 2000, lilikuwa na wanachama 204 kutoka pembe zote za dunia. Shirikisho hili huandaa mashindano mbalimbali ya soka kama vileKombe la Dunia la FIFA na pia huwatunuku wachezaji.
Orodha ya Wachezaji Maarufu Duniani
Orodha ifuatayo inaonyesha baadhi ya wanasoka maarufu duniani, lakini haiashirii usanjari huu kulingana na ubora. Wapo wengine wengi ambao hawajatajwa hapa.[6]
Mchezo ulipelekwa Afrika na Waingereza wakati wa ukoloni. Mechi za kwanza zilizorekodiwa mwaka 1862 hukoCape Town naPort Elizabeth[7].
Ilhali ulikuwa mwanzoni mchezo wa kizungu ulienea haraka kati ya vijana Waafrika kupitia shule, jeshi na wafanyakazi wa reli. Kwa mfano kisiwaniUnguja walikuwa wafanyakazi Wazungu na Wahindi waliocheza soka pamoja wakitazamiwa na wenyeji, halafu wanafunzi wa shule ya misioni St Andrew's yaUMCA. Khamis Fereji alikumbuka jinsi gani mnamo 1910 soka ilichezewa na watoto na vijana kote Zanzibar mjini wakitumia mipira ya tennis mtaani au mwambanoni wakati wa jioni ilhali wazee walitazama. Vivyi hivyo aliandika Dr. Nmandi Azikiwe katika kumbukumbu ya maisha yake ya kwamba alipokuwa mtoto Calabar (Nigeria) kabla ya Vita Kuu ya Kwanza walicheza mpira kila mahali kwa kutumia maembe, machungwa au mipira ya tennis[8]
Mchezo ukaendelea kupanuka na kuendeshwa na wenyeji katika klabu zilizoundwa wakati miji ilikua na kuwa na wakazi wengi Waafrika[9].
Tangu uhuru soka ilipanuka sana katika nchi huru za Afrika. Baada ya kujiunga naFIFA wawakilishi wa nchi huru za Afrika waliweza kuhakikisha ya kwamba Afrika Kusini ilitengwa kwa sababu ya siasa yake yaapartheid (ubaguzi wa rangi).
Tangu 1970 mpango wa kombe la dunia ulibadilishwa kuhakikisha nafasi kwa kila bara na Afrika ilipewa nafasi 1 ya hakika. 1986 zilikuwa nafasi 2, 1998 nafasi 4 na tangu kombe la 2002 kuna nafasi 5 kwa timu kutoka Afrika.[10]
KwaTanzania na nchi nyingi zaAfrika kuna uhaba wawafadhiliː hiyo husababishatimu ambazo hazina uwezo wa kiuchumi kukata tamaa. Tatizo kubwa ni uhamisho wa wachezaji vijana wenye uwezo kuhamia nje ya Afrika. Wakati wa kombe la dunia idadi kubwa wachezaji wa timu za kitaifa kutoka Afrika wanaajiriwa na klabu huko Ulaya; wakati wa kombe la dunia dunia 2010 walikuwa asilimia 80 za wachezaji Waafrika kwenye kombe la dunia waliocheza kwa klabu za Ulaya. Hali hii inashusha uwiano wa soka katika ligi za kitaifa kwa sababu wachezaji bora wako ng'ambo wakipatikana tu kwa mechi za kimataifa wakishiriki katika timu ya kitaifa.[11]
Mpira wa miguu nje ya kanuni za kawaida
Video inaonyesha namna nyingi jinsi gani mpira unachezewa duniani.Katika mpira wa miguu, madhumuni ya msingi ya mashabiki ni kuhamasisha timu yao wakati wa mechi.
Hali halisi kuna namna nyingi kucheza soka hata pasipo na wachezaji 22 au uwanja kamili. Kila mahali dunaini watu hasa vijana hucheza barabarani au shambani kwa kila idadi ya wachezaji, ilhali fimbo au mawe mawili hudokeza goli. Pasipo na mpira kamili vijana hujitengenezea kifaa kwa karatasi au plastiki iliyoshikwa kwa kamba katika umbo la kufanana na tufe.
Kwa mazingira ya pekee kuna pia mapatano juu ya kanuni maalumu kwa timu ndogo (kwa mfano wachezaji 5/5) au mahali kama mchanga wa mwabaoni (beach soccer), katika ukumbi (indoor soccer) au kwa wachezaji walemavu.