Moroko (piaMaroko, kwaKiarabu المغرب), rasmi kamaUfalme wa Moroko, ni nchi katikaAfrika ya Kaskazini, inayopakana naBahari ya Atlantiki naBahari ya Mediteranea kaskazini,Algeria mashariki, na Sahara Magharibi kusini. Ina idadi ya watu takriban milioni 37, ikiwa ya 40 duniani. Jiji lake kubwa zaidi niCasablanca, wakati mji mkuu niRabat. Moroko imegawanyika katika mikoa 12, inayosimamia utawala wa ndani wa nchi. Inajulikana kwa historia yake tajiri ya kifalme, miji ya kihistoria kama Fez na Marrakesh, na urithi wake wa kipekee unaochanganya tamaduni za Kiarabu, Berber, na Ulaya.
Eneo la Moroko nikm² 446,550. Sehemu kubwa nijangwa laSahara. Watu walio wengi huishi kwenye sehemu zarutuba karibu na pwani.
Kunamilima inayofunika maeneo makubwa. Milima yaRif inaongozana na pwani ya Mediteranea yenye mwelekeo kutoka kaskazini-magharibi kwenda kaskazini-mashariki. Milima yaAtlas iko katikati ya nchi kutoka kusini-magharibi kwenda kaskazini-mashariki.
Miji mikubwa
Mji mkuu niRabat wenye wakazi milioni 1.2.Mji mkubwa niCasablanca (kwa Kiarabu: الدار البيضاء dar al-baiDa = nyumba nyeupe). Miji yote miwili mikubwa ni miji yabandari.
Miji mitano mikubwa ni kama ifuatavyo (namba zasensa ya mwaka2004):
Habari za kimaandishi za kwanza ni kutokakarne za kwanzaKK.Wafinisia walijenga miji yao pwani lakini eneo la ndani lilibaki nchi yaWaberber walioundaufalme wa Mauretania ya Kale (usiuchanganye na nchi ya kisasaMauretania) uliounganisha sehemu kubwa ya Moroko ya kaskazini.
Mwanzoni Moroko ilikuwa sehemu yamilki ya khalifa yaWaomawiyya waliotawalaDameski (Siria). Baada ya kupinduliwa kwa Waomawiyya naWaabasiya waBaghdad (Iraq) mkimbizi MwarabuIdris ibn Abdallah (788-791) alikusanya makabila ya Waberber na kuunda milki ya kujitegemea. Hii ilikuwa mwanzo wa Moroko kuwa milki ya Kiislamu inayojitawala.
Watawala wa kienyeji
Vipindi vyahistoria husebabiwa kufuatana na familia zilizofuatana za wafalme Waarabu au Waberber.
Wamuwahidun waliendelea kupanuka kuelekeaMisri lakini baadaye walidhoofika wakapaswa kuwaachia Wahispania Wakristo sehemu zaAndalusia.Athira ya milki ya Moroko ilipungua baadaye hadiHispania yote ikarudishwa kwa watawalaWakristo mwaka1492; pia utawala kusini kwaSahara haukuendelea.
Wareno waWahispania waliendelea kuteka miji kwenye pwani za Moroko. Utawala wa Hispania juu yaCeuta naMelilla leo ni mabaki ya nyakati zile.
Sehemu za nchi zilianza kujitawala bila kukubali tena mamlaka wa juu, kwa mfano makabila ya Waberber milimani au miji ya Rabat naSale iliyounda dola dogo laJamhuri ya Bou Regreg katikakarne ya 17 na kujishughulisha nauharamia.
Baada yavita Wafaransa walijaribu kukandamiza mwendo huo wakamwondoaSultaniMohammed V nchini1953.Ghasia zikaongezeka, Sultani akarudi na nchi ikapewa uhuru mwaka1956.
Utawala wa mwanaeHassan II kuanzia mwaka1961 uliitwa "miaka ya risasi" kwa sababu mfalme alikataa kukubali utaratibu wa kidemokrasia.Chaguzi zilikuwa zauwongo,wapinzani wakatupwajela au kuuawa. Hassan II alishinda majaribio mbalimbali ya kumpindua.Siasa ya kushikamana naMarekani ilimsaidia mfalme kimataifa lakini baada ya mwisho wa "vita baridi" alilazimishwa na Wamarekani kulegeza utawala wake.
Kaskazini mwa nchi ambakokitovu chake niFes kuna zaiditabia ya Kiarabu, wakatu kusini ambako kitovu chake ni Marakesh kuna tabia ya Kiberber zaidi.
Lugha
Lugha rasmi ya nchi niKiarabu naKiberberi. Waberber wengi, hasa kaskazini, wameacha lugha yao na kutumia Kiarabu lakini walileta maneno yao katikalahaja ya Kiarabu cha Kimaroko. HataKifaransa kinatumika sana.
Dini
Uislamu ndiodini rasmi na ndio unaofuatwa na wakazi wengi sana (98.9%), hasaWasunni. Wengine niWakristo (0.9%) naWayahudi (0.2%). Wakristo karibu wote ni wa asili yaUlaya. Wayahudi waliwahi kuwa wengi kidogo, lakini idadi yao imepungua katika miaka ya nyuma kutokana nauhamaji hata kama hali yao katikataifa ni nzuri kulingana na nchi nyingine za Kiarabu.
Uchumi
Nguzo za uchumi wa nchi ni kilimo na magodi ya kuchimba madini, pamoja na uvuvi na utalii.
Zaidi ya asilimia 40 za wananchi hulima. Kwa jumla asilimia 18 za eneo la Moroko zinatumiwa kwa kilimo, hasa katika magharibi na kaskazini-magharibi.
Nchi hii ina akiba kubwa ya fosfati inayochimbwa na kuuzwa nje kwa matumzi ya mbolea. Akiba ya fosfati ni kubwa duniani. Moroko ina nafasi ya tatu katika uzalishaji baada ya China na Marekani[1].
Umuhimu wautalii kwa uchumi umezidi kukua; mwaka 2018 idadi ya watalii ilifikia milioni 12.3[2]Vivutio vya kitalii ni pamoja na mahali paurithi wa dunia kama vile
Makala hii kuhusu maeneo yaAfrika bado nimbegu. Je unajua kitu kuhusuMoroko kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
↑Phosphorus A Looming Crisis, Vaccari, David A. (2009). "Phosphorus: A Looming Crisis" (PDF). Scientific American. 300 (6): 54–9.