Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Molekuli

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Molekuli fulani inavyoonekana ikikuzwa.

Molekuli ni maungano ya kudumu ya angalauatomi mbili au zaidi. Ni pia kitengo kidogo cha kiladutu. Kama molekuli inapasuliwa ni dutu tofauti zinazojitokeza.

Molekuli ni ndogo sana haionekani kwa macho.

Muungo atomia

[hariri |hariri chanzo]

Atomi ndani ya molekuli hushikwa kwa nguvu yaelektroni aumuungo atomia. Maungano ya atomi katika molekuli hufuata maumbile ya atomi.Maumbile haya Kwa mfano atomi zahidrojeni huwa na nafasi moja ya kushikana na atomi nyingine,oksijeni huwa na nafasi mbili ya kushikana na atomi nyingine.Kaboni ina nafasi nne nanaitrojeni ina nafasi tatu. Hapo ni sababu ya kwambamaji ni molekuli ya H2O yaani hidrojeni ina mkono mmoja na oksijeni ina mikono miwili hivyo atomi moja ya oksijeni ikishika atomi za hidrojeni (yenye mkono moja) mbili ni molekuli thabiti na imara hakunamkono unaobaki.

Fomula

[hariri |hariri chanzo]

Fomula ya molekuli inaeleza idadi na aina ya atomi ndani ya molekuli. Kwa mfanosukari ina formula ya C6H12O6. Maana yake ni kwamba molekuli moja ya sukari huwa na atomi 6 za kaboni, 12 za hidrojeni na 6 za oksijeni.

Molekuli nahali maada

[hariri |hariri chanzo]

Katikagesi molekuli zina uhuru wa kuelea.

Katikagimba mango kila molekuli ina mahali pake.

Katikakiowevu molekuli zinakaa pamoja lakini ni rahisi kubadilishana nafasi.

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mambo yakemia bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuMolekuli kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Molekuli&oldid=1305477"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp