Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Mmea

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Aina mbalimbali za mimea.

Mimea (kwaKiingereza: "plants", kutokaKilatini "Plantae") nimoja kati yamakundi yaviumbe haiduniani likijumuishamiti,maua,mitishamba na kadhalika. Kuna zaidi ya aina 300,000 ya mimea.

Sayansi inayochunguza mimea huitwabotania ambayo ni kitengo chabiolojia. Kwenyeuainishaji wa kisayansi mimea hujumlishwa katikahimaya ya plantae kwenyemilki yaEukaryota (viumbehai vyenyekiini cha seli nautando wa seli).

Kwa hiyo mimea huwa na utando wa seli wenyeselulosi. Mmea unapata sehemu kubwa yanishati kutokanuru yajua kwa njia yausanisinuru, yaani hujilisha kwa msaada wa nuru. Ndani yamajani ya mimea kunaklorofili,dutu yarangi yakijani, inayofanyakazi ya kupokea nuru na kupitisha nishati yake kwa sehemu nyingine ya mmea ambamo inatumiwa kujengamolekuli zinazotunza nishati kwa njia yakikemia na kutumiwa katikametaboli yamwili.

Mimea kadhaa imepoteza uwezo wa kutengeneza klorofili ya kutosha, hivyo inajipatia nishati kamavimelea kutoka kwa mimea au viumbehai wengine.

Mimea mingi inazaa kwa njia yajinsia, yaani kwa kuunganishaseli za kiume na kike; mara nyingi viungo vya kiume na vya kike vinapatikana ndani ya mmea mmoja. Kuna pia mimea inayozaa kwa njia isiyo ya kijinsia, kwa mfano kwa kuoteshamzizi wahewani ambao unaingia ardhini na kuendelea kama mmea wa pekee.

Mimea ni msingi muhimu kwa viumbehai wengine duniani kwa sababu sehemu kubwa yaoksijeni katikaangahewa ya dunia inatengenezwa na mimea.[1].

Mimea inatoachakula kwabinadamu kama vilenafaka,matunda namboga za majani, pialishe kwawanyamawa kufugwa.

Picha

[hariri |hariri chanzo]
  • Mvumo wa Asia Borassus flabellifer
  • Mavumo Borassus flabellifer (yaitwayo Thaati Munjelu kwa kienyeji) yanayouzwa katika soko ya Guntur, Uhindi.
    MavumoBorassus flabellifer (yaitwayo Thaati Munjelu kwa kienyeji) yanayouzwa katika soko ya Guntur, Uhindi.
  • Manjano
    Manjano
  • Kiazi kitamu, Ipomoea batatas, Bustani ya Kibotaniki ya Maui Nui
    Kiazi kitamu,Ipomoea batatas, Bustani ya Kibotaniki ya Maui Nui
  • Mkadi wa Asia (Pandanus amaryllifolius)
    Mkadi wa Asia (Pandanus amaryllifolius)
  • Papai la Kalifornia
    Papai la Kalifornia
  • Mapapai (Carica papaya), kultivari 'Sunset'
    Mapapai (Carica papaya), kultivari 'Sunset'
  • Mzumari (Cymbopogon citratus)
    Mzumari (Cymbopogon citratus)
  • Pachyrhizus erosus, aina ya tunguu. Situgede, Bogor, Java ya Magharibi, Indonesia.
    Pachyrhizus erosus, aina ya tunguu. Situgede, Bogor, Java ya Magharibi, Indonesia.
  • Tufaa aina ya Kiku
    Tufaa aina ya Kiku
  • Miche ya Sauropus androgynus
    Miche yaSauropus androgynus
  • Nazi (Cocos nucifera)
    Nazi (Cocos nucifera)

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. Field, C.B.; Behrenfeld, M.J.; Randerson, J.T.; Falkowski, P. (1998). "Primary production of the biosphere: Integrating terrestrial and oceanic components".Science.281 (5374): 237–240.Bibcode:1998Sci...281..237F.doi:10.1126/science.281.5374.237.PMID 9657713.
Makala hii kuhusu mambo yabiolojia bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuMmea kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Mmea&oldid=1166905"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp