Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Mexico (mji)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jiji la Mexico
Jiji la Mexico is located in Mexiko
Jiji la Mexico
Jiji la Mexico

Mahali pa mji wa Mexico katika Mexico

Majiranukta:19°26′0″N99°8′0″W /19.43333°N 99.13333°W /19.43333; -99.13333
NchiMexiko
Tovuti:  http://www.df.gob.mx/
Mexico
Nembo ya Jiji la Mexiko tangu mwaka 1523.

Jiji la Mexico(kwaKihispania: Ciudad de México) nimji mkuu piamji mkubwa wa nchi yaMexico. Jiji lina wilaya 16, ambazo kila moja zimegawanywa katika vitongoji aucolonias.

Uko kwenyenyanda za juu za Mexico kwenyekimo cham 2000 juu yaUB katikabonde refu linalopakana namilima mirefu. Kati ya milima hii nivolkeno zaPopocatepetl naIztaccihuatl na nyororo yaSierra Nevada.

Mji wa Mexico ni piamkoa wa kujitegemea, huitwa mara nyingi na Wamexiko wenyewe "Mexico DF" au kwa kifupi "DF" (DF = Distrito Federal, Mkoa wa Shirikisho), lakini tangu mwaka2016 unaelekea kujitegemea zaidi kiutawala.

Idadi ya wakazi nimilioni 9, lakini pamoja na mitaa ya karibu idadi inafikia karibu milioni 20.4. Ni kati ya miji mikubwa kabisaduniani.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Historia ya mji ilianzamwaka1325. Wakati ule kikosi chaAztekiwahamiaji walifika kwenyeziwa la Texcoco na kujenga makao kwenyekisiwa ziwani wakauita mji "Tenochtitlan".

Kunahadithi ya kale juu ya kuundwa kwa Tenochtitlan ambao ni mji wa Kiazteki uliotangulia Mexiko City.

Zamani ile Waazteki waliishi maisha ya kuhamahama na kutafuta mahali pa kujenga mji wa kudumu.Mungu wao Huitzilopochtli aliwaambia wamtafute anayekalia mpungate (kakati) na kushikanyoka. Mpungate utapatikana kwenyemwamba katika kisiwa ziwani. Hadithi yaendelea kusema ya kwamba baada ya matembezi ya miaka 200 walikuta ziwa la Texcoco penye mwamba na mpungate. Walipokaribiatai aliyeshika nyoka akaketi kenye mpungate huu.

Baada ya kupokeaishara hiyo waliunda mji wao wa Tenochtitlan uliokuwa baadaye mji mkuu waDola la Azteki. Ulikuwa na wakazi 300,000 wakati wa kufika kwaWahispania mwaka1519.

Mwaka 1519 alifika MhispaniaHernan Cortez pamoja najeshi laaskari 450. Baada ya kupokewa vizuri namfalme wa AztekiMontezuma walimkamata kamamfungwa na kuchukuadhahabu kutokamahekalu.

Wenyeji wa mji waliwashambulia na kuua Wahispania wengi. Cortes aliweza kukimbia akarudi na jeshi jipya akaweza kuteka mji tarehe13 Agosti1521 na kuuharibu kabisa.

Mji wa Mexico

[hariri |hariri chanzo]

Wahispania walianzisha mji mpya juu ya maghofu ya mji wa kale.Makanisa yalijengwa mahali pa mahekalu ya kale.

Tangu mwaka1525 mji wa Mexiko ulikuwa mahali paserikali ya nchi, tangu1535 mji mkuu wa "Ufalme Mdogo wa Hispania Mpya". Makoloni ya Hispania yaGuatemala,Kuba,Florida na hataUfilipino katikaAsia yalitawaliwa kutoka hapa.

Mji ulikuwa mji mkuuwa wa nchi huru tangu1821.

Katikakarne ya 20 ilikua haraka sana.

Makala hii kuhusu maeneo yaMexiko bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuMexico (mji) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Mexico_(mji)&oldid=1264646"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp