Alitazamiwa na Waroma sawa na munguHermes katikamitholojia ya Kigiriki hivyo aliabudiwa kama mtume aliyebeba ujumbe kutoka mungu mmoja kwa wengine, pia kama mungu wa biashara, uchumi, mawasiliano na wezi.
Katika mitholojia alikuwa mwana wa mungu mkuu Jupiter na mungu wa kike Maia. Tabia yake kuu ilikuwa uwezo wa kuhama haraka hivyo sanamu zake mara nyingi zilionyesha viatu na kofia yenye bawa. Mwendo wake wa haraka ilisababisha pia kumwunganisha na sayari ya kwanzaUtaridi iliyo na mwendo wa haraka kwa sababu obiti yake ni fupi kuliko sayari nyingine.
Kwa Kilatini na lugha za Ulaya sayari hii iliitwa pia Mercurius, kwa Kiingereza "Mercury". Mercury imekuwa pia jina lametali ya zebaki kwa Kiingereza kutokana na mwendo wake wakati inamwagika.