Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Meksiko

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Muungano wa Madola ya Meksiko
Estados Unidos Mexicanos (Kihispania)
Wimbo wa taifa:Himno Nacional Mexicano
"Wimbo wa Taifa wa Meksiko"
Mahali pa MeksikoMahali pa Meksiko
Mji mkuu
na mkubwa
Mexico (mji)
Lugha rasmiKihispania
Lugha za kikabila68 lugha za asili
 Rais
Claudia Sheinbaum
 Rais waSeneti
Gerardo Fernández Noroña
Historia
  Mwanzo wa Vita ya Uhuru
16 Septemba 1810
  Tangazo la Uhuru
27 Septemba 1821
  Katiba ya sasa
5 Februari 1917
Eneo
  Jumlakm2 1,972,550(ya 13)
  Maji (asilimia)1.58%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2025131,946,900
  Msongamano61/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2025
  Jumla $3.408 trilioni
  Kwa kila mtu $25,557
PLT (Kawaida)Kadirio la 2025
  Jumladecrease $1.818 trilioni(ya 12)
  Kwa kila mtudecrease $13,630
HDI (2023) 0.789kati
Gini (2022)40.2
SarafuPeso ya Meksiko (MXN)
Majira ya saaUTCUTC−8 hadi −5
UTC−7 hadi −5 (DST)
Upande wa magariKushoto
Msimbo wa simu+52
Jina la kikoa.mx

Meksiko, rasmiMuungano wa Madola ya Meksiko' (kwaKihispania:Los Estados Unidos Mexicanos), ninchi katikaAmerika ya Kaskazini. Inapakana naMarekani upande wa kaskazini,Guatemala naBelize upande wa kusini,Bahari ya Karibi upande wa mashariki, naBahari ya Pasifiki upande wa magharibi. Meksiko ina eneo la takriban kilomita za mraba 1,964,375, na ni miongoni mwa nchi kubwa zaididuniani. Ina mandhari mbalimbali kuanzia jangwa la Chihuahua hadi misitu ya mvua ya Yucatán, na historia tajiri inayojumuishaustaarabu wa kale kamaWamaya naWaazteki.

Ina idadi ya watu inayokadiriwa kuwa zaidi ya milioni 126 (2024), na hivyo kuwa nchi ya 10 kwa idadi ya watu duniani. Mji mkuu na mji mkubwa zaidi wamji wa Meksiko ni Mexico City, ambao pia ni kitovu chasiasa,uchumi, nautamaduni wataifa hilo. Licha ya changamoto kama ukosefu wa usawa wakijamii na usalama, Meksiko ni moja ya nchi zenyeuchumi mkubwa baraniAmerika, na ni mwanachama wa mashirika muhimu kamaUmoja wa Mataifa,G20, na Jumuiya ya Nchi za Amerika (OAS).

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Nchi jinsi ilivyo leo imeundwa na wakoloni Wahispania walioivamia kuanzia mwaka1519 na kuvunjautawala wa milki za wenyeji kamaAzteki naMaya.

Kabla ya uvamizi wa Hispania

[hariri |hariri chanzo]

Watu wa kwanza waliofika huko kutoka kaskazini walikuwaWaindio, wajukuu wa wahamiaji walioingiaAmerika kutokaAsia ya Kaskazini. Hakuna uhakika kufika huko kulitokea lini: labda miaka 10,000 iliyopita[1].

Hao Waindio walikuwawakulima hodari sana namazao mbalimbali ambayo leo ni msingi wachakula koteduniani yalianzishwa na kupandishwa nao, yakiwa pamoja namahindi,mboga nanyanya.Kilimo cha mahindi hukadiriwa kilianzishwa takriban mnamo mwaka9000 KK[2][3].

Sanamu ya kichwa ya Kiolmeki

Kilimo kiliweka msingi kwavijiji najamii zilizoshirikiana katika maeneo makubwa.Miji ya kwanza inajulikana kuanzia takriban mwaka1500 KK.

Staarabu mbalimbali zilistawi na kukua katika maeneo ya pwani (Waolmeki, Wamaya) na katikanyanda za juu za Mexico ya kati (Wazapoteki,Wamixeki,Watolteki, Waazteki).

Ustaarabu wa kwanza unaojulikana ulikuwa waWaolmeki baina ya 1500 KK na400 KK. Habari zao zinajulikana kutokana naakiolojia na mabaki ya miji nasanaa yao. Waolmeki walijenga miji wakaacha mifano ya sanaa yenye kiwango cha juu.

Waliishi katika kanda la pwani la Mexiko katika majimbo ya leo yaVeracruz naTabasco. Ni watu wa kwanza katika Mexiko wanaojulikana kubunimwandiko nakalenda,mchezo wampira naujenzi wapiramidi zahekalu. Walikuwa hodari sana kuchongasanamu yamawe, hasavichwa vikubwa vyenyeurefu WA zaidi yamita 3. Walifaulu kuunda sanaa hii bila kujua vifaa vyametali.

Hekalu - piramidi ya Kimaya
Ukurasa kutoka kitabu cha Kimaya - maandishi ya hiroglifi

Sanamu nyingine inayorudirudi ni mtu-jagwaa inayounganisha sehemu yamaumbile yabinadamu najagwa. Takriban mwaka 400–300 KK miji yao iliachwa na wakazi; hakuna uhakika ni nini iliyosababisha mwisho wa ustaarabu huu.

Upande wamashariki wa Waolmeki ustaarabu waWamaya ulianza tangu takriban mwaka2000 KK. Wamaya walikaliarasi yaYucatan pamoja na Guatemala na Belize ya leo. Waliishi katika vijiji na miji iliyojitegemea na kugombana kati yao mara kwa mara.

Wamaya walibuni mwandiko wahiroglifi wenyealama nyingi kupita maandishi mengine katikaAmerika ya Kale na kutungavitabu. Waliendeleza piahisabati, wakijuanamba "sifuri" na kuboresha mfumo wa kalenda.

Walikuwa hodari sana katikaastronomia yaanielimu yanyota. Walipamba miji yao kwamajengo makubwa na mazuri na kuwawafanyabiashara hodari. Sanaa yao ilijuauchongaji wa mawe na piauchoraji.

Jamii ya Wamaya ilifikia kiwango cha juu kuanzia mwaka500 KK wakati miji mikubwa ya kwanza ilipotokea. Mnamo mwaka800BK jamii za Wamaya katika Yucatan ziliporomoka;wataalamu wengi huamini ya kwamba mabadiliko yaekolojia nahalihewa pamoja na kuchoka kwarutuba yaardhi yalisababisha kutoka kwa watu katika makazi ya awali.

Lakini ustaarabu huu uliona tena kipindi cha kustawi katika maeneo mengine hadi kuja kwa Wahispania. Miji mbalimbali ya Wamaya iliendelea kujitetea dhidi ya wavamizi naNojpeten, mji wa mwisho wa kujitegemea ulitekwa mwaka1696 tu.

Teotihuacan

[hariri |hariri chanzo]
Barabara ya mahekalu na piramidi ya jua mjini Teotihuacan

Teotihuacan ilikuwa mji mkubwa katika nyanda za juu, karibu na Mexico City ya leo. Kuanzia mwaka100 KK hadi takriban550 BK ilikuwa mji mkubwa wa Amerika, pia moja kati ya miji mikubwa duniani nakitovu chautamaduni kilichoathiri staarabu zote za Mexiko.

"Teotihuacan" ilikuwajina la Waazteki kwa mji huu, jina la kienyeji halikuhifadhiwa. Maana ya jina ni "mahali pa kuzaliwa kwamiungu". Wakati wamaendeleo yake mji ulikuwa na eneo lakilomita za mraba 30 ukiwa na wakazi angalau 150,000, labda hata 250,000 walioishi humo[4].

Hakuna uhakika ni akina nani waliojenga Teotohuacan. Mji wote ulipangwa kwa kufuatabarabara mbili zilizoelekea kaskazini-kusini na mashariki-magharibi. Hekalu kubwa na piramidi zinaonyesha umuhimu wadini, na mabaki yanyumba za wakubwa na watu wa kawaida yanaruhusu kupatapicha ya jamii iliyoishi hapa.

Teotohuacan ilikuwa kitovu chabiashara ya misafara ya mbali na pia ya elimu. Ukubwa wa mji unaonyesha kiwango cha juu chautawala naushirikiano kati ya watu wake.

Katikakarne ya 6 BK sehemu kubwa ya majengo iliharibika na kuchomwa. Hakuna uhakika kama hii ilikuwa tokeo la uvamizi kutoka nje au vurugu aumapinduzi ndani ya mji. Baada ya maharibio yale mji ulianza kurudi nyuma na idadi ya watu kupungua. Mnamo mwaka750 BK watu wote waliondoka: nimaghofu ya majengo makubwa tu yaliyobaki[5].

Milki ya Azteki

[hariri |hariri chanzo]
Askari wa Azteki

Kuanzia mwaka 1325 kabila laAzteki likaunda mji waTenochtitlan kwenye kisiwa chaziwa la Tezcoco. Waazteki wakaendelea kuunda milki kubwa lililoeena na kutawala sehmu kubwa ya nyanda za juu za Mexiko. Msingi wa milki yao ilikuwa ushirikiano na mji miwili jirani iliyounda mwungano wa pande tatu lakini Waazteki waliendelea kuwa mshiriki mkuu na mtawala wa Tenochtitlan hatimaye alikuwa mtawala mkuu. Walishambulia maeneo ya miji na makabila jirani na kuwalazimisha kulipa kadi kwao. Kama walikubali kutoa kodi kila mwaka na pia kushiriki katika vita za milki watawala wa kienyeji waliruhusiwa kuendelea na utawala wa ndani. Dini yao iliweka uzito kwa sadaka za binadamu waliochinjwa kwenye mahekalu ya miungu yao. Waliunda mfumo wa mikataba ya vita na milki nyingine ambako walikutana kwa mapigano yaliyo kubaliwa awali kwa shabaha ya kukamata wafungwa wengi iwezekanavyo na kuwatoa kama sadaka kwa miungu hekaluni baadaye.

Uvamizi wa Wahispania

[hariri |hariri chanzo]

Mwaka 1519 MhispaniaHernan Cortez alifika kwenye pwani la Mexiko. Katika miaka iliyofuata alifaulu kuendelea hadi mji wa Tenochtitlan akiongozana na kundi la Wahispania mamia kadhaa. Cortez aliweza kuungana na miji na makabila ya Waindio waliochoka utawala wa Azteki na kumpa askari za usaidizi. Mwaka 1520 waliingia Tenochtitlan kama wageni wa mfalmeMontezuma II wakaendelea kumkamata lakini baada ya kifo cha mfalme walifukuzwa wakakimbia kwa matatizo katika "usiku wa huzuni" (Kihisp.noche triste). Waazteki walidhoofishwa sana kutokana naepidemia ya ugonjwa wandui[6]. Cortez aliweza kukusanya jeshi kubwa la Waindio waliopinga Waazteki akavamia na kuharibu Tenochtitlan mwaka 1521 na kwenye magofu ya mji huu alianzisha mji mpya waMexico City (Kihisp.Ciudad de Mexico).

Jinsi Bikira Maria alivyomtokea Juan Diego kwenye kilima Tepeyac, Mexico City.

Baada ya Hispania kuteka sehemu kubwa ya nchi mwaka 1521, liliundwakoloni laHispania Mpya chini ya makamu wa mfalme.

Bila kujaliukatili wa Wahispania,Waindio walijiunga haraka naKanisa Katoliki kuhusiana nanjozi ya mwenzaoJuan Diego aliyetokewa naBikira Maria hukoGuadalupe (12 Desemba1531), wakachanganyikana na wavamizi na kufanyataifa jipya lenye sura yakichotara, kiasi kwamba wengi wanajiona "mestizos" (machotara) hata wasipokuwa nadamu mchanganyiko.

Tangu uhuru hadi leo

[hariri |hariri chanzo]

Baada yakarne tatu na baada yavita vyaukombozi, mwaka 1821 wakazi walijipatiauhuru kwa jina la Mexico.

Vita ya uhuru

[hariri |hariri chanzo]

Mfano wauhuru wa Marekani mwaka1776 ulikuwa na athira pia kati ya wasomi wenyeji wa Mexiko. Jamii ya kikoloni iliundwa juu yaubaguzi kati ya Kreoli (walowezi wenye asili ya Hispania bila mchanganyiko na Waindio), Mestizos (asilimia kubwa ya wenyeji waliotokana nandoa zawanaume Wahispania nawanawake Waindio) na Waindio wenyewe. Lakini vyeo vyote vya juu, kama maafisa wa juu wa serikali, vilipatikana pekee kwa watu waliozaliwa Hispania na kutumwa Mexiko. Mawazo ya uhuru yalianza kupatikana kati ya Kreoli na Mestizos wa matabaka ya juu.

Chanzo cha vita ya uhuru kilikuwa mabadiliko katikaUlaya.Napoleon mtawala waUfaransa alimkamata mfalmeFerdinand VII wa Hispania akamlazimisha kujiuzulu na kumpakaka yakeYosefu Napoleonufalme wa Hispania. Hatua hii ilifuatwa na wimbi la uasi nchini Hispania dhidi ya mfalme Mfaransa.

Katika Hispania Mpya (Mexico) kamati za miji kadhaa zilizoongozwa na Kreoli ziliapa kumfuata mfalme mfungwa halali pekee. Kamati Kuu ya Mexiko City ilitaka kuanzisha bunge la pekee kwa sababu Hispania haikuwa tena na serikali halali. Mfalme mdogo (gavana mkuu) alikubali. Viongozi wengine walitangaza ilhali mfalme halali hayuko tena sasa, nguvu yote iko mkononi mwa wananchi. Hapo Wahispania katika koloni walioshika vyeo vikuu waliamua kumpindua mfalme mdogo na kuwakamata viongozi wa Kreoli.

Uasi ulifaulu lakini vikundi vidogo vya wapinzani wa uhuru kutoka Hispania waliendelea kukutana nchini na kukusanya viongozi. Hatimayepadre KreoliMiguel Hidalgo y Costilla alikusanya jeshi lawanamgambowakulima Waindio na Kreoli akapigana na jeshi lililokuwa chini ya mamlaka ya maofisa Wahispania. Miguel Hidalgo alishindwa na kuuawa, lakini hii ilikuwa chanzo cha uasi mkubwa ambao Wakreoli na wakulima Waindio walipigana na jeshi lililofuata amri ya Wahispania katika koloni.

Mwaka kiongozi wa upande wa migambo ya uhuru Guerrero na jenerali wa jeshi la serikaliAgustin de Iturbide walikutana wakapatana kuungana. Vikosi vingi vya jeshi la kikoloni vilihamia upande wao. Gavana mpya aliyefika kutoka Hispania aliamua kukubali uhuru uliotangazwa tarehe28 Septemba1821. Iturbide alikuwarais wa kwanza na baadaye kwa kipindi kifupiKaisari wa Mexiko hadi kujiuzulu mwaka1823: hapo Mexiko ikaendelea kuwajamhuri.

Karne ya 19

[hariri |hariri chanzo]
Maeneo yaliyoongezwa, yaliyotengwa au kujitenga na Mexiko tangu uhuru wa mwaka 1821: A) Maeneo yaliyotwaliwa na Marekani (nyekundu, kichungwa, nyeupe), Chiapas kuchukuliwa kutoka Guatemala (buluu), eneo la Yucatan lililotwaliwa (nyekundu) na maeneo ya Shirikisho la Amerika ya Kati (zambarau).

Katika miaka iliyofuata nchi haikupata msimamo imara kisiasa wala kiuchumi. Serikali mara nyingi zilikuwa hafifu na kubadilishana.

Vikundi vyaushikiliaji ukale nauliberali vilipigana hadi kuingia katikavita ya wenyewe kwa wenyewe.

Mwaka wa uhuru maeneo ya kusini yalijitenga na kuwaShirikisho la Amerika ya Kati lililofarakana baadaye kuwa nchi zaGuatemala,Honduras,El Salvador,Nikaragua naCosta Rica.

Mwaka1835 Marekani ilijaribu kununua maeneo yaTexas naKalifornia lakini Meksiko ilikataa. Hata hivyo utawala wa Mexiko kuhusu maeneo haya ya kaskazini yake ulikuwa hafifu na wa juujuu tu, Waindio walijitegemea hali halisi nje ya miji michache. Hivyo serikali ya Mexiko ilikaribisha walowezi kutoka Marekani kuhamia Texas. Hao walowezi wenye utamaduni waKiingereza-Kimarekani walitangaza uhuru wao mwaka1836 wakaundaJamhuri ya Texas iliyochukuliwa na Marekani mwaka1845 kuwa jimbo lake.

Hatua hii ilisababishaVita ya Marekani na Mexiko ya miaka18461848. Mexiko ikashindwa na kaskazini yote ikawa sehemu ya Marekani (Kalifornia,New Mexico,Arizona,Nevada,Utah naColorado, jumlatheluthi moja ya eneo lake lote.

Mexiko ilishambuliwa mara mbili naUfaransa kutokana na madai juu yamadeni ya taifa kwaraia aubenki za nje. Kwenyevita ya keki (1838-1839) Ufaransa ilidai fidia kwa uharibifu uliotokea katika duka la keki la Mfaransa mjini Mexiko namanowari za Ufaransa zilishambulia bandari za Mexiko hadi rais wake kukubali deni hili.

Mashambulio makubwa zaidi yalifuata mwaka1861. Mexiko ilishindwa kulipa madeni kwa mataifa ya nje. Ufaransa chini yaNapoleon III iliamua kufanya Mexiko nusu-koloni yake; jeshi la Ufaransa ilivamia nchi, kufukuza serikali na kumwekaMwaustriaMaximilian I kama "Kaisari wa Mexiko". Serikali ya raisBenito Juarez ilipinga uvamizi huu kwa njia ya vita ya wanamgambo na mwaka1866 Wafaransa walipaswa kuondoka tena, Maximilian aliuawa mwaka1867.

Karne ya 20

[hariri |hariri chanzo]

Utawala wa raisPorfirio Díaz uliendelea kwa miaka zaidi ya 30 na kuwasha moto yamapinduzi ya Mexiko alipojaribu kushinda tena kwa udanganyifu mwaka1910.

Miaka hadi 1921vita ya wenyewe kwa wenyewe iliharibu sehemu kubwa za nchi. Kuna makadirio ya kwamba wananchi milioni 1,5 (kati ya milioni 15) waliuawa na zaidi ya 200,000 walikuwawakimbizi, hasa kwenda Marekani[7].

Mwaka1917 katiba mpya ya nchi ilitolewa na mkutano wa bunge maalumu. Katiba hii ilikuwa katiba ya kwanza duniani kutangazahaki za kijamii. Hizo haki zililenga kutunza na kuboresha hali ya wananchi wenye maisha magumu kama wafanyakazi na wakulima dhidi yamabepari na wenye mashamba makubwa[8]. Katiba hii iliweka mamlaka nyingi mikononi mwa rais wa taifa anayechaguliwa na wananchi wote kwa kipindi kimoja cha miaka 6, halafu hawezi kuchaguliwa tena. Shabaha nyingine ya vifungu katika katiba ilikuwa kupunguza uwezo wa Kanisa Katoliki kuathiri siasa na jamii na hatimaye kukomeshaimani hiyo.

Siasa hii dhidi yaUkristo iliendelea chini ya rais Calles na kusababisha kipindi kingine cha vita vya wenyewe kwa wenyewe miaka ya1926-1929. Katika mapigano hayo yaliyoitwaLa Cristiada wakulima wengi walichukua silaha kwa jina laKristoMfalme dhidi ya jeshi la serikali ili kuteteauhuru wa dini, wakipinga kufungwa kwamakanisa, kuzuiwaibada mbalimbali za hadhara na kuuawa kwa mapadre kamaMtakatifuKristofa Magallanes na wenzake. Vita hivyo vilisababisha vifo 250,000 na idadi hiyohiyo ya wakimbizi waliojisalimisha Marekani.

Baada ya mapinduzi mamlaka ilichukuliwa na Chama cha kitaifa cha mapinduzi (Partido Nacional Revolucionario PNR) kilichoendelea kutawala kwa miaka 71 kuanzia 1929 hadi2000.

Watu

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi ni 129,875,529: wengi wao ni machotara wenyedamu yaWahindi wekundu (31/55% hivi) naWazungu (42/65% hivi). Wenye asili yaUlaya tu ni 9/18%. Wenye asili yaAfrika ni 2%.

Ni nchi ya kwanza duniani kwa wingi wa watu wanaotumialugha yaKihispania ambayo nilugha ya taifa, lakini wengine (9.8/14.9%) wanaendelea kutumia lugha asilia tangu kabla yaukoloni kama vileNahuatl,YukatekMaya,Mixtek naZapotek.

Nchini wanaishi Wamarekani milioni 1, halafuwahamiaji wengine kutoka Amerika ya Kati,Lebanon, nchi nyingine zaAsia n.k. Kinyume chake, Wameksiko 13 milioni wako Marekani, na raia wengine 23 milioni wa nchi hiyo wana asili ya Meksiko.

Upande wadini walio wengi ni wafuasi waYesu Kristo katikaKanisa Katoliki (77.7%) aumadhehebu mengine (11.2%). Ni nchi ya pili duniani kwa wingi wa Wakatoliki, baada yaBrazil, na karibunusu kati yao wanashirikiibada kilawiki. Wasio na dini ni 8.1%.

Majimbo ya Mexiko

[hariri |hariri chanzo]
  1. Aguascalientes
  2. Baja California
  3. Baja California Sur
  4. Campeche
  5. Chiapas
  6. Chihuahua
  7. Coahuila
  8. Colima
  9. Durango
  10. Guanajuato
  11. Guerrero
  12. Hidalgo
  13. Jalisco
  14. Mexico
  15. Michoacán
  16. Morelos
  17. Nayarit
  18. Nuevo León
  19. Oaxaca
  20. Puebla
  21. Querétaro
  22. Quintana Roo
  23. San Luis Potosí
  24. Sinaloa
  25. Sonora
  26. Tabasco
  27. Tamaulipas
  28. Tlaxcala
  29. Veracruz
  30. Yucatán
  31. Zacatecas
Ramani ya Mexiko

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. Michael S. Werner (January 2001). Concise Encyclopedia of Mexico. Taylor & Francis. pp. 386–. ISBN 978-1-57958-337-8
  2. A single domestication for maize shown by multilocus microsatellite genotyping, Proc Natl Acad Sci U S A. 2002 Apr 30; 99(9): 6080–6084. doi: 10.1073/pnas.052125199
  3. ""The Evolution of Corn". University of Utah HEALTH SCIENCES. Retrieved 2 January 2016". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2016-04-01. Iliwekwa mnamo2016-03-20.
  4. "Architecture, Astronomy, and Calendrics in Pre- Columbian Mesoamerica, Vincent H. Malmstrom"(PDF). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo(PDF) mnamo 2006-11-03. Iliwekwa mnamo2016-03-21.
  5. Teotihuacan, Department of Arts of Africa, Oceania, and the Americas, The Metropolitan Museum of Art October 2001
  6. Ndui ilikuwa ugonjwa iliyokuwa kawaida katika Ulaya wakati ule lakini ilikuwa ugonjwa mgeni kwa wenyeji wa Amerika ambao walikosa kinga dhidi yake; hivyo ilikuwa kati ya magonjwa wa kuambukizwa kutoka Ulaya yaiyoua Waindio wengi katika karne zilizofuata.
  7. Robert McCaa, "Missing millions: the human cost of the Mexican Revolution." Mexican Studies 19#2 (2001)
  8. Akhtar Majeed, Ronald Lampman Watts, and Douglas Mitchell Brown (2006). Distribution of powers and responsibilities in federal countries. McGill-Queen's Press. p. 188. ISBN 0-7735-3004-5.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  • Camp, Roderic A.Politics in Mexico: Democratic Consolidation Or Decline? (Oxford University Press, 2014)
  • Davis, Diane.Urban leviathan: Mexico City in the twentieth century (Temple University Press, 2010)
  • Domínguez, Jorge I (2004). "The Scholarly Study of Mexican Politics".Mexican Studies / Estudios Mexicanos.20 (2): 377–410.
  • Edmonds-Poli, Emily, and David Shirk.Contemporary Mexican Politics (Rowman and Littlefield 2009)
  • Kirkwood, Burton.The History of Mexico (Greenwood, 2000)online editionIlihifadhiwa 24 Desemba 2009 kwenyeWayback Machine.
  • Krauze, Enrique (1998).Mexico: Biography of Power: A history of Modern Mexico 1810–1996. New York: Harper Perennial. uk. 896.ISBN 0-06-092917-0.
  • Meyer, Michael C.; Beezley, William H., whr. (2000).The Oxford History of Mexico. Oxford University Press. uk. 736.ISBN 0-19-511228-8.
  • Levy, Santiago.Good intentions, bad outcomes: Social policy, informality, and economic growth in Mexico (Brookings Institution Press, 2010)
  • Meyer, Michael C., William L. Sherman, and Susan M. Deeds.The Course of Mexican History (7th ed. Oxford U.P., 2002)online editionIlihifadhiwa 2 Februari 2011 kwenyeWayback Machine.
  • Russell, Philip (2010).The history of Mexico: from pre-conquest to present.Routledge.ISBN 978-0-415-87237-9. Iliwekwa mnamoJulai 9, 2010.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  • Tannenbaum, Frank.Mexico: the struggle for peace and bread (2013)
  • Werner, Michael S. ed.Encyclopedia of Mexico: History, Society & Culture (2 vol 1997) 1440pponline editionIlihifadhiwa 24 Januari 2010 kwenyeWayback Machine.
    • Werner, Michael S. ed. Concise Encyclopedia of Mexico (2001) 850pp; a selection of unrevised articles

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Meksiko&oldid=1422699"
Jamii:
Jamii zilizofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp