Jina la Mbeya limetokana naneno laKisafwa "Ibheya" ambayo maana yake nichumvi, kwani miaka mingiwafanyabiashara walikuwa wanafika mahali hapo kubadilishana mazao yao kwa chumvi.
Mlima mkubwa ulio karibu ulijulikana kwa jina la "Mbeya"[1] wakati waukoloni wa Kijerumani, na mji ulipokea baadaye jina kutokana na mlima huu.
Mji wa kisasa wa Mbeya ulianzishwa nawakoloniWaingereza mnamo mwaka1927. Wakati uledhahabu ilianza kupatikana mlimani karibu na Mbeya hadiChunya.
Mji ulianzishwa katika sehemu zinazoitwa bado Uhindini, Uzunguni na Majengo. Mji ulipangwa kufuatana na kawaida ya miji wa kikoloni yaAfrika ya Mashariki kuwa na sehemu tatu:
Mahali pamakanisa ya kale panaonyesha ugawaji huu wa kihistoria:
Kanisa laAnglikana lililokuwadhehebu rasmi laUingereza lipo chini ya Uzunguni na karibu na ofisi za kiserikali (zinazoelekea siku hizi kuhamishwa kwendaForesti) kamaMkuu wa Mkoa na mahakama. Kanisa hili nijengo dogo kwa sababu lilipangwa kwa kundi dogo la maafisa na wafanyabiashara pamoja nawakulima Waingereza wa Mbeya.
Kanisa la mjini laMoravian, ambalo ni dhehebu laKikristo asilia la Mbeya liko Majengo iliyokuwa sehemu kwa Waafrika. Kati ya Waingereza hawakuwepo Wamoravian.
Kanisa KuuKatoliki lilihudumia Wazungu wachache, hasaWaeire, kati ya wakoloni pamoja na Wahindi kutokaGoa na pia Waafrika: kwa hiyo iko kati ya Uzunguni na Uhindini karibu na Majengo.
Mji uliendelea kupanuka pande zote. Barabara kuu yaTANZAM inaunganisha sehemu za nje kati ya Uyole na Mbalizi.
Vilevile njia yareli yaTAZARA hupita Mbeya kuelekea Zambia. Kunaghala kubwa kwa ajili ya mizigo ya Malawi inayofikishwa kwa reli kutoka Dar es Salaambandarini ikihamishwa kwamalori kwenda Malawi.
Mbeya imekuwa nauwanja wa ndege mdogo usiokuwa nahuduma ya kawaida kwa muda mrefu. Lakini kuna mipango ya kujenga uwanja mpya hukoSongwe zipatazo km 40 kufuata njia ya kwenda Zambia.
Tangumiaka ya 1990 kitovu cha mji kinahamishwa kutoka eneo la zamani kwenda karibu na barabara kuu ya Dar es Salaam – Zambia.
Mbeya ni mji wa nne kwa ukubwa nchiniTanzania.Idadi ya wakazi imehesabiwa kuwa 385,279 katikasensa yamwaka 2012. Katikasensa ya mwaka2022 walihesabiwa 541,603[2]. Wengine 300,000 hivi wanaishi katika mazingira karibu na Mbeya mjini.
Uchumi wa Mbeya mjini umetegemeakilimo cha mazingira yake na biashara.
Viwanda mbalimbali vilianzishwa, lakini havikufaulu sana. Kuna viwanda kwa mfanoZana za kilimo, Highland Soap, Mbeya Textiles. Mbeya Ceramics iliporomoka kitambo.
Makala hii kuhusu maeneo yaMkoa wa Mbeya bado nimbegu. Je unajua kitu kuhusuMbeya (mji) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.