Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Mawese

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tunda la mchikichi

Mawese nimafuta ya kula yanayotolewa katikamatunda yamti wamchikichi (Elaeis guineensis). Ni mafuta ya kupikia yaAfrika, hasa penye asili ya mchikichi kutokana na kupatikana kwa wingi katika nchi za kanda yaGuinea.

Mawese kutokana na nyama ya tunda

[hariri |hariri chanzo]

Kuna aina mbili za mawese; mawese hasa hutolewa na nyama ya tunda, inaranginyekundu navitamini nyingi. Inatumika kama mafuta ya kupikia ama moja kwa moja ikitolewa nawakulima wenyewe na kuonyesha rangi nyekundu. Kama mawese inatengenezwakibiasharakiwandani rangi inaondolewa kwa njia ya kusafisha mafuta kwenye vichujio. Baada ya kusafishwa huwekwa kwenyemakopo auchupa na kuuzwamadukani au kupelekwa nje. Mafuta haya yanatumika pia viwandani kwa kutengeneza majarini,sabuni,mishumaa, mafuta ya kupakaa mwilini na aina mbalimbali ya madawa na urembaji.

Dizeli ya mawese

[hariri |hariri chanzo]

Mawese hutumika piakiteknolojia tangu miaka ya nyuma kwa kutengenezadizeli. Hasa nchiniMalaysia teknolojia hii imesonga mbele. Malaysia inajaribu kupunguzagharama za kununuapetroli nadizeli kwa kutengeneza kiwanda kikubwa cha kusafisha mawese kuwa dizeli.Sheria ya Malaysia inadai kuanzia mwaka2007 ya kwamba dizeli yote inayouzwa nchini iwe na 5% dizeli ya mawese.

Mawese kutokana na kiini cha tunda

[hariri |hariri chanzo]

Aina ya pili ni mafuta yanapatikana katika kiini cha tunda. Haya baadhi ya wenyeji huyaita mafuta ya mise. Mafuta haya yanahalijoto ya kuyeyuka kwenye 26 – 28. Hivyo kwa kawaida ni imara, si majimaji. Inatumika katika viwanda vya vyakula lakini pia kwamajarini. Yanatumika pia sana katika madawa ya urembaji na madawa ya kusafishia. Hata viwanda vya kutengenezaalumini hutumia aina hii ya mawese. Kuna biashara kubwa ya viini vya mchikichi (mise) kwa sababu husafirishwa bila kuharibu mafuta ndani yake.

Matatizo kutokana na matumizi makubwa

[hariri |hariri chanzo]

Nchi zinazopanda michikichi hasa niMalaysia naIndonesia zenye mavuno ya 80% ya mawese yotr duniani.Brazil naKolumbia ziemanza vilevile kupanda michikichi kwa wingi.Uthai,Papua–Guinea Mpya na nchi zaAfrika ya Magharibi zinachangiaasilimia ndogo kwenyesoko la dunia ya mawese.

Kwa jumlamawese ina nafasi ya pili duniani kati ya mafuta kutokana namimea inayotumika zaidi baada ya mafuta yasoya.

Mawese katika historia ya Afrika ya Magharibi

[hariri |hariri chanzo]

Mawese ilikuwa muhimu sana katikauchumi nahistoria ya Afrika ya Magharibi wakati wakarne ya 19BK.Ulaya iliingia katikamapinduzi ya viwandani ikahitaji mafuta ya kutiagrisi kwa ajili yamashine za viwanda vyake. Mafuta haya yalipatikana katika nchi za Guinea hasa eneo ladelta ya Niger.

Kiuchumi kwa nchi za Afrika ya Magharibi biashara ya mawese ilichukua nafasi yabiashara ya watumwa; hadi mwanzo wa karne ya 19 falme za pwani zilitajirika kwa kuwauziawafanyabiasharaWazunguwatumwa kwa ajili ya masoko yaAmerika.

Biashara hii ya watumwa ilipigwa marufuku polepole. Mabadiliko ya sheria katikaUingereza yalitangulia. Mapatano ya kimataifa kwenyeMkutano wa Vienna mwaka1815 yalipakana biashara hii ikapungua hadi kwisha.

Umuhimu mpya wa Afrika ya Magharibi kwa ajili ya Ulaya ulikuwa mafuta ya mawese. Hasa viini vilipelekwa Ulaya kwa sababu mawese asilia huharibika haraka. Kabla ya kuwepo kwa viwanda Afrika kwenyewe viini viliweza kusafirishwa mbali bila kuharibu mafuta ndani yake. Mawese ya tunda lenyewe linaharibika kama haitengenezwi kwa kufuatambinu mbalimbali zinazopatikana kiwandani lakini si rahisi kuzitumia katikauzalishaji wa kienyeji.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]

Athari za kijamii na za kiikolojia za matengenezo ya mawese

[hariri |hariri chanzo]

Habari nyingine za mawese

[hariri |hariri chanzo]
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Mawese&oldid=1321291"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp