Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Jicho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutokaMacho)
Jicho la binadamu.
Macho ya kuungwa ya nzi.

Jicho ni sehemu yamwili inayowezesha kuona. Niogani inayotambuamwanga na kutumahabari zake kwaubongo.

Aina za macho ya viumbehai

[hariri |hariri chanzo]

Kuna mifumo mbalimbali ya macho kati ya aina mbalimbali zawanyama.

Macho ya kimsingi kwaviumbehai vidogo yanatambua tu kamamazingira yana mwanga au la. Hata kati ya viumbehai wenyeseli moja kuna wenyeprotini zinazotofautishagiza nanuru. Kunakonokono ambao hawawezi "kuona"picha ya mazingira lakini wanatambua mwanga na uwezo huu unawawezesha kuepukana na mwanga wajua ambao ungewakausha.

Macho yaliyoendelea kiasi yanaumbo kamakikombe na hili linawezesha kutambua upande gani nuru inatokea.

Wanyama wengi huwa na macho yaliyoendelea zaidi: yana uwezo wa kuona picha halisi ya mazingira pamoja narangi namwendo.

Jicho la nzi (drosophila) chini yahadubini;lenzi ya kilaomatidi inaonekana kamanusu tufe.

Macho ya kuungwa

[hariri |hariri chanzo]

Wadudu naarthropoda huwa namacho ya kuungwa na vijicho vingi vidogo vinavyoitwaomatidi; kila kijicho huwa na umbo lakijiti na kwenye mwisho wake kuna lenzi yachitini. Mdudu anaweza kuwa na vijichoelfu kadhaa na picha ya mazingira inaunganishwa kutokana na picha nyingi ndogo za kila kijicho.

Macho haya ya kuungwa yanamwezesha mdudu kuangaliaasilimia kubwa ya mazingira yake: kwa aina kadhaa hata nyuma yake. Macho ya kuungwa yanaweza kufunika hadi asilimia 80 ya eneo lakichwa. Mdudu haoni vikali kama mtu lakini anaona mabadiliko na mwendo haraka sana.

Wanyama wanaoishi katikavilindi vyabahari penye giza nene huwa na macho ambamofuwele ziko kamakioo na kupazia nuru hafifu.

Kuna wanyama wanaoweza kuona nuru ambayo ni nje yaupeo wa kibinadamu; kwa mfanonyuki huonamnururisho wainfraredi.

Macho ya mamalia

[hariri |hariri chanzo]

Macho yabinadamu kama yamamalia wengine huwa na lenzi moja tu. Lakinimuundo wa jicho unaruhusu kuona rangi,umbali na mengi madogo.

Shida za macho

[hariri |hariri chanzo]

Shida za macho ni nyingi kama vileupofu, kutoonarangi, macho kujiliza, wekundu uliokithiri pamoja na kutoa majimaji. Shida hizo huletwa navumbi, kuzaliwa ukiwakipofu,jua jingi bila kuvaliamiwani vizuia jua.

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Makala hii kuhusu mambo yaanatomia bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuJicho kama matumizi yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Jicho&oldid=1297443"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp