Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Litania

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Shemasi waKiorthodoksi akiongoza litania akishika ncha yaorarion yake kwa mkono wa kulia ili kuiinua kila anapomaliza ombi mojawapo.

Litania ni aina yasala yaUkristo ambayo upekee wake ni kuwa na mfululizo wa maneno ya sifa na maombi ambayo yanaitikiwa na mkusanyiko kwa namna iliyopangwa, kwa kawaida ya kujirudiarudia.

Jina linatokana na neno laKigirikiλιτανεία (litaneía), linalotokana naλιτή (litê), yaani "dua".

Mtindo huo wa kusali ulistawi kuanziaAntiokia ukaenea kwanza Mashariki halafu Mashariki hasa katikakarne IV.

Mfano wa litania fupi katikaliturujia niMwanakondoo wa Mungu inayotumika katikaMisa, na litania ndefu nilitania ya watakatifu inayotumika katika ibada muhimu kadhaa, kama vileupadrisho.

Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Litania&oldid=895613"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp