Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Kilatini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutokaLat.)
Kilatini
Lingua Latina (la)
Lugha
AsiliItalia (Dola la Roma)
Wasemaji

L1 : Hakuna wasemaji wa asili
L2: Takriban milioni moja (wasemaji wa Kilatini cha kisasa)

Jumla: ~1 milioni
Familia za lughaKihindi-Kiulaya
Kilatini-Kihispania
Kilatini-Faliski
Aina za AwaliKihindi-Kiulaya cha Kale
Kilatini cha Kale
Kilatini cha Kawaida
Mfumo wa kuandikaAlfabeti ya Kilatini
Lugha Rasmi
Lugha rasmi kwaMji wa Vatikani
Nambari za Msimbo
ISO 639-1la
ISO 639-2lat
Glottologlati1261
Nahau ya Kilatini ("Kukosa ni jambo la kibinadamu").

Kilatini(Lingua Latinala) ni lugha ya kale yaKihindi-Kiulaya ambayo ilizungumzwa katikaDola la Roma. Ilianza kama lugha ya eneo la Lazio nchiniItalia na baadaye ikawa lugha kuu ya utawala waKirumi, ikienea koteUlaya kupitia upanuzi waDola la Roma. Ingawa haizungumzwi tena kama lugha ya asili, Kilatini bado hutumika katika taasisi za kidini, sayansi, sheria, na elimu ya juu, hasa katika Mji wa Vatikani na taasisi za kitaaluma. Lugha za Kirumi kamaKihispania,Kifaransa,Kiitaliano,Kireno, naKiromania zilichipuka kutoka Kilatini cha Kawaida (Vulgar Latin), ambacho kilitumiwa na watu wa kawaida katika Milki ya Roma

Historia

[hariri |hariri chanzo]
Ramani ya uenezi walugha za Kirumi za leo zilizotokana na Kilatini.

Kilatini kilikuwalugha hai takriban kati ya miaka500 KK na600BK na baadayelahaja zake mbalimbali ziliendelea na kukomaa kuwa lugha za pekee zinazojulikana kamalugha za Kirumi, kamaKiitalia,Kifaransa,Kihispania,Kireno,Kiromania n.k.

Kilatini ni piajina lamwandiko au aina yaherufi (alfabeti ya Kilatini) inayotumika kwa lugha nyingiduniani. HataKiswahili huandikwa siku hizi kwa herufi za Kilatini kama kwa mfano ukurasa huu waWikipedia.

Kilikuwa

Hadi leo Kilatini ina athira kubwa katika lugha yasayansi naelimu. Hadi leo hufundishwa mashuleni hasa Ulaya. Tena ni

Urithi wa Kilatini katika Kiswahili

[hariri |hariri chanzo]

Kiswahili kimerithimaneno yenyeasili ya Kilatini hasa kupitiaKiingereza kilichopokea karibuasilimiahamsini ya maneno yake yote kutoka Kilatini kupitia hasa Kifaransa. Maneno mengine ya Kilatini yameingia Kiswahili kupitia Kireno, Kifaransa n.k.

Mifano:

Kilatini cha kisasa

[hariri |hariri chanzo]
Systema Naturae nikitabu maarufu kilichoandikwa mnamo mwaka1735 kwa Kilatini naCarl Linnaeus. Ni msingi wauainishaji wa kisayansi wamimea nawanyama hadi leo

Kilatini kilikuwa na upanuzi mkubwa kuanziakarne ya 16; misingi ya sayansi ya kisasa ilijadiliwa katikaUlaya kwa Kilatini kilichokuwa lugha ya vyuo vikuu kote Ulaya. Katikakarne ya 18 na19mataifa mengi yaliimarisha lugha zao na kuzitumia kwa ngazi zote za elimu. Lakiniwataalamu wa Ulaya naMarekani waliendelea kutumia majina ya Kilatini kwa kutaja habari za kisayansi na kubuni majina mapya kufuatana na kanuni za Kilatini kwa kutaja vitu na viumbe vilivyotambuliwa na kuelezwa kisayansi. Kazi hii iliendelea hata wakati matumizi ya Kilatini kama lugha ya kujadiliana yalishafikia mwisho wake.

Katikakarne ya 20 kulikuwa na harakati ya wapenzi wa lugha kuundamisamiati ya "Kilatini cha Kisasa" yenye maneno kwa ajili ya mitambo ya kisasa,mtandao n.k.Wikipedia ya Kilatini ilifikia makala zaidi ya 130,000 kwenye mwaka2019.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mambo yalugha bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuKilatini kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Kilatini&oldid=1404527"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp