Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Kurani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutokaKorani)
Sehemu yamfululizo wa makala juu ya

Uislamu

Imani na ibada zake

Umoja waMungu
Manabii
Misahafu
Malaika
Uteule
Kiyama
Nguzo za Kiislamu
ShahadaSwalahSaumu
HijaZaka

Waislamu muhimu

Muhammad

Abu BakrAli
Ukoo wa Muhammad
Maswahaba wa Muhammad
Mitume na Manabii katika Uislamu

Maandiko na Sheria

AzifQur'anSunnahHadithi
Wasifu wa Muhammad
Sharia
Elimu ya Sheria za KiislamuKalam

Historia ya Uislamu

Historia
SunniShi'aKharijiyaRashidunUkhalifaMaimamu

Tamaduni za Kiislamu

ShuleMadrasa
TauhidiFalsafaMaadili
Sayansi
SanaaUjenziMiji
KalendaSikukuu
Wanawake
ViongoziSiasa
Uchumi
UmmaItikadi mpyaSufii

Tazama pia

Uislamu na dini nyingine
Hofu ya Uislamu

Kurani (kwaKiarabu: القرآن,Qur'an) nikitabu kitukufu chaUislamu ambacho kinaaminiwa naWaislamu kuwa ni "Neno laAllah (Mwenyezi Mungu)". Kitabu hicho kwao ni tofauti kabisa namaandiko yadini nyingine kwa maana hicho kinaaminika kwamba kimeandikwa moja kwa moja na Mwenyezi Mungu, kupitiamtume wake wa mwisho,Muhammad.

Kadiri ya Kurani (42:8), Mungu alimuambia Muhammad: "Na namna hivi tumekufunulia Kurani kwa Kiarabu ili uwaonye watu waMakka na walio pembeni mwake"

Kurani imeandikwa na kusomwa kwalugha yaKiarabu pekee kwa zaidi ya miaka 1,445.

Lakini, kwa vile leo Waislamu walio wengi ulimwenguni hawajui Kiarabu, maana halisi ya Kurani hutolewa kwalugha nyingine, hivyo kupelekea wasomaji kuelewa vyema yale maneno ya Kiarabu kwenye Kurani yana maana gani. Vitabu hivyo ni kamakamusi kwa ajili ya Kurani - hawavisomi hivi kama moja ya sehemu ya Kurani na Waislamu, ili kuwa badala ya Kurani ya Kiarabu.

Waislamu wengi wanaamini kwambatafsiri ile si ya Kurani tukufu wala si ya kweli; ni nakala ya Kiarabu tu iliyotolewa kwenye Kurani ya kweli.[1]

Waarabu wa kabla ya Uislamu waliundahadithi na hadithi juu yamiti,visima namilima, na waliundaibada zinazohusiana namiamba na milima huko Safa, Marwa, Abu Kubeys, Arafat, Mina na Muzdalifah. Ingawa Kurani ilifuta ibada nyingine, haikupingana na maandiko ya Kiarabu yenye mizizi, badala yake, iliendeleza sana ibada hizo.[2] Wakati mwingine inakuwa vigumu kuelewa Kurani bila kujua mazoea ya zamani; kihistoria, wanadamu hawakutumia kipimo chawakati kikubwa kulikomwezi. Hivyo, mtu ambaye alisema, "Ninaumri wa miaka 200." alikuwa akihesabu miezi, sio miaka. Kwa kweli alikuwa na umri wa miaka 16.[3] "Tulimpeleka Nuhu kwa watu wake na akakaa kati yao kwa miaka elfu, isipokuwa miaka hamsini." (Ankebut: 14)

Kwa kuongezea vyanzo vilivyoandikwa, masomo mengi na mashujaa, ambayo mengine ni tu katika utamaduni wa hadithi za Kiarabu, yamefunikwa kwa kifupi katika lugha ya Kurani, na marejeo madogo yanafanywa. Hadithi za Yusuf na Züleyha, İsa, Musa, İskender / Zülkarneyn ni hadithi ndefu zaidi. Hadithi za uumbaji na mafuriko, ibada ya Ibrahimu na Dhabihu, hadithi za manabii wa Kiebrania, imani ya Kiyahudi na historia, kama vile kutoka kwa Waisraeli kutoka Misri, zinachukua nafasi kubwa katika Kurani.

Historia

[hariri |hariri chanzo]
Sura ya kwanza ya Kurani tukufu. Sura hii imeandikwa kwa Kiarabu.
Petra. Kulingana na mtafiti wahistoria ya Kiislamu naakiolojiaDan Gibson, hapa ndipo mahali ambapo Mohammed aliishiujana wake na kupokea mafunuo yake ya kwanza. Kama misikiti ya kwanza ya Waislamu namakaburi yanavyoonyesha, pia ulikuwa mwelekeo wa kwanza (Kibla) wa Waislamu.[4][5]Patricia Crone naMichael Cook walidhani, kulingana na maandishi na utafiti wa akiolojia, kwamba "Masjid al-Haram" haikuwepo Maka, lakini katika Rasi ya kaskazini magharibi mwa Arabia.[6]

Waislamu wanaamini kwamba Kurani mtume Muhammad alipewa namalaikaJibrīl kwenye pango la mlimaHira, kwa kipindi cha zaidi ya miaka ishirini na tatu hadi mauti yake ilipomfikia.

Kurani haikuwa kitabu cha maandiko wakati wa uhai wa mtumeMuhammad; iliwekwa kwa mawasiliano ya kimdomo tu. Bimaana, watu walihifadhi kichwani.

Mtume labda hakuwa anajua kusoma wala kuandika, lakini kwa mujibu wa Waislamu, swahaba wakeAbu Bekr alikuwa akiandika maandiko yale juu ya kitu fulani wakati huo mtumeMuhammad yu hai. Pale Abu Bekr alipokuja kuwa khalifa, ameileta Kurani na kuwa kitabu kitakatifu.

Uthman, ambaye ni khalifa wa tatu, ameondoa vipengele ambavyo vilikuwa havihusiani na Kurani tukufu.

Elementi, Sura, Mistari, Aya

[hariri |hariri chanzo]

Kuna sehemu 30 katika Kurani, ambayo inafanya kuwa nasura 114. Kila sura ina namba tofauti ya mistari.

Kwa mujibu wa mafunzo ya Kiislam, sura 86 kati ya hizi zimeshuka mjiniMakka, sura 24 kati ya hizi zimeshuka mjiniMadina.

Miongoni mwa sura zilizoshushwa mjiniMedina ni pamoja na Al-Baqara, Al Imran, Al-Anfal, Al-Ahzab, Al-Ma'ida, An-Nisa, Al-Mumtahina, Az-Zalzala, Al-Hadid, Muhammad , Ar-Ra'd, Ar-Rahman, At-Talaq, Al-Bayyina, Al-Hashr, An-Nasr, An-Nur, Al-Hajj, Al-Munafiqun, Al-Mujadila, Al-Hujraat, At-Tahrim, At-Taghabun, Al-Jumua, As-Saff, Al-Fath, At-Tawba, Al-Insan.

Mahusiano baina ya Kurani na Biblia

[hariri |hariri chanzo]
Safina ya Nuhu, Zubdetü't-Tevarih. Kulingana na wasomi huria, hadithi ya mafuriko ya Gilgamesh imekopwa kutoka kwa Wababeli na kutafsiriwa tena katikaTorati na katikaKurani.[7][8][9]
Mchoro waLawrence Alma-Tadema: Kuokolewa kwa Musa kutoka Mto Nile kunatajwa mara 136 katika Kurani; hadithi hiyo ni kama ile ya mfalmeSargon Mkuu hukoAkkad. (Qasas Sura 7-9 / Kutoka 1:15-22).

Katika Qu'ran , inasomwa kwambaWayahudi naWakristo pia huamini Mungu wa kweli. Dini hizo pamoja naUislamu huitwaDini za Abrahamu kwa sababu ya mahusiano hayo.

Kuna baadhi ya kurasa za Qu'ran zinazoelezeahabari za mambo ya watu wa katikaBiblia. Kwa mfano watu wa katika Biblia waliotajwa kwenye Qu'ran ni pamoja naAdamu,Nuhu,Abrahamu,Lutu,Ismaili,Yakobo,Yosefu,Haruni,Musa,mfalme Daudi,Solomoni,Elisha,Yona,Ayubu,Zekaria,Yohane Mbatizaji,Bikira Maria naYesu.

Hata hivyo, kuna tofauti za muhimu kabisa baina ya Uislamu na toleo la Biblia katika kuelezea habari za aina moja. Kwa mfano, Qu'ran inaelezea kwambaYesu Kristo siMwana wa Mungu, kama jinsi Wakristo wanavyoamini; kwa Waislamu, alikuwanabii tu, anayeheshimiwa kwa jina laIsa bin Mariamu.

Uislamu unafundisha kwamba haya yanatokea kwa sababu maandiko ya awali ya Biblia yamepotea na hivyo kuna baadhi ya watu wameyabadilisha. Lakini nje ya Qu'ran hakuna uthibitisho wa fundisho hilo.

Ilipokaribia saa ya kuzaa,Bikira Mariamu alitikisamtende ili kupatamatunda mapya. Habari kama hiyo haipatikani katikaBiblia ya Kikristo[10]

Kurani na ulimwengu wa leo

[hariri |hariri chanzo]

Sheria zinazotegemea matamshi na ufafanuzi wa Kurani ni shida leo kuzilinganisha nahaki za binadamu, usawa wa kijinsia na dini ya binafsi na uhuru wa kusema.[11]

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. Qur'an, Encyclopedia Britannica, retrieved on 8 Januari 2009
  2. https://www.researchgate.net/publication/317604040_Cahiliye_Arap_Hac_Rituellerinin_Kur'an'daki_Menasikle_Diyalektik_Iliskisi/link/5e20c19d458515ba208de0a1/download
  3. https://evrimagaci.org/zamani-olcmek-gun-hafta-ay-yil-kavramlari-nasil-olustu-7715
  4. Dan Gibson: Qur'ānic geography: a survey and evaluation of the geographical references in the qurãn with suggested solutions for various problems and issues. Independent Scholars Press, Surrey (BC) 2011,ISBN 978-0-9733642-8-6
  5. https://www.mdpi.com/2077-1444/11/3/102/htm
  6. https://dergipark.org.tr/tr/download/article-file/592002
  7. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2018-07-01. Iliwekwa mnamo2021-07-09.
  8. https://dergipark.org.tr/tr/download/article-file/557354
  9. https://www.icr.org/article/noah-flood-gilgamesh
  10. Leirvik 2010, pp. 33–34.
  11. https://www.iusinitinere.it/clash-between-sharia-law-and-human-rights-in-light-of-pace-resolution-2253-23827

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu kitabu fulani bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuKurani kama Mwandishi wake, hadithi au matoleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Kurani&oldid=1402881"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp