Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Kisirili

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Kisirili ni aina yamwandiko aualfabeti inayotumiwa kuandikalugha mbalimbali zaUlaya ya Mashariki naAsia ya Kati, kwa mfanoKirusi,Kiserbia,Kitajiki.

Mwandiko kwa ajili ya lugha za Kislavoni

[hariri |hariri chanzo]

Jina limetokana nammonaki namtaalamuMgirikiMt. Sirili (827 -14 Februari869) aliyesemekana aliunda namna hiyo ya mwandiko kwa ajili yalugha za Kislavoni pamoja na mdogo wakeMt. Methodio.

Hali halisi hawakuanzisha aina hii ya alfabeti lakini waliendeleza namna ya kuiandika iliyosaidia kusambaza mwandiko kati ya mataifa wasemaji wa lugha za Kislavoni. Lugha hizo zinasauti kadhaa ambazo hazinaherufi katika alfabeti yaKilatini. (Mwandiko wa Kilatini hutumiwa siku hizi kwa lugha nyingiduniani, zikiwa pamoja naKiswahili naWikipedia hii.)

Kuna lugha za Kislavoni, kama vileKipolandi,Kicheki naKikroatia, zinazoandikwa kwaalfabeti ya Kilatini, lakini kunaalama za nyongeza kwa ajili ya sauti za pekee za lugha za Kislavoni kwa mfano: "Č" kwa sauti ya "tsh" au "Ž" kwa aina ya "sh laini".

Alfabeti za Kisirili zinatofautiana kiasi kati ya lugha na lugha; kuna namna tofauti za kuandika sauti ileile au pia herufi za pekee kwa ajili ya sauti za pekee katika lugha fulani. Alfabeti inayotumiwa na watu wengi ni ya Kirusi inayoonyeshwa hapa.

Lugha za Kislavoni zinazoandikwa kwa alfabeti ya Kisirili ni:

Mwandiko wa lugha za Kiasia

[hariri |hariri chanzo]

Kutokana na athira yaUrusi katika Asia ya Kati kuna pia lugha mbalimbali za Kiasia ambazo zinaandikwa kwa mwandiko wa Kisirili tangukarne ya 19 au mwanzo wakarne ya 20. Nchi zinazohusika zilikuwa ama sehemu zaUmoja wa Kisovyet au nchi jirani kamaMongolia.

Lugha kadhaa za Kiasia zinazoandikwa siku hizi kwa alfabeti za Kisirili ni:

Mfano wa alfabeti ya Kirusi

[hariri |hariri chanzo]
Herufi za Kisirili
(kubwa / ndogo)
Herufi za Kilatini zinazolinganaMatamshi
А аA aa baba wangu
Б бB bbbaba
В вV vvvitabu
Г гG gg (w)gani, na uhuru kwakiukraine
Д дD dddada, ndogo
Е еE ee / ye Kwakirusi:yeye. Kwa lugha si kirusi: yeye.
Ё ёË ëyoYohane
Ж жŽ žsh lainikiingerezavision,Kifaransaje
З зZ zz maziwa
И иI ii kiswahili
Й йJ ji fupiyeye
К кK kkkaka
Л лL lllakini,italiki
М мM mmmaziwa,mtoto, damu
Н нN nnnani
О оO oo mtoto,kifaransal'eau
П пP pppole
Р рR rrrafiki
С сS sssisi
Т тT tt mtoto
У уU uuuhuru
Ф фF ff safari,fisi, rafiki
Х хKh khkama matamshi ya Kiarabu
"Alkhamisi" (Alhamisi) subulkheri
Ц цC ctskijerumaniZehn,kiitaliapizza,
Ч чČ čtsh (ky)chumba,kiingerezachair
Ш шŠ šshshamba
Щ щŜ ŝshtsh/kipolandi szcz~śś:ɕ:
Ъ ъ" (alama gumu)alama hii hunonyesha matamshi
„magumu“ ya herufi inayotanguulia
Ы ыY yY y[ɨ],[ʉ];kiingereza chaMarekaniroses
Ь ь(alama laini)alama hii huonyesha sauti
ya "y" baada ya herufi vyakula?
Э эÈ èe fupi ndege,kijerumaniZehn
Ю юÛ ûyuyunifomu,kiingerezauseful
Я я âyayangu
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Kisirili&oldid=1417008"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp