Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Keir Starmer

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Picha rasmi ya kiserikali ya Sir Keir Starmer.

Sir Keir Rodney Starmer (amezaliwa 2 Septemba1962) nimwanasiasa na wakili waUingereza ambaye amehudumu kamaWaziri Mkuu wa Uingereza tangu 5 Julai2024, na amekuwa kiongozi wa 19 waChama cha Labour tangu mwaka2020.[1] Pia aliwahi kuwaKiongozi wa Upinzani kutoka 2020 hadi 2024. Tangu mwaka2015, amekuwaMbunge wa Holborn na St Pancras, jimbo la ndani yaLondon. Starmer amechaguliwa tena kama Mbunge wa jimbo hilo katikauchaguzi mkuu wa2017 na wa2019.

Kiongozi wa Labour

[hariri |hariri chanzo]

Mnamo Januari 2020, Starmer alitangaza kugombea nafasi yaKiongozi wa Chama cha Labour katikauchaguzi wa 2020.[2] Mnamo 4 Aprili 2020, Starmer alichaguliwa kuwa kiongozi wa Chama cha Labour, na kwa kuwa Labour ilikuwa na idadi ya pili ya viti katikaBunge la Commons, alifanywa kuwaKiongozi wa Upinzani.[3] Alishinda uongozi wa Chama cha Labour katika raundi ya kwanza ya upigaji kura kwa kutumiambinu ya kura inayoweza kuhamishwa. Starmer alipata kura 275,780 (56.2%). Alipata asilimia 53.13% ya kura zawanachama wa vyama washirika, asilimia 56.07% ya kura za wanachama wa Chama cha Labour, na asilimia 78.64% ya kura za wafuasi waliosajiliwa.[4]

Maisha binafsi

[hariri |hariri chanzo]

Starmer nihaamini uwepo waMungu,[5] lakini amesema kuwa anaamini katika imani na nguvu yake ya kuwaleta watu pamoja. Mke wake, Victoria Alexander, niMyahudi, na watoto wao wawili wanalelewa katikaimani hiyo.[6]

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. "Starmer Is U.K.'s New Prime Minister".New York Times. 5 Julai 2024.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "Labour leadership: Sir Keir Starmer enters race" (kwa Kiingereza (Uingereza)).BBC News. 4 Januari 2020. Iliwekwa mnamo4 Januari 2020.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Keir Starmer Elected as new Labour leader".BBC News. 4 Aprili 2020. Iliwekwa mnamo4 Aprili 2020.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  4. "Leadership and Deputy Leadership election 2020 - Results".The Labour Party. 2023.Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 26 Machi 2023. Iliwekwa mnamo3 Oktoba 2023.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  5. Williams, Rhiannon (11 Aprili 2021)."Keir Starmer: I may not believe in god, but I do believe in faith".inews.co.uk (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo23 Januari 2023.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  6. Harpin, Lee (16 Novemba 2020). Simons, Jake Wallis (mhr.)."Starmer: Our kids are being brought up to know their Jewish backgrounds".The Jewish Chronicle [Kigezo:Separated entries].Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 25 Septemba 2022. Iliwekwa mnamo3 Oktoba 2023.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Keir_Starmer&oldid=1371311"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp