Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Kazi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Wachimbaji wamfereji wamaji kwenyemto Cedar,Washington (1899).
Wanawake wengi pamoja katika kazi yaofisini.
Mwanafalsafa kazini alivyoonyeshwa nasanamu yaAugust Rodin, "Le penseur" (= "Mwenye kufikiri").
Mfanyakazi akishughulikiamashine (picha yaLewis Hine,1920).

Kazi ni sehemu muhimu yamaisha yabinadamu, hivyo ina nafasi kubwa katikaanthropolojia,falsafa,teolojia,fizikia nasosholojia.

Inafafanuliwa kamautendaji unatumianguvu yaakili au yamwili ili kufikia lengo fulani, ambalo mara nyingi nifaida yakiuchumi ili kuweza na kuwezesha kuendelea kuishi.

Lakinithamani yake halisi haiishii katikauzalishaji wa vitu, bali inategemea hasa ustawishaji wautu katika vipawa vyake vyote kulingana namaadili namaisha ya kiroho.

Kwa msingi huo, niwajibu wa kila mtu aliyefikiaukomavu fulani.

Ni pia mchango muhimu katikajamii na inayostahili kuheshimiwa na kutunzwa na wote kuanziaserikali hadi watu binafsi.

Kwa kuwa ni wajibu, kazi ni vilevilehaki ya msingi ya binadamu. Bila kuwa nayo, mtu anaelekea kunyong'onyea na kujiona hama maana, hasa kamautovu wa kazi unadumu muda mrefu na kumzuia asiweze kupangamaisha yake, kwa mfano upande wandoa nafamilia, kwa sababu ya kutojitegemea.

Sheria mbalimbali zinaratibu mahusiano kazini, hasa kama kunamwajiri namwajiriwa.

Kazi katika Biblia

Biblia inazungumzia maisha halisi ya watu, hivyo haikuweza kuisahau kazi. Tokakitabu cha Mwanzo (1:1-2:4a) inaonyeshaheshima ya kufanya kazi kwa kumchoraMungu akitenda kazi kama binadamu kwasikusita, akipumzika ile yasaba.

Ndiye aliyewaagizaAdamu naEva wafanye kazi katikadunia ili kuistawisha (Mwa 2:15).

Baada yadhambi ya asili waliyoifanya wajibu huo umebaki, ila kamaadhabu sasa unachosha (Mwa 3:17-19).

Pamoja na hayo,Yesu alikubali kufanya kazi kwamikono yake kamafundi (labdaseremala) kwa sehemu kubwa kabisa ya maisha yake, alipoishi nafamilia yake au walaumama yakekijijiniNazareti (Mk 6:3).

Mtume Paulo alipinga kwa nguvuuzembe wa waliodai kazi haihitajiki tena kwa sababu eti,ufalme wa Mungu umefika. Aliandika, "Asiyetaka kufanya kazi, asile chakula" (2Thes 3:10).[1] Mwenyewe, pamoja na kuhubiriInjili alikuwa akiendelea na kazi yake yakushonamahema ili kupata mahitaji yake bila kulemea wengine.

Marejeo

  1. "Aya kuhusu kazi".

Viungo vya nje

  • [1] Tovuti rasmi ya International Labour Organization
  • [2] Ushauri kuhusu kazi toka Unesco
Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuKazi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Kazi&oldid=1100817"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp