Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Karafuu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Karafuu kadhaa
Karafuu ikiangaliwa kwa karibu
Maua kwenye mkarafuu
Karafuu tayari kukauka

Karafuu (kutokaKiarabu قَرَنْفُلqaranful[1]) nimatumba (macho yamaua) makavu yamikarafuu ambayo nimiti yafamilia yaMyrtaceae.

Karafuu hutumiwa kamakiungo chachakula na chanzo chamafuta yenyeharufu inayopendwa nawatu wengi.

Asili ya mti na pia matumizi ya matumba nivisiwa vyaIndonesia. Katikakarne ya 19 mikarafuu ilipelekwaUnguja naPemba hasa namtawala waOmani na kuanzishauzalishaji mkubwa saa wa karafuu kwenye visiwa hivi.

Matumizi

[hariri |hariri chanzo]

Karafuu hutumiwa katikaupishi wa nchi nyingi zaAsia,Afrika,Ulaya na hataAmerika. Hutumiwa katika kupikanyama, curry namichuzi mbalimbali pamoja na kupikamatunda pamoja navinywaji. Ni kiungo cha lazima kwenyepilau.

Hutafunwa piamdomoni kuboresha harufu yapumzi.

Kutafuna karafuu nidawa ya kupunguzamaumivu yameno.

Nchini Indonesiasigara huungwa na mafuta ya karafuu.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Karafuu zilifanyiwabiashara tangu kale. Kunaushuhuda wa karafuu katika chombo kilichopatikana nchiniSyria kilichogunduliwa kuachwa huko mnamo mwaka1721 KK[2].

Kunataarifa ya kwamba mtawala nchiniChina alitaka watu wanaotaka kuongea naye watafune karafuu ili wawe na pumzi ya kupendeza.[3]

Katikakarne ya 17 karafuu ilikuwa kati ya vivutio vyakiuchumi vilivyoletaUholanzi kuanzishamakoloni yake kwenye visiwa vya Indonesia.

Katikakarne ya 18MfaransaPierre Poivre alifaulu kuibamiche ya mikarafuu na kuipelekaMorisi ambakoWafaransa walianzishakilimo hicho.

Soko la karafuu lilikuaduniani na hii ilikuwachangamoto yaSultani wa Omani kupeleka miti hiyoUnguja na Pemba iliyoendelea kuwa nchi ya kuzalisha karafuu nyingi zaidi duniani na kuundautajiri wa Zanzibar ilhali kilimo hicho kilichochangia pia katikabiashara ya watumwa waliotumiwa kuzalishazao hili katika karne ya 19.[4]

Mapato ya karafuu yalimsababishaSaid bin Sultani kuhamishamakao makuu yake Unguja na baada yakifo chakeUsultani wa Zanzibar ulianzishwa kama nchi ya pekee na Omani.

Tanbihi

[hariri |hariri chanzo]
  1. Waarabu walipokea jina kutoka Kigiriki καρυὁφυλλονkaryofilon , tazamakamusi ya Sacleux, "Karafuu".
  2. Turner, Jack (2004). Spice: The History of a Temptation. Vintage Books. pp. xxvii–xxviii.ISBN 0-375-70705-0.
  3. Andaya, Leonard Y. (1993). "1: Cultural State Formation in Eastern Indonesia". Katika Reid, Anthony (mhr.).Southeast Asia in the early modern era: trade, power, and belief. Cornell University Press.ISBN 978-0-8014-8093-5.
  4. The world's oldest clove tree, BBC, 23 June 2012

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Karafuu&oldid=1233764"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp