Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Jumuiya ya Afrika Mashariki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutokaJumuiya ya Afrika ya Mashariki)
Kwa nchi iliyopendekezwa, tazamaShirikisho la Afrika Mashariki.
Jumuiya ya Afrika Mashariki
East African Community (en)
Communauté d'Afrique de l'Est(fr)
Kaulimbiu: "One People, One Destiny" (Watu Mmoja, Hatima Moja)
Wimbo wa taifa: "Wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki"
Eneo la Jumuiya ya Afrika MasharikiEneo la Jumuiya ya Afrika Mashariki
Mji mkuuArusha, Tanzania
Mji mkubwaKinshasa, Kongo JK
Lugha rasmiKiingereza,Kifaransa,Kiswahili
SerikaliJumuiya ya Kikanda
  Mwenyekiti wa Kikao cha Wakuu wa Nchi
William Ruto
  Mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri
Deng Dau Deng
  Rais wa Mahakama ya EAC
Nestor Kayobera
  Spika wa Bunge la Afrika Mashariki
Joseph Ntakarutimana
  Katibu Mkuu
Veronica Nduva
Historia
  Ilianzishwa
1967
  Ilisambaratika
1977
  Ilifufuliwa
7 Julai 2000
Eneo
  Jumlakm2 5,449,717 km²
  Maji (asilimia)3.83%
Idadi ya watu
  Kadirio la 2024 343,328,958
  Msongamano63/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
  Jumla Int$1.027 trilioni
  Kwa kila mtu Int$2,991
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
  Jumla $349.774 bilioni
  Kwa kila mtu $1,019
HDI (2022)0.515
chini
SarafuSarafu mbalimbali (Shilingi ya Kenya,Shilingi ya Tanzania,Shilingi ya Uganda,Faranga ya Rwanda,Faranga ya Burundi,Pauni ya Sudan Kusini,Faranga ya Kongo)
Majira ya saaUTC+3 EAT
Upande wa magariKushoto/Kulia (Inategemea Nchi)
Tovuti rasmi:
www.eac.int

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) nishirika lakisiasa kati ya nchi nane za kanda yaMaziwa Makuu ya Afrika:Burundi,Kenya,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,Rwanda,Somalia,Sudan Kusini,Tanzania, naUganda. Lengo kuu la EAC ni kukuza ushirikiano wa kikanda katika nyanja mbalimbali ikiwemobiashara, forodha, na ushirikiano wakisiasa. Jumuiya hii ilianzishwa awali mwaka 1967, lakini ilisambaratika mwaka 1977 kutokana na tofauti zakisiasa, kabla ya kufufuliwa rasmi mwaka 2000 kwa kutiwa saini kwa mkataba mpya. Kufikia mwaka 2024,William Ruto,Rais wa Kenya, ndiye mwenyekiti wa sasa wa EAC.

Tangu kufufuliwa kwake, Jumuiya ya Afrika Mashariki imeanzisha hatua mbalimbali muhimu za ujumuishaji, ikiwa ni pamoja na kuanzishwa kwa Umoja wa Forodha mwaka 2005, Soko la Pamoja mwaka 2010, na juhudi zinazoendelea kuelekea Muungano wa Fedha na hatimaye Shirikisho la Kisiasa. EAC pia imekuwa ikifanya kazi ya kuoanisha sera katika sekta kama usafiri, afya, elimu, na nishati. Ikiwa na jumla ya watu wanaozidi milioni 300 na msisitizo wa pamoja juu ya maendeleo ya kikanda, EAC ina nafasi inayoongezeka katika masuala ya bara na inachukuliwa kama mfano wa ushirikiano wa kikanda barani Afrika.[1][2][3][4]

Kwa sasa eneo la Mtangamano nikm2 4,810,363, likiwa na wakazi 312,362,653 (kadirio la mwaka2022), hivi kwamba ingekuwa nchi moja tu ingekuwa yanneduniani.

Demografia

Idadi ya Watu

Jumuiya ya Afrika Mashariki ina idadi ya watu takriban milioni 333.93 ambapo aslimia 31 wanaishi katikaJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ,Sudan Kusini ndiyo iliyo na watu wachache sana ikiwa na watu takriban milioni 11.48 .Asilimia ya wakazi wanaoishi mijini ni 20 tu, lakini wanaongekeza kwa 4.71% kila mwaka

Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kulingana na Idadi ya watu
  1. Kongo JK 105.83 (31.7%)
  2. Tanzania 66.62 (19.9%)
  3. Kenya 55.53 (16.6%)
  4. Uganda 48.86 (14.6%)
  5. Somalia 18.36 (5.49%)
  6. Rwanda 13.95 (4.17%)
  7. 13.69 (4.09%)
  8. Sudan Kusini 11.48 (3.43%)
[{"value":105.83,"color":"#36A","label":"Kongo JK $v"},{"value":66.62,"color":"#1A9","label":"Tanzania $v"},{"value":55.53,"color":"#6A5","label":"Kenya $v"},{"value":48.86,"color":"#CC5","label":"Uganda $v"},{"value":18.36,"color":"#928","label":"Somalia $v"},{"value":13.95,"color":"#E33","label":"Rwanda $v"},{"value":13.69,"color":"#E72"},{"value":11.48,"color":"#E79","label":"Sudan Kusini $v"}]
{"legend":true,"caption":"Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki kulingana na Idadi ya watu","size":200}
Idadi ya Watu katika Jumuiya ya Afrika Mashariki
PangilioNchiIdadi ya Watu (milioni)Asilimia
1Kongo, JK105.8331.69
2Tanzania66.6219.95
3Kenya55.3416.57
4Uganda48.6614.57
5Somalia18.365.50
6Rwanda13.954.18
7Burundi13.694.10
8Sudan Kusini11.483.44

Dini

Ukristo ndiyo dini kubwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa na wafuasi milioni 261.86 na asilimia 79% ya watu wa EAC,Kongo,JK ndio iliyo na wafuasi wengi takriban milioni 100 au asilimia 95.4 .Uislamu ina wafuasi takriban milioni 56.69 ambayo ni asilimia 16.98 ya watu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiongozwa naSomalia ambapo 99 ni waislamu.Dini za jadi ni asilimia 2.4% haswaaSudan Kusini ambapo asilimia 35 ni wafuasi wadini za jadi,Wasio na dini ni asilimia 1.75%

Mgawanyo wa Dini katika Jumuiya ya Afrika Mashariki
  1. Ukristo 261.86 (78.4%)
  2. Uislamu 56.69 (17.0%)
  3. Dini za Jadi 8 (2.40%)
  4. Wasio na Dini 5.83 (1.75%)
  5. Zingine 1.53 (0.46%)
[{"value":261.86,"color":"#36A","label":"Ukristo $v"},{"value":56.69,"color":"#1A9","label":"Uislamu $v"},{"value":8,"color":"#6A5","label":"Dini za Jadi $v"},{"value":5.83,"color":"#CC5","label":"Wasio na Dini $v"},{"value":1.53,"color":"#E33","label":"Zingine $v"}]
{"legend":true,"caption":"Mgawanyo wa Dini katika Jumuiya ya Afrika Mashariki","size":200}
Dini katika Jumuiya ya Afrika Mashariki
PangilioNchiUkristo (%)Uislamu (%)Dini za Jadi (%)Wasio na Dini (%)
1Burundi85.94.32.16.2
2Kenya85.510.90.71.5
3Kongo, JK95.41.52.62.5
4Rwanda93.82.23.0
5Somalia99.8
6Sudan Kusini60.56.232.9
7Tanzania63.134.11.21.5
8Uganda81.713.20.2

Lugha

Kiswahili,Kiingereza naKifaransa ndizo Lugha rasmi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.Kiswahili hutumika kama Lingua Franca katika nchi hizi hukuKiingereza naKifaransa zikitumika kama lugha za kufundishia shuleni. Lugha za Jumuiya ya Afrika mashariki zimegawanyika katika kundi tatu ambazo ni Lugha zaKibantu ambayo ndiyo kundi kubwa ya Lugha katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, Lugha za Kinilotiki na Lugha za Kikushi.

Mijini na Vijijini

Asilimia ya watu walioishi mijini katika Jumuiya ya Afrika Mashariki ni 35% na walioishi Vijijini asilimia 64%.Somalia naJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ndizo nchi zilizokuwa na asilimia kubwa ya wakazi wa mijini zikiwa na asilimia 46% na 45% mtawaliwa.Burundi naSudan Kusini ndizo nchi zilizokuwa na wakazi wa mjini wachache sana zikiwa na asilimia 13% na 17% ya wakazi wanaoishi mijini huku asilimia 86% na 82% mtawaliwa wakiishi vijijini.

RankNchiMijini (%)Vijijini (%)Wakazi (Mijini) (milioni)
Jumuiya ya Afrika Mashariki35.1364.87117.30
1Somalia46.7353.278.58
2Kongo, JK45.6454.3648.30
3Tanzania37.4162.5924.92
4Kenya28.4971.5115.77
5Uganda26.7773.2313.03
6Sudan Kusini20.8579.152.39
7Rwanda17.7282.282.47
8Burundi13.4086.601.83

Muhtasari

Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), yenye makao yake makuu Arusha, Tanzania,kazi yake kuu ni kuendeleza muungano wakiuchumi,kisiasa, nakijamii katika ukanda huu. Mwenyekiti wa sasa wa EAC niWilliam Ruto,Rais wa Kenya, anayeongoza Mkutano wa Wakuu wa Nchi, ambao ndio chombo cha juu zaidi cha maamuzi katika jumuiya hii.

Kwa miaka iliyopita, EAC imepiga hatua muhimu ikiwemo kuanzishwa kwa Umoja wa Forodha, Soko la Pamoja, na mikataba ya kuunda Umoja wa Fedha. Pia imeongeza uanachama wake, ikiwemo kuipokeaJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ,Somalia naSudan Kusini. Miradi mikubwa ya miundombinu ya kikanda, programu za kurahisisha biashara, na ushirikiano katika sekta za afya na usalama ni miongoni mwa mafanikio yanayoonyesha ushawishi unaokua wa jumuiya hii katika kuendesha mipango ya maendeleo yaAfrika Mashariki.

Historia

Jumuiya ya kwanza

Nchi tatu za Afrika ya Mashariki zilizokuwa chini yautawala waUingereza zilianzauhuru wao kwa kuendelezaushirikiano wa karibu uliorithiwa kutokana nautawala wa pamoja wakati waukoloni.

Baada ya kupatauhuru mwaka1961 nchi hizo ziliundaMamlaka ya Huduma za Pamoja za Afrika ya Mashariki (kwa Kiingereza East African Common Services Organisation – kifupi EACSO).

Ushirikiano ulihusufedha (East African Shilling),forodha (Customs Union), huduma zareli (East African Railway),ndege (East African Airways), mabandari,posta nasimu naelimu ya juu (Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki chenyekampasiMakerere,Dar es Salaam naNairobi).Mkataba ulilenga piamahakama kuu ya pamoja nasera ya kiuchumi yasoko la pamoja. Haya yote yalitakiwa kuwa chini yaBunge la Afrika Mashariki.

Tangu1965 umoja huo ulianza kurudi nyuma kila nchi ilipoanzishapesa yake.

Mwaka1967 nchi tatu zilijaribu upya kuimarisha umoja wao kwaMkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki wakiita umoja wao "Jumuiya ya Afrika ya Mashariki" ikiwa namakao makuuArusha, Tanzania.

Lakini mielekeo ya nchi zote tatu zilitofautiana mno: Kenya iliendelea kwa njia yaupebari lakini Tanzania ilijaribu kujengaUjamaa (usoshalisti) kuanzia mwaka 1967. Uganda uliingia katika kipindi chaudikteta kali yaIdi Amini aliyeharibuuhusiano na majirani alipoanza kudai sehemu za maeneo yao.

Sababu nyingine ni madai ya Kenya ya kuwa na viti zaidi kuliko Uganda na Tanzania katikakamati za maamuzi,[5] huku kukiwa na kutokuelewana kulikosababishwa na udikteta waIdi Amin nchini Uganda, Usoshalisti huko Tanzania, nasoko huria nchini Kenya,[2] hivyo wanachama hawa watatu wakapoteza ushirikiano wa miaka zaidi ya sitini namanufaa yaukubwa wa jumuiya hii kiuchumi. Kila mmoja wa wanachama hawa ilimbidi kuanza kutoahuduma na kujenga viwanda ambavyo hapo awali vilikuwa chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Hivyo mwaka1977 Jumuiya ya Afrika Mashariki ilikoma kufanya kazi yoyote na1983 ilifutwa rasmi.Mali iliyobaki iligawanywa kati ya nchi zote tatu.

Kufufuka kwa Jumuiya ya Afrika ya Mashariki tangu 1993

Tangumiaka ya 1990 majaribio ya kujenga umoja mpya yalionekana tena.

MaraisDaniel arap Moi wa Kenya,Ali Hassan Mwinyi wa Tanzania, naYoweri Kaguta Museveni wa Uganda walipatana katikaMkataba wa Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki hukoArusha, tarehe30 Novemba1993, na kuanzisha Tume ya Ushirikiano ya nchi hizi tatu. Shughuli ya kuzileta pamoja nchi hizi kisiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni,utafiti nateknolojia,ulinzi,usalama, masuala ya kisheria na kimahakama ilianza.

Mkataba wa kufufua jumuiya ulitiwa sahihi tarehe 30 Novemba 1999 ukaanza kuwa rasmi tarehe7 Julai 2000.

Vyombo vya Jumuiya mpya ya Afrika ya Mashariki vilianza kufanya kazi mnamo Januari2001 penye makao makuu ya jumuiya hii hukoArusha.

Mkataba2004 uliwekamsingi waUmoja wa Forodha ulioanzishwa2005.

Kuna tenaBunge la Afrika ya Mashariki linalojumuisha wabunge waliochaguliwa na mabunge ya nchi wanachama.

PiaMahakama Kuu ya Afrika ya Mashariki imeundwa upya.

Mwaka2008, baada ya majadiliano naJumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (Southern Africa Development Community, kifupi SADC) naSoko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (Common Market for Eastern and Southern Africa, kifupi COMESA), Mtangamano huo ulikubali nchi zote za miundo hiyo mitatu ziunde eneo pana labiashara huria. Kwa sasa Jumuiya ya Afrika Mashariki ni mojawapo ya nguzo muhimu za hiyoJumuiya ya Kiuchumi ya Afrika (African Economic Community, kifupi AEC).

Mwaka2010, Mtangamano ulitangazasoko la pamoja kwabidhaa,kazi na mitaji kati ya nchi hizo tano, kwa lengo la kuanzishapesa ya pamoja na hatimayeShirikisho kamili.[6]

Kuna majadiliano ya kuanzishashilingi mpya ya pamoja kwa nchi za Jumuia ya Afrika ya Mashariki. Kwanza ilitarajiwa kuanzishwa mwaka2012, halafu mwaka2015, sasa mwaka2024. Mwaka2013 ulisainiwamkataba wa kuamua kuanzisha hiyopesa ndani ya miaka 10.[7]

Uchumi

Pato la taifa

Jumuiya ya Afrika Mashariki inauchumiunaoendelea ikiwa naPato la taifa jumla dola bilioni 399 zaMarekani kwa Kawaida na trilion 1.197 kwaUsawa wa nguvu ya ununuzi (PPP) hata hivyo ni uchumiwa pili kwa ukubwa baraniAfrika baada yaAfrika Kusini.Kenya ndiyo iliyo na uchumi mkubwa zaidi katika jumuiya hii, ikichangia asilimia 37% ya jumla,Tanzania,Kongo, JK zilichangia asilimia 24% na 22% mtawaliwa.Sudan kusini naBurundi ndizo zilizokuwa na uchumi mdogo zaidi. Jumuiya ya Afrika Mashariki ni ya kipato cha chini ikiwa na pato la taifa kwa kila mtu dola 1,197 .Sudan Kusini ndiyo nchi maskini zaidi ikiwa na pato la taifa kwa kila mtu dola 252 zaMarekani,Kenya ndiyo nchi iliyo na pato la taifa kwa kila mtu dola kubwa zaidi ya dola 2,468 za Marekani.

Pato la taifa la Jumuiya ya Afrika Mashariki (2025)
OrodhaNchiPLT (Kawaida) 'bilioni USDPLT (PPP) 'bilioni USDKwa kila mtu (Kawaida)Kwa kila mtu (PPP)Asilimia ya EAC
EAC399.561,199.42$1,197$3,592100.0%
1Kenya131.67401.97$2,468$7,53536.55%
2Tanzania85.98293.59$1,318$4,50123.87%
3Kongo, JK79.12200.76$743$1,88421.96%
4Uganda64.28187.11$1,339$3,89717.85%
5Rwanda14.7758.12$1,043$4,1054.10%
6Somalia12.9932.5$766$1,9163.61%
7Burundi6.7513.98$493$1,0201.87%
8Sudan Kusini4.0011.39$252$7161.11%

Biashara ya Kimataifa

Mnamo 2023, jumla yabiashara ya kimataifa ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) ilifikia dola bilioni 130.4. Mchango mkubwa zaidi ulitokaJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (JKK), ambayo ilichangia asilimia 25.8 ya jumla hiyo, ikifuatiwa naKenya (24.7%) naTanzania (24.6%). Kwa upande mwingine, nchi zilizo na mchango mdogo zaidi zilikuwaSudan Kusini (1.8%) naBurundi (0.7%). Kwa Mahuruji (mauzo ya nje)Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo iliongoza zaidi ikichangia asilimia 40% ya mauzo ya nje ya Jumuiya hii, HukuKenya ikiongoza kwaMaduhuli ikichangia asilimia 30% ya Maduhuli ya Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kati ya nchi zote, Kongo,JK ilikuwa na mizani chanya ya biashara (balance of trade) ya dola bilioni 7.8, ikiwa ya juu zaidi katika kanda, hukuKenya (-16.24),Tanzania (-9.90), na Somalia (-4.22) zikiripoti nakisi kubwa zaidi yabiashara, ishara ya uagizaji mkubwa wa bidhaa kuliko mauzo ya nje.

RankNchiJumlaMahurujiMaduhuliMizani ya Biashara
1Congo, JK33.6020.7012.907.80
2Kenya32.167.9624.20-16.24
3Tanzania32.1011.1021.00-9.90
4Uganda19.698.3911.30-2.91
5Somalia6.110.955.16-4.22
6Rwanda3.551.352.20-0.85
7Sudan Kusini2.320.701.62-0.92
8Burundi0.870.200.68-0.48
EAC Jumla130.4051.3579.06-27.71

Nchi Wanachama

Kutokakushoto: RaisYoweri Museveni waUganda, RaisMwai Kibaki waKenya na RaisJakaya Kikwete waTanzania wakati wa mkutano waoArusha, mnamo Novemba2006.
Rais wa Rwanda Paul Kagame katika mkutano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki mwaka wa 2006. Rwanda ilijiunga na Jumuiya ya Afrika mashariki tarehe 1 Julai 2007
NchiMji mkuuKujiungaWakaziEneo (km2)GDP
(US$ bn)[8]
GDP
kwa mtu
(US$)[8]
GDP PPP
(US$ bn)[9]
GDP PPP
kwa mtu
(US$)[9]
Bendera ya Burundi BurundiGitega2007&0000000012722976.00000012,722,976&0000000000027834.00000027,8343.4&0000000000000272.400000272.410.8&0000000000000855.600000855.6
Bendera ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Jamhuri ya Kidemokrasia ya KongoKinshasa2022&0000000095944984.00000095,944,984&0000000002344858.0000002,344,85851.2&0000000000000669.400000669.4127.4&0000000000001315.9000001,315.9
Bendera ya Kenya KenyaNairobi2000&0000000056553921.00000056,553,921&0000000000580367.000000580,367114.7&0000000000002252.0000002,252308.7&0000000000006061.4000006,061.4
Bendera ya Rwanda RwandaKigali2007&0000000013705697.00000013,705,697&0000000000026338.00000026,33812.1&0000000000000910.00000091037.2&0000000000002807.6000002,807.6
Bendera ya Somalia SomaliaMogadishu2024&0000000016500000.00000016,500,000&0000000000637657.000000637,65712.49&0000000000000756.980000756.9834.02&0000000000002060.0000002,060
Bendera ya Sudan Kusini Sudan KusiniJuba2016&0000000011501583.00000011,501,583&0000000000644329.000000644,3295.7&0000000000000392.700000392.713.5&0000000000000927.400000927.4
Bendera ya Tanzania TanzaniaDodoma2000&0000000063732235.00000063,732,235&0000000000945087.000000945,08777.5&0000000000001260.1000001,260.1206.6&0000000000003358.3000003,358.3
Bendera ya Uganda UgandaKampala2000&0000000049135753.00000049,135,753&0000000000241550.000000241,55046.4&0000000000001060.4000001,060.4129.5&0000000000002960.5000002,960.5
&0000000303397152.000000303,397,152&0000000004810363.0000004,810,3633251106.38342,841.4

Kenya, Tanzania na Uganda zinahistoria yaushirikiano tangu mwanzoni mwakarne ya 20, wakati waukoloni, ikiwa ni pamoja na Umoja wa Forodha baina ya Kenya na Uganda mwaka 1917,Tanganyika ilijiunga mnamo mwaka1927, katikaUbalozi wa Afrika Mashariki (1948-1961), 'East African Common Services Organisation' (1961-1967) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (1967-1977).[10]

Jumuia ambayo ilianzishwa baada yauhuru ilidumu miaka 10 tu, lakini ilifufuliwa kwa mkataba wa tarehe30 Novemba1999, ulioanza kufanya kazi tarehe7 Julai2000, miaka 23 baada yakifo cha ile ya kwanza.

Burundi naRwanda, ambazo ziliwahi kuwakoloni moja naTanzania bara kabla yaVita vikuu vya kwanza, zilijiunga na Mtangamano tarehe6 Julai2009.[11]

Mara baada ya kupatauhuru mwaka2011, Sudan Kusini iliomba kujiunga na Jumuia, lakini haikukubalika hadi Machi 2016 kutokana na hali yavita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.

Tarehe23 Novemba2021 Baraza la Mawaziri la EAC limependekeza kwa Wakuu wa nchi wanachama wakubali ombi la kujiunga laJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo[12], nao wakakubali rasmi tarehe 29 Machi2022.

Hatua kubwa ya awali katika kuanzishaShirikisho la Afrika Mashariki nimuungano wa forodha katikamataifa husika uliotiwasaini mnamo Machi 2004 na ulioanza kutumika tarehe1 Januari mwaka2005. Chini ya masharti ya mkataba, Kenya, ambayo ndiyo nchi inayopata mauzo bora zaidi nje ya nchi katika kanda ya Afrika Mashariki, iliendelea kulipaushuru kwabidhaa zake zinazoingia nchi nyingine wanachama hadi mwaka2010, kwakiwango kilichopungua na wakati.Mfumo sawa waushuru utatumika kwa bidhaa kutoka nchi ambazo si wanachama.

Changamoto

Kwa ujumla, mataifa wanachama kwa kiasi kikubwa wanaona neema yaShirikisho la Afrika Mashariki, lakini utafiti usio rasmi unaonyesha kwamba Watanzania wengi (asilimia themanini ya wakazi wake) wanamtazamo hasi.[13]

Tanzania imekuwa na historia yaamani tangu kunyakua uhuru, ikilinganishwa nafujo navita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyoshuhudiwa katika mataifa yaKenya,Rwanda,Burundi, naUganda. Wakati huu Afrika Mashariki inajaribu kudumishautulivu namafanikio katikati ya migogoro inayoendelea katika nchi yaJamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo,Pembe ya Afrika naSudan Kusini.

Pia ni kwamba Tanzania inaardhi kubwa, na baadhi ya Watanzania wanahofu yaunyakuzi wa ardhi na wakazi wa sasa wa mataifa mengine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.[14][15][16]

Uhaba wa ardhi ni suala nyeti katika eneo la Afrika Mashariki, hasa nchini Kenya, ambako mapigano ya wenyewe kwa wenyewe upande waMlima Elgon mwaka2007 yaliwaacha zaidi ya watu 150 wamefariki na kulazimisha takriban watu wengine 60,000 kugura makazi yao.[17]

Serikali na Utawala

Mahakama ya Afrika Mashariki

Mahakama ya Afrika Mashariki ndiyomahakama inayosimamiakesi zote katika eneo hilo. Kwa sasa imo mjini Arusha, Tanzania.

Bunge la Afrika Mashariki

Bunge la Afrika Mashariki ndichokitengo cha kutengeneza sheria katika eneo la Afrika Mashariki. Ina wajumbe 27 ambao wote wamechaguliwa na mabunge ya nchi wanachama. Linahusika na masuala yote ambayo yanahusu Jumuiya hii kama vile kujadilibajeti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na masuala yote ya Jumuiya na kutoa mapendekezo kwa Baraza juu ya mambo wanayoyadhani muhimu kwa utekelezaji wa mkataba, kushirikiana pamoja na Bunge husika na kuanzishakamati kwa makusudi kama vile wanavyodhani ni muhimu. Tanguuzinduzi wake mwaka 2001,bodi hii imekuwa na vikao kadhaa mjini Arusha,Kampala na Nairobi.

Viungo

Pasipoti ya Afrika Mashariki

Pasipoti ya Afrika Mashariki ilizinduliwa rasmi tarehe1 Aprili1999 ili kurahisishausafiri na kuvuka mipaka ya nchi husika.[18][19] Nihalali kwa kusafiri ndani ya eneo la Afrika Mashariki (Kenya,Uganda na Tanzania) na kutoahaki ya kuingia na kukaa kwa miezi sita katika nchi yoyote na kisha unaweza ukaitumia tena.[18] Pasipoti hii inapatikana katika Makao Makuu yaIdara ya Uhamiaji katika miji ya Nairobi, Kampala na Dar es Salaam. Niraia tu wa Afrika Mashariki wanaoweza kuomba pasipoti hii.[18][19]Gharama ya pasipoti hii ni dola 10 zaMarekani au pesa sawa ukibadilisha kwa sarafu za nchi za Afrika mashariki.[19] Baada ya kujaza fomu za kupata pasipoti hii itachukua muda wawiki mbili au tatu kuipata tayari kwa matumizi. Ingawa pasipoti hii ni halali tu ndani ya Afrika Mashariki, majadiliano yalifanywa ili kuwa na hati sawa za kusafiri kwa watu wote wa Afrika Mashariki.[18]

Viza moja kwa watalii

African Union

Makala hii imepangwa kwa mfululizo:
Siasa na serikali ya
the African Union


Decentralised bodies

Nchi zingine ·Atlasi

Lilikuwatarajio la wengi kuwa kabla ya 2006 kungekuwa na viza moja kwa watalii wote wanaozuru Afrika Mashariki, iwapo mpango huo ungeidhinishwa na mamlaka yasekta husika chini ya jumuiya hiyo. Iwapo ingekubalika basi viza hiy ingetumika kote katika ardhi ya wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Chini ya pendekezo hili viza yoyote mpya ya Afrika Mashariki ingeweza kupokewa kutokaubalozi wowote katika eneo la Afrika Mashariki.

Mtandao

Matumizi yawavuti katika eneo la Afrika Mashariki bado yako chini mno yakilinganishwa na mataifa yaliyostawi kiuchumi.

Eneo la Afrika Mashariki ni kituo kizuri kiuchumi huku likikadiriwa kuwa na wakazi zaidi ya milioni 150. Inakadiriwa kuwa asilimia 10 ya wakazi wa Afrika Mashariki - milioni 15 - huutumiaMtandao.

Mkakati wa Jumuiya ya Afrika Mashariki unasisitiza ushirikiano wa kiuchumi namaendeleo kwa kuzingatiauwezo wa kijamii.

Wengi wa wakazi wa Afrika Mashariki hutumia mtandao kuangaliahabari, kusomabarua pepe na kwenyemitandao mingine ya kijamii.

Hivi karibuni kumekuwa na majukwaa mengi yanayoibuka katika eneo hili kwa lengo la kuileta pamoja Afrika Mashariki.

Kasi ya mawasiliano kupitia kwa mtandao pia iko chini mno katika eneo la Afrika Mashariki, ikilinganishwa na mataifa yaliyostawi. Hii labda ni mojawapo ya vikwazo vya maendeleo ya mawasiliano ya mtandao Afrika Mashariki.

Jiografia

Mtangamano ungekuwa nchi moja tu, ungekuwa ya 7duniani kwa eneo (kilometa mraba 4,812,618).

Lake Victoria
Ziwa Victoria kati ya nchi za Mtangamano.
Mount Kilimanjaro
Mlima Kilimanjaro, mrefu kuliko yote ya Afrika, uko Tanzania.

Sudan Kusini, Uganda, Rwanda na Burundi hazinapwanibaharini, lakini zinamvua za kutosha.

Huku inapatikana minne kati ya milima mirefu zaidibaraniAfrika:Mlima Kilimanjaro (Tanzania),Mlima Kenya (Kenya), milima yaRwenzori (Uganda/DRC) naMlima Meru (Tanzania).

Ziwa Turkana, Kenya, ndiyo ziwa lajangwani kubwa na lenyemaji ya chumvi nyingi kuliko yote duniani.

Ziwa Victoria linaunganisha nchi za Kenya, Uganda na Tanzania na ni la pili duniani kwa eneo.

Ziwa Tanganyika kati ya Tanzania, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni la pili duniani kwa kina.

Kenya pekee inajangwa,jangwa la Chalbi katikaKaunti ya Marsabit.

Wildebeest#Migration
Uhamaji wawanyamapori niajabu la kimaumbile la 7 duniani
Mount Kilimanjaro
Ziwa Nakuru, maarufu kwa flamingo.
Dar es Salaam, ukiwa na watu milioni 4 ndiomji mkubwa kuliko yote ya Mtangamano baada tu yaKinshasa.
Nairobi,kitovu chabiashara cha Mtangamano

Ugatuzi katika nchi za Jumuia ya Afrika Mashariki (E.A.C.)

Burundi

  1. Bubanza
  2. Bujumbura Mjini
  3. Bujumbura Vijijini
  4. Bururi
  5. Cankuzo
  6. Cibitoke
  7. Gitega
  8. Karuzi
  9. Kayanza
  10. Kirundo
  11. Makamba
  12. Muramvya
  13. Muyinga
  14. Mwaro
  15. Ngozi
  16. Rutana
  17. Ruyigi

Kenya

  1. Mombasa
  2. Kwale
  3. Kilifi
  4. Tana River
  5. Lamu
  6. Taita–Taveta
  7. Garissa
  8. Wajir
  9. Mandera
  10. Marsabit
  11. Isiolo
  12. Meru
  13. Tharaka-Nithi
  14. Embu
  15. Kitui
  16. Machakos
  17. Makueni
  18. Nyandarua
  19. Nyeri
  20. Kirinyaga
  21. Murang'a
  22. Kiambu
  23. Turkana
  24. West Pokot
  25. Samburu
  26. Trans-Nzoia
  27. Uasin Gishu
  28. Elgeyo-Marakwet
  29. Nandi
  30. Baringo
  31. Laikipia
  32. Nakuru
  33. Narok
  34. Kajiado
  35. Kericho
  36. Bomet
  37. Kakamega
  38. Vihiga
  39. Bungoma
  40. Busia
  41. Siaya
  42. Kisumu
  43. Homa Bay
  44. Migori
  45. Kisii
  46. Nyamira
  47. Nairobi

Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia

  1. Mkoa wa Équateur
  2. Mkoa wa Ituri
  3. Mkoa wa Kasai
  4. Mkoa wa Kasai Kati
  5. Mkoa wa Kasai Mashariki
  6. Mkoa wa Katanga Juu
  7. Mkoa wa Kinshasa
  8. Mkoa wa Kivu Kaskazini
  9. Mkoa wa Kivu Kusini
  10. Mkoa wa Kongo Kati
  11. Mkoa wa Kwango
  12. Mkoa wa Kwilu
  13. Mkoa wa Lomami
  14. Mkoa wa Lomami Juu
  15. Mkoa wa Lualaba
  16. Mkoa wa Mai-Ndombe
  17. Mkoa wa Maniema
  18. Mkoa wa Mongala
  19. Mkoa wa Sankuru
  20. Mkoa wa Tanganyika
  21. Mkoa wa Tshopo
  22. Mkoa wa Tshuapa
  23. Mkoa wa Ubangi Kaskazini
  24. Mkoa wa Ubangi Kusini
  25. Mkoa wa Uele Chini
  26. Mkoa wa Uele Juu

Rwanda

  1. Kigali
  2. Kaskazini
  3. Kusini
  4. Magharibi
  5. Mashariki

Somalia

  1. Awdal
  2. Bari
  3. Nugal
  4. Mudug
  5. Galguduud
  6. Hiran
  7. Shebeli wa Kati
  8. Banaadir
  9. Shebeli wa Chini
  10. Togdheer
  11. Bakool
  12. Woqooyi Galbeed
  13. Bay
  14. Gedo
  15. Juba wa Kati
  16. Juba wa Chini
  17. Sanaag
  18. Sool

Sudan Kusini

  1. Bahr el Ghazal Kaskazini
  2. Bahr el Ghazal Magharibi
  3. Lakes
  4. Warrap
  5. Western Equatoria
  6. Central Equatoria
  7. Eastern Equatoria
  8. Jonglei
  9. Greater Upper Nile
  10. Unity
  11. Upper Nile
  12. Eneo la Abyei
  13. Eneo la Pibor
  14. Eneo la Ruweng

Tanzania

  1. Arusha
  2. Dar es Salaam
  3. Dodoma
  4. Geita
  5. Iringa
  6. Kagera
  7. Katavi
  8. Kigoma
  9. Kilimanjaro
  10. Lindi
  11. Manyara
  12. Mara
  13. Mbeya
  14. Morogoro
  15. Mtwara
  16. Mwanza
  17. Njiombe
  18. Pemba Kaskazini
  19. Pemba Kusini
  20. Pwani
  21. Rukwa
  22. Ruvuma
  23. Shinyanga
  24. Simiyu
  25. Singida
  26. Songwe
  27. Tabora
  28. Tanga
  29. Unguja Kaskazini
  30. Unguja Mjini Magharibi
  31. Unguja Kusini

Uganda

  1. Mkoa wa Kaskazini
  2. Mkoa wa Kati
  3. Mkoa wa Magharibi
  4. Mkoa wa Mashariki

Tazama pia

Tanbihi

  1. "– Born in anonymity". Ms.dk. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2012-04-15. Iliwekwa mnamo2010-07-01.
  2. 12East African trade zone off to creaky start,Christian Science Monitor, 9 Machi 2006
  3. We Celebrated at EAC Collapse, Says Njonjo.
  4. "East African Community – Quick Facts". Eac.int. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2009-03-19. Iliwekwa mnamo2010-07-01.
  5. "ms.dk - Born in anonymity". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2012-04-15. Iliwekwa mnamo2009-12-03.
  6. "FACTBOX-East African common market begins".Reuters. 1 Julai 2010. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2012-01-18. Iliwekwa mnamo1 Julai 2010.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  7. "East African trade bloc approves monetary union deal".Reuters. 30 Novemba 2013. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2015-09-24. Iliwekwa mnamo2015-01-23.{{cite news}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  8. 12"Report for Selected Countries and Subjects".www.imf.org.
  9. 12"Report for Selected Countries and Subjects".www.imf.org.
  10. From Co-operation to Community (eac.int)
  11. "EAC Update E-newsletter".www.eac.int. Directorate of Corporate Communications and Public Affairs. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2012-04-26. Iliwekwa mnamo10 Desemba 2011.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  12. https://www.eac.int/press-releases/2288-eac-council-of-ministers-green-light-report-on-drc-verification-mission-for-consideration-by-eac-heads-of-state
  13. allAfrica.com: Tanzania: Fast-Tracking Political Federation
  14. EAC federation fears justified?Ilihifadhiwa 27 Septemba 2007 kwenyeWayback Machine. Tanzania's Daily News On Saturday; 5 Mei 2007
  15. Kenya: Tears for Mt Elgon as Schools Re-Open
  16. Sabiny Demand Land as Karamajong Raid Reduce
  17. AlertNetIlihifadhiwa 20 Juni 2010 kwenyeWayback Machine. Kenya land clashes kill 60, displace thousands
  18. 1234"EAC News ..." Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2004-12-21. Iliwekwa mnamo2004-12-21.
  19. 123"Travelling in East Africa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutokachanzo mnamo 2004-07-01. Iliwekwa mnamo2004-07-01.

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nadharia
Watetezi
Location of Africa
Location of Africa

Wanasiasa:Nnamdi Azikiwe ·Kamuzu Banda ·Amílcar Cabral ·David Comissiong ·Muammar Gaddafi ·Marcus Garvey ·Kenneth Kaunda ·Jomo Kenyatta ·Patrice Lumumba ·Nelson Mandela ·Thabo Mbeki ·Abdias do Nascimento ·Gamal Abdel Nasser ·Kwame Nkrumah ·Julius Nyerere ·John Nyathi Pokela ·Thomas Sankara ·Leopold Sedar Senghor ·Haile Selassie ·Robert Mangaliso Sobukwe ·Ahmed Sékou Touré ·I.T.A. Wallace-Johnson
Wengine:Marimba Ani ·Molefi Kete Asante ·Steve Biko ·Edward Wilmot Blyden ·Stokely Carmichael ·John Henrik Clarke ·Cheikh Anta Diop ·W. E. B. Du Bois ·Frantz Fanon ·John G. Jackson ·Leonard Jeffries ·Yosef Ben-Jochannan ·Maulana Karenga ·Fela Kuti ·Malcolm X ·Bob Marley ·Zephania Mothopeng ·George Padmore ·Motsoko Pheko ·Runoko Rashidi ·Paul Robeson ·Walter Rodney ·Burning Spear ·Henry Sylvester-Williams ·Omali Yeshitela

Mashirika
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Jumuiya_ya_Afrika_Mashariki&oldid=1454415"
Jamii:
Jamii zilizofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp