Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Jibini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Soko la jibini mjini Gouda (Uholanzi)
Kiwanda cha jibini ya Parmigiano (Italia)
Aina za jibini hukoBasel (Uswisi)

Jibini nichakula kinachotokana namaziwa.

Maziwa yang'ombe,kondoo aumbuzi hugandishwa. Hupikwa katikasufuria nadawa asilia kutokatumbo landama ya ng'ombe (kimeng'enya charenini) humwagwa humo pamoja nachumvi. Maziwa yanaganda mara moja na kumwagwa katikakitambaa ili majimaji yatoke na hatimaye sehemu imara pekee ibaki.

Jibini mbichi inaweza kukandamizwa na kuwa imara zaidi. Baadaye, ilhali ni bado laini, huwekwa katikabakuli na kupokeaumbo lake wakati inaendelea kukauka.

Baadaye inakaa na kuiva. Aina mbalimbali za jibini huiva kwamuda tofautitofauti.

Katika nchi zajoto ni vigumu zaidi kutengeneza jibini bilamashine nafriji, lakini katika nchi nyingi jibini ni sehemu yautamaduni. Jibini nichakula bora chenyeprotini namafuta sawa na maziwa.Kiuchumi ni muhimu kama njia ya kutunza maziwa kwa miezi mingi.

Nchi kamaUholanzi,Ufaransa,Uswisi naItalia ni maarufu kwa aina nyingi za jibini, kila moja ikiwa naladha narangi tofauti.

Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuJibini kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Jibini&oldid=1024719"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp