Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Jamaika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Commonwealth of Jamaica
Bendera ya JamaikaNembo ya Jamaika
BenderaNembo
Kaulimbiu ya taifa: Out of many, one people(kutoka wengi - taifa moja)
Wimbo wa taifa:Jamaica, Land We Love
Wimbo wa kifalme:God Save the King
Lokeshen ya Jamaika
Mji mkuuKingston
17°59′ N 76°48′ W
Mji mkubwa nchiniKingston
Lugha rasmiKiingereza
SerikaliUfalme wa kikatiba
Charles III
Sir Patrick Allen
Andrew Holness
Uhuru
kutokaUingereza
6 Agosti1962
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
10,991 km² (ya 166)
1.5
Idadi ya watu
 -Julai 2012 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
2,889,187 (ya 139)
252/km² (ya 49)
FedhaDollar ya Jamaika (JMD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC-5)
(UTC)
Intaneti TLD.jm
Kodi ya simu+1-876]]

-



Jamaika ninchi ya kisiwani katikaBahari ya Karibi. Ikokm 150kusini mwaKuba na 150 upande wamagharibi waHaiti na ni kisiwa kikubwa cha tatu kati yaAntili Kubwa. Katikalugha yaKiingereza visiwa hivyo huitwa "West Indies" (visiwa vyaUhindi wa Magharibi).

Jina limetokana naneno laKiarawak "Xaymaca" au "Chaymaka" linalomaanisha "nchi yachemchemi" (yaani kisiwa chenye maji matamu).

Mji mkuu niKingston.

Ramani ya Jamaika

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Kisiwa kinaurefu wa km 240 naupana hadi km 85. Eneo lake nikm² 10.991.

Visiwa vidogo vya Pedro Cays vyenye eneo laha 23 jumla ni sehemu ya nchi ya Jamaika.

Mashariki mwa kisiwa kunasafu ya milima yabuluu yenye urefu wa km 100 penyekilele chaBlue Mountain Peak (m 2256 juu yaUB).

Katikati kunanyanda za juu zilizojengwa kwa mawe yachokaa yenye mabonde marefu.

Upande wa kusini nyanda za juu zinamtelemko mkali hadimwambao wabahari.

Iko mito mingi mifupi;mto mrefu niBlack River yenye km 53.4. Mto waHector's River una mwendo wa km 6 chini yaardhi.

Mtelemko mkali kwenye pwani ya Jamaika

Hali ya hewa

[hariri |hariri chanzo]

Hali ya hewa ni ya kitropiki. Hakuna tofauti kubwa yahalijoto mwaka wote. Halijoto ya wastani katika Kingston ni 25°C wakati waJanuari na 27 °C wakati waJulai.

Usimbishaji hutofautiana katika kanda mbalimbali ya kisiwa. Milima ya kaskazini-mashariki hupokea zaidi yamm. 5.000 lakini Kingston ina mm 813 pekee.Mvua inanyesha hasaMei,Juni,Oktoba naNovemba. Miezi yaSeptemba na Oktoba inaonadhoruba kali zatufani mara kwa mara.

Miji

[hariri |hariri chanzo]

Miji muhimu ikomwambaoni kwa sababu ya milima ya ndani.


Historia

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi wa kwanza wa Jamaika walikuwaWataino ambao nikabila mojawapo laWaarawak kutokaAmerika Kusini. Walikuwawakulima nawavuvi. Wamepotea kamautamaduni wa pekee baada ya kufika kwa Wazungu kutokana na magonjwa mageni yaliyofika na Wahispania na mauaji wakati wa vita. Waliobaki waliingia katikandoa na Wazungu au Waafrika waliofika baadaye na kuwa sehemu ya wakazi chotara kisiwani.

Kristoforo Kolumbus alifika mwaka1494 na kuweka kisiwa chini yautawala wa Hispania. Aliamini ya kwamba alifikaUhindi akaita visiwa hivi "Uhindi wa Magharibi" na wenyeji wakaitwa "Indios" (kwaKihispania "Wahindi") na baadaye mara nyingi "Wahindi wekundu".

Mwaka1655 Waingereza waliteka kisiwa wakaanzishauchumi wa mashamba makubwa yamiwa. Jamaika imekuwa mahali pakuu pa kutengenezasukari duniani kote. Watumwa wengi Waafrika walipelekwa kisiwani kamawafanyakazi kwenye mashamba hayo. Ndio mababu wa 90% wa wakazi wa leo wa Jamaika.

Kati ya miaka1834 na1838utumwa ulifutwa.

Mwaka1958 Jamaika ilianza kuelekeauhuru kamajimbo la "Shirikisho la Uhindi wa Magharibi".

Uhuru kamili ulipatikana mwaka1962.

Wakazi

[hariri |hariri chanzo]

Mwaka 2012 Jamaika ilikuwa na wakazi 2,889,187.Nusu yao waliishi mjini.Umri wa wastani ni miaka 23,thuluthi moja niwatoto hadi miaka 14.

Takriban 91.4% ya wakazi ni wa asili yaAfrika. Mababu walikuwawatumwa kutokaAfrika waliofikishwa kisiwani katikakarne ya 17 nakarne ya 18 au ni machotara au wa asili yaUlaya naUchina.

Wakazi asilia walikuwaWaarawak naWataino ambao hawako tena kama vikundi vya pekee; wengi walikufa kutokana namagonjwa yaWazungu auvita vya miaka ya kwanza baada ya kufika kwaWahispania. Wengine walichanganyikana na vikundi vingine.

Mbali ya wakazi, Wajamaika au wenye asili ya kisiwa kama 2,500,000 wanaishi nje ya nchi.

Lugha

[hariri |hariri chanzo]

Pamoja nalugha rasmi ambayo ni Kiingereza kuna pia aina yaKrioli yenye asili yaKiingereza: ndiyo inayotumika kawaida.

Dini

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi walio wengi hufataUkristo hasa katikamadhehebu yaUprotestanti kama vile:

Wakatoliki ni 2%, na vilevileMashahidi wa Yehova.

Dini iliyoanzishwa Jamaika niRastafari ambayo mwaka2001 ilikuwa na wafuasi 24.000.

Utamaduni

[hariri |hariri chanzo]

Muziki ni sehemu muhimu sana katika utamaduni wa Jamaika. Hasa muziki yaReggae umejulikana kote duniani.Mwanamuziki mashuhuri hasa wa Jamaika alikuwaBob Marley na kikundi chake cha "The Wailers".

Pia Wajamaika wana mafanikio makubwa katikariadha, hasa ya masafa mafupi.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi huru
Kamili
Sehemu
Maeneo chini ya nchi nyingine
Udani
Ufaransa
Uholanzi
Ufalme wa Muungano
Marekani
Makala hii kuhusu maeneo yaBahari ya Karibi bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuJamaika kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Jamaika&oldid=1328648"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp