Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Ijumaa Kuu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutokaIjumaa kuu)
Msalaba wa Ijumaa Kuu kwenyeMonasteri yaUtatu Mtakatifu,Meteora,Ugiriki.
Mwaka wa liturujia
Magharibi
Mashariki
Picha takatifu yakarne ya 16 ikionyesha tendo la kumsulubuYesu kadiri yaTheophanes wa Krete (Stavronikita Monastery,Mlima Athos,Ugiriki).
Siku ya Ijumaa KuuWakatoliki wanapokeaekaristi ingawaMisa haiadhimishwi (Our Lady of Lourdes,Philadelphia,Marekani).
Njia ya Msalaba ikiadhimishwa kwenyeColosseum mjiniRoma siku ya Ijumaa Kuu. Mwishoni,Papa anatoa neno.
Picha yaEl Greco ikimuonyeshaYesu akibeba msalaba,1580.
Epitafyo yaKiorthodoksi ikionyeshamwili wa Yesu ukizikwa.
Epitafyo ikichukuliwa katikamaandamano.

Ijumaa Kuu nisiku yaIjumaa kabla yaPasaka ambapoWakristo wengiduniani wanaadhimishakifo chaYesu Kristomsalabani.

Kufuatana na taarifa zaInjilinne katikaBiblia ya Kikristo,Yesualisulubiwa siku kabla yaSabato (auJumamosi), yaani Ijumaa. Mahali pa kumsulubisha palikuwakilima chaGolgotha kilichokuwepo wakati ule nje yakuta zamji waYerusalemu.

Tarehe

[hariri |hariri chanzo]

Kadiri yaInjili yaMtume Yohane, kesho yake ilikuwaSabato na piaPasaka, jambo lisilotokea kila mwaka. Kwa sababu hiyowataalamu mbalimbali wameweza kukadiria ilikuwatarehe7 Aprili30.

Sikukuu hii haina tarehe thabiti katikakalenda ya kawaida. Ilhali hutangulia Pasaka inafuata pia mabadiliko ya tarehe za Pasaka. Pamoja namapokeo yaliyo tofauti kati yaUkristo wa Magharibi (Wakatoliki naWaprotestanti wengi) naUkristo wa Mashariki (makanisa ya Kiorthodoksi naWakatoliki wa Mashariki), kuna tarehembili tofauti za Pasaka, na hivyo pia kila mwaka kuna tarehe mbili tofauti za Ijumaa Kuu.

MwakaUkristo wa
Magharibi
Ukristo wa
Mashariki
201830 Machi06 Aprili
201919 Aprili26 Aprili
202010 Aprili17 Aprili
202102 Aprili30 Aprili
202215 Aprili22 Aprili

Katika liturujia ya makanisa

[hariri |hariri chanzo]

Ijumaa kuu ni sehemu yaJuma Kuu linaloanza kwa adhimisho laYesu kuingia mji huo akishangiliwa kamamfalme wa Wayahudi (yaaniMasiya auKristo). Adhimisho hilo linafanyika mwanzoni mwawiki, yaaniJumapili ya matawi.

Ijumaa kuu ni pia sehemu yasiku tatu kuu za Pasaka zinazoadhimisha mateso nakifo chake (Ijumaa), kulalakaburini (Jumamosi), na hatimayekufufuka kwautukufu (Jumapili), kwa ufupi:

  1. Yesu mteswa,
  2. mzikwa na
  3. mfufuka.

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuIjumaa Kuu kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Ijumaa_Kuu&oldid=1203259"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp