Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Hungaria

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Magyarország
Hungaria
Bendera ya HungariaNembo ya Hungaria
BenderaNembo
Kaulimbiu ya taifa: --
Wimbo wa taifa:Himnusz("Isten, áldd meg a magyart")
"Wimbo" ("Mungu wabariki Wahungaria wote")
Lokeshen ya Hungaria
Mji mkuuBudapest
47°26 N 19°15 E
Mji mkubwa nchiniBudapest
Lugha rasmiKihungaria (Magyar)
SerikaliSerikali ya kibunge Jamhuri
Tamás Sulyok
Viktor Orbán
Uhuru
Principality of Hungary
Ufalme wa Hungaria
Kuachana kwa
Milki ya Austria-Hungaria
Jamhuri ya Hungaria

896
Desemba1000

1918
1989
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
93,030 km² (ya 109)
0.74%
Idadi ya watu
 -2024 kadirio
 -2023 sensa
 - Msongamano wa watu
 
9,580,000 (ya 95)
9,599,744
103/km² (ya 78)
FedhaForint ya Hungaria (HUF)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
CET (UTC+1)
CEST (UTC+2)
Intaneti TLD.hu1
Kodi ya simu+36
1 pia.eu kama nchi yaUmoja wa Ulaya


Hungaria (kwaKihungariaMagyarország), rasmi kamaJamhuri ya Hungaria, ni nchi isiyo na pwani katikaUlaya ya Kati, inayopakana naSlovakia kaskazini,Ukraini kaskazini-mashariki,Romania mashariki,Serbia naKroatia kusini,Slovenia kusini-magharibi, naAustria magharibi. Ina idadi ya watu takriban milioni 9.6, ikiwa ya 94 duniani. Jiji lake kubwa zaidi na mji mkuu niBudapest. Hungaria imegawanyika katika mikoa 19 na jiji la Budapest.

Kihungaria ndiyolugha rasmi na ya kawaida kwa wananchi.

Wakazi walio wengi (52.9%) niWakristo. hasaWakatoliki (37.4%) naWakalvini (11.1%).

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Historia ya awali

[hariri |hariri chanzo]

Hungaria ilitokea kama nchi ya pekee wakati wakarne ya 10BK.

Tangu zamani zakuzaliwa kwake Kristo (milenia ya kwanza) sehemu kubwa ya Hungaria ilijulikana kamaPanonia ikawa sehemu yaDola la Roma.

Tangu kuporomoka kwa nguvu ya Waroma ilivamiwa na makabila mbalimbali kama vileWagermanik,Wahunni naWaslavi.

Baada ya mwaka900 Wahungaria chini yamtemiArpad walivamia eneo hili. Wakati ule Wahungaria walikuwa mkusanyiko wa makabila wahamiaji waliojiita "Majari" (Magyar) waliotoka katika maeneo kati yamto Volga namilima ya Ural.

Kutoka makazi yao mapya katika Panonia waliendelea kuvamia maeneo mengine ya Ulaya hadimilima ya Pirenei.

Baada ya kupokea Ukristo

[hariri |hariri chanzo]

Baada ya kushindwa naWajerumani mwaka955 walibaki katika makazi yao na mnamo mwaka1000 mfalme Ishtvan (Stefano wa Hungaria) alipokeaubatizo akaongoza taifa lake kuingia katikaUkristo.

Wakati wauvamizi waWamongolia baada yaChingis Khan katikakarne ya 13 nchi iliangamizwa, na nusu ya wakazi wakauawa.

Baadaye wafalme Wahungaria waliwakaribishawalowezi kutokaUjerumani walioanzisha vijiji vingi na pia miji.

Wakati wakarne ya 15WaturukiWaosmani walianza kuenea kwenye Balkani, wakaingia katika Hungaria kutoka upande wa mashariki. Katikamapigano ya Mohacs mwaka1526 Hungaria ilishindwa na sehemu kubwa ikawa chini ya Waosmani. Magharibi ya nchi ikaendelea kuitwaufalme wa Hungaria lakini ufalme uliingia mikononi mwa nyumba yaHabsburg yaani chini ya watawala waAustria.

Katika karne zilizofuata watawala wa Habsburg walirudisha Waosmani nyuma na ufalme wa Hungaria ukawa sehemu ya milki ya Habsburg yaani Austria.

Katikakarne ya 19 mnamo1848 Wahungaria waliasi dhidi ya watawala lakini walishindwa. Hata hivyoKaisariFranz Joseph I alibadilishasiasa yake akatafuta usaidizi wa Wahungaria katika utawala wa ufalme. Katiba mpya iliunda cheo cha sawa kati ya Austria na Hungaria chini ya mtawala yeye yule mwenye vyeo vya Kaisari wa Austria na Mfalme wa Hungaria na milki ikaitwa "Austria-Hungaria".

Austria-Hungaria ilikuwa milki kubwa katika Ulaya ya Kati na Mashariki kuanzia mwaka1867 hadi1918.

Kuanzia karne ya 20

[hariri |hariri chanzo]

Baada yavita kuu ya kwanza ya dunia milki ikaporomoka na Hungaria ikaendelea kama nchi ya pekee yenye katiba ya ufalme lakini bila mfalme.

Katikavita kuu ya pili ya dunia Hungaria ikaingia upande waUjerumani ukaendelea kuwatesaWayahudi wake wa kushikamana na siasa yaHitler na mwishowe ikashindwa pamoja na Ujerumani. Hungaria ikavamiwa najeshi laUmoja wa Kisovyeti na mabwana hao wapya walihakikisha ya kwambachama cha kikomunisti ilishikaserikali. Hivyo Hungaria ikawa sehemu yaMapatano ya Warshawa ikasimama upande wa mashariki katika kipindi chavita baridi.

Mwaka1956 wananchi wengi walipindua serikali ya kikomunisti na serikali mpya chini yaImre Nagy ilianzishademokrasia yavyama vingi. Lakini wanajeshi wa Kisovyeti wakaingia kati wakarudisha utawala wa chama cha kikomunisti ulioendelea hadi kuporomoka kwaukomunisti mnamo1989.

Hungaria imekuwa nchi mwanachama waUmoja wa Ulaya tangu2004.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi zaUmoja wa UlayaBendera ya Umoja wa Ulaya
Austria |Bulgaria |Eire |Estonia |Hispania |Hungaria |Italia |Kroatia |Kupro |Latvia |Lituanya |Luxemburg |Malta |Polandi |Slovakia |Slovenia |Romania |Ubelgiji |Ucheki |Udeni |Ufaransa |Ufini |Ugiriki |Uholanzi |Ujerumani |Ureno |Uswidi
Nchi huru
Nchi zisizokubaliwa
na umma wa kimataifa
Maeneo yanayojitawala
chini ya nchi nyingine
1 nchi yaAsia ya Magharibi kijiografia ambayo huhesabiwa kuwa sehemu yaUlaya kiutamaduni2nchi ya kimabara
Makala hii kuhusu maeneo yaUlaya bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuHungaria kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Hungaria&oldid=1406461"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2026 Movatter.jp