Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Hong Kong

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mkoa Maalum wa Utawala wa Hong Kong
香港特別行政區 (Xianggang Tebie Xingzhengqu)
Wimbo wa taifa:"March of the Volunteers"

Wimbo wa Kujitolea (Wimbo wa Taifa la China)
Mahali pa Hong KongMahali pa Hong Kong
Miji mikuuHakuna rasmi (Makao makuu ya serikali yako Tamar, Admiralty)
Mji mkubwaHong Kong
Lugha rasmiKichina (Kikantoni) naKiingereza
  Mkuu wa Mtendaji
John Lee
Uhuru kutoka Uingereza
  Makoloni ya Uingereza
26 Januari 1841
  Kukabidhiwa kwa China
1 Julai 1997
Eneo
  Jumlakm2 1,110.18(ya 167)
  Maji (asilimia)59.70%
Idadi ya watu
  Kadirio la 20247,492,000
  Msongamano6,801/km²/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2024
  Jumla $569.83 Bilioni[1]
  Kwa kila mtu $75,410[1]
PLT (Kawaida)Kadirio la 2024
  Jumla $401.75 Bilioni[1](ya 46)
  Kwa kila mtu $53,160[1]
HDI (2021) 0.952 (ya 4)
juu sana
Gini (2016)Ongezeko hasi 53.9
SarafuDola ya Hong Kong
Majira ya saaUTC+8 (HKT)
Upande wa magariKushoto
Msimbo wa simu+852
Jina la kikoa.hk
Hong Kong

Hong Kong (Kichina: 香港; pinyin: Xiānggǎng) niMkoa Maalum wa Utawala (SAR) wa China. Upo kusini mwa pwani ya nchi, kando yaBahari ya Kusini ya China. Inajumuisha Kisiwa cha Hong Kong, Rasi ya Kowloon, na New Territories. Jiji la Hong Kong, lililopo kwenye Kisiwa cha Hong Kong, ndilo jiji kubwa na idadi ya watu katika mkoa.Hong Kong lina takriban milioni 7.5 katika eneo la kilomita za mraba 1,110

Hong Kong ilikuwakoloni laUingereza katika pwani ya China kwa zaidi ya miaka 99. Hong Kong ilirudishwa kwaChina kutoka Uingereza mnamo Julai 1, 1997, chini ya makubaliano ya "nchi moja, mifumo miwili," ikiruhusu Hong Kong kudumisha uhuru wake wa kisiasa na kiuchumi kwa miaka 50. Hata hivyo, kwa muda, China imeongeza udhibiti wake, hasa kupitia maandamano ya kupinga muswada wa kukabidhi wahalifu wa 2019 na Sheria ya Usalama ya Kitaifa ya 2020, ambayo ilipunguza uhuru na haki za Hong Kong.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Baada ya China kushindwa naDola la Uingereza katikaVita vya kwanza vya Afyuni (1839-1842), Hong Kong ikawa koloni la Uingereza kuanzia Kisiwa cha Hong Kong, ikifuatiwa na Musoma ya Kowloon mwaka1860 namkataba wa miaka 99 kwa Majimbo Mapya katika1898.

Baada ya kumilikiwa naJapan wakati waVita Kuu ya Pili (1941-1945), Waingereza waliiteka tena hadi Juni 30, 1997.

Kuelekea mwishoni mwamiaka ya 1970, Hong Kong ikawa imara kama mlango mkuu kati yadunia nzima na China.

Kama matokeo yamazungumzo kati ya China na Uingereza, Hong Kong ilirudishwa kwa Jamhuri ya Watu wa China chini ya Azimio la Pamoja la mwaka1984. Mji ukawa wa kwanza kati ya Mikoa yenye utawala maalumu nchini China tarehe1 Julai 1997 chini ya kanuni ya "nchi moja, mifumo miwili". Siku hiyo inaitwa 香港回歸 (xiāng gǎng huí guī), kwa Kiswahili "unganisho jipya la Hong Kong". Jina lingine ni 香港回歸祖國 (xiāng gǎng huí guī zǔ guó), kwa Kiswahili "Hong Kong kurudishwa kwa nchi mama".

Demografia

[hariri |hariri chanzo]
Kitovu cha Hong Kong wakati wa usiku

Hong Kong ni maalumu kwa ajili ya mandhari yake pana,bandari asili yakina namsongamano wa watu (milioni saba na nusu juu ya nchi yaKm² 1108 (sq mi 428).

Asili/Kabila

[hariri |hariri chanzo]

Idadi ya sasa ya wakazi wa Hong Kong inajumuisha 92% ya Wachina asilia. Wengine ni Wafilipino (2.5%), Waindonesia (2.1%) n.k.

Sehemu kubwa ya wakazi wanazungumza Kichina cha Canton (Kikantoni), Hong Kong ikiwa jirani na jimbo la Guangdong, ambalowafanyakazi wenyeujuzi walikimbia baada ya serikali yaKikomunisti kuchukua China mwaka1949 na baadaye husafishwa idadi ya watu mwaka1960.

Upande wadini, wengi hawana au wanafuata kidogo jadi, lakini kunauhuru wa dini mkubwa. 56.1% hawana dini yoyote,Wabuddha naWatao ni 21.3%,Wakristo ni 12% (6.5%Waprotestanti na 5.1%Wakatoliki),Waislamu ni 4%.

Uchumi

[hariri |hariri chanzo]

Mji unamaendeleo makubwa kabisa duniani kamakitovu chabiashara na kituo chafedha, inachukuliwa kuwa mji katika dunia na mmoja wa Alpha + majiji nane.

Inashika nafasi ya tano katika 2014 Global Miji Index baada yajiji laNew York,London,Tokyo naParis.

Mji wa kumi kwakipato cha juu cha kila mwananchi katika dunia, lakini pia inaongozaongoza miongoni mwa nchi zenye uchumi mkubwa kwa kukosa usawa wa kipato cha wakazi.

Hong Kong ni ya tatu kama kituo cha biashara muhimu zaidi baada ya New York na London. Huduma uchumi, kwakodi ya chini nabiashara huria, imekuwa huru sana, nafedha yake,dola ya Hong Kong, ni ya 13 kutumika zaidi duniani.

Udogo wa eneo ulileta haja ya miundombinu mingi jirani, na mji ukawa katikati ya vielelezo vyausanifu wa kisasa upande wa majengo, na kuipa Hong Kongmandhari ya mji unaoelekea juu wima.

Hong Kong ina maendeleo makubwa hata upande wausafiri wa umma duniani ukiwa na mtandao wa asilimia 90, kiwango cha juu zaidi duniani, na inategemea wingi wa watu kupita kwa njia yabarabara aureli.

Uchafuzi wa hewa bado ni mkubwa, viwango vyauzalishaji vikiwatatizo. Hata hivyo wakazi wa Hong Kong wanamatarajio ya kuishi kirefu kuliko watu wengine duniani.

Utalii

[hariri |hariri chanzo]

Watalii huenda Hong Kong kwa mvuto wautamaduni,chakula pamoja nasinema,muziki wa Wachina.

Ingawa Hong Kong ina watu wengi wamatabaka mbalimbali, chakula kwa kawaida huwa kimetokana na utamaduni wa Cantonese au Guangdong cuisine.Wali huliwa kwa wingi pamoja nakuku namboga zilizotokamashambani. Chakula huliwa maratano kwa siku yaani:staftahi, chakula chamchana,chai yaadhuhuri, chakula chajioni nasiu yeh ambacho ni chakula cha kuliwa kabla uende ukalale.

Mambo ya kuona Hong Kong ni kama vileKisiwa chaLantau ambapo kivutio kikubwa niGiant Buddha,mchongo ulio mkubwa sana waBuddha, The Peak ambapo utaona Victoria Harbour, Hong Kong Disney Land Resort na Ocean Park Theme.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Serikali
Biashara
Nchi na maeneo yaAsia

Afghanistan |Armenia2 |Azerbaijan |Bahrain |Bangladesh |Bhutan |Brunei |China |Falme za Kiarabu |Georgia2 |Hong Kong3 |Indonesia |Iran |Iraq |Israel |Jamhuri ya China (Taiwan) |Japani |Kamboja |Kazakhstan |Kirgizia |Korea Kaskazini |Korea Kusini |Kupro2 |Kuwait |Laos |Lebanoni |Macau3 |Malaysia |Maldivi |Mongolia |Myanmar |Nepal |Omani |Pakistan |Palestina |Qatar |Saudia |Singapuri |Sri Lanka |Syria |Tajikistan |Timor ya Mashariki |Turkmenistan |Ufilipino |Uhindi |Urusi1 |Uthai |Uturuki1 |Uzbekistan |Vietnam |Yemen |Yordani

1. Nchi ina maeneo katikaAsia naUlaya. 2. Nchi ikoAsia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi zaUlaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.
Makala hii kuhusu maeneo yaChina bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuHong Kong kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
  1. 1234IMF."Hong Kong GDP peofile" (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo2025-02-20.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Hong_Kong&oldid=1459073"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp