Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Homa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kipimajoto ni kifaa cha kupimia homa.

Homa ni hali yawanyama kuwa nahalijoto yamwili juu ya halijoto ya kawaida (37°C katikamamalia).

Halijoto ya kawaida yamwanadamu ni kati ya 36.6 na 37sentigredi zaSelsiasi ikipimwa chini yaulimi.

Maelezo

[hariri |hariri chanzo]

Mara nyingi homa husababishwa naugonjwa; nidalili ya kwambakingamwili inapambana navijidudu auvijimea vinavyosababisha ugonjwa fulani.

Homa si ugonjwa wenyewe bali dalili ya magonjwa mbalimbali. Katikalugha ya kilasikumalaria mara nyingi huitwa "homa" ingawa kupanda kwa halijoto ya mwili wakati wa malaria ni dalili ya mapambano dhidi ya vijidudu vyaplasmodium tu. KatikaKenya "homa" hutumiwa kumaanisha mafua,mafua ya kawaida hasa.

Hadi kiwango cha sentigredi 39 homa sihatari sana, lakini ikipanda juu ya 40°C inaanza kudhoofishaumbile lamtu hadi kuwa hatari yenyewe.

Inashauriwa kumwonadaktari na kutumiamadawa ya kutuliza homa. Kufikia 42°C homa inaweza kumwua mtu kwa kusababisha uharibifu wa viungo vya ndani vya mwili.

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mambo yatiba bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuHoma kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Homa&oldid=1156976"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp