Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Hakimiliki

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Alama ya hakimiliki.
Video inayoeleza historia ya hakimiliki

Hakimiliki(kwaKiingereza: copyright) ni utaratibu wakisheria unaompammiliki wakazi zaakili (kama vilekitabu,sinema,picha,wimbo autovuti)haki ya kuamulia matumizi yake. Sheria za hakimiliki zinalenga kukinga watungaji wa kazi za akili dhidi ya matumizi ya kazi yao na wengine wanaojipatiafaida kwa njia hiyo bila kumzingatia mtungaji anayeweza kukosa ruzuku kutokana na kazi yake.

Chini ya sheria za hakimiliki, kazi ya kiakili inaweza kunakiliwa pekee ikiwa mmiliki anatoaruhusa. Ikiwa mtu ananakili kazi bila kibali, anakiuka hakimiliki.

Kutegemeana na sheria za nchi mbalimbali mkiukaji anaweza kushtakiwa chini ya sheria zabiashara au wakati mwingine sheria zajinai. Mkiukaji anaweza kuhukumiwa kulipa fidia au hata kwendajela. Kwa kawaida, sheria za hakimiliki hulinda haki za watungaji nawarithi wao kwa kipindi fulani, katikasheria ya kimataifa angalau hadi miaka 50 baada yakifo cha mtungaji[1]. Nchi mbalimbali huwa na vipindi virefu zaidi[2].

Katika nchi zinazofuata zaidi sheria zaMarekani kuna kanuni zinazorahisishakampuni kushika hakimiliki badala yawafanyakazi wake kama kazi ilitekelezwaofisini.

Historia ya hakimiliki

[hariri |hariri chanzo]

Hakimiliki ilianzishwa kwawaandishi wa vitabu. Kabla ya kupatikana kwauchapishaji, vitabu viliweza kunakiliwa tu kwamkono, kazi ambayo inachukuamuda mrefu. Lakini kwa kutumiamashine za kuchapa, vitabu vinaweza kunakiliwa kwa haraka na urahisi. Kwa sababu hiyo, vitabu vingi vilinakiliwa, ila waandishi walikosamapato. Ndiyo chanzo cha kutunga sheria ya kumpa mwandishi hakimiliki kuhusu kazi yake.

Kutokana namaendeleo yateknolojia, sheria za hakimiliki zilianza kupanuliwa zikitaja pia media kama picha,sauti, na filamu.

Nani anamiliki hakimiliki?

[hariri |hariri chanzo]

Katika nchi nyingi, watungaji wanamiliki hakimiliki kwa kazi yoyote waliyotengeneza au kuunda, maadamu hawampi mtu mwingine hakimiliki.

Kama mtungaji analipwa kufanya kazi kwa mtu mwingine,mwajiri mara nyingi atapata hakimiliki badala ya mwandishi mwenyewe. Kwa mfano, ikiwa mtu anayefanya kazi kwa kampuniMicrosoft inaunda mpango mpya waprogramu ya kompyuta kazini, kampuni ya Microsoft inakuwa na hakimiliki. Ni kawaida kwamba kampuni itasajili hakimiliki ili kuwazuia wafanyakazi wao kudai kazi zao.

Urefu wa ulinzi wa hakimiliki

[hariri |hariri chanzo]

Sheria za hakimiliki kawaida hulinda wamiliki wa hakimiliki zaidi yamaisha yao. Katika nchi nyingine, kamaKanada,New Zealand naTanzania, kazi zinalindwa kwa miaka 50 baada ya mwandishi kufa. Katika nchi nyingine, kamaMarekani naUingereza, kinga hiyo hudumu kwa miaka 70 baada ya kifo.[3] Wakati kipindi cha ulinzi wa hakimiliki kimekwisha, muziki, kitabu, picha, au kazi nyingine yoyote yaubunifu iko kwenye uwanja waumma . Hii inamaanisha kuwa hakuna mwenye hakimiliki tena, na kila mtu yuko huru kuiga, kuitumia na kuibadilisha bila kuwa na ruhusa ya kuomba au kumlipa mmiliki.

Maudhui huria

[hariri |hariri chanzo]

Ili kuepukana na masuala ya kisheria, vikundi vya waandishi wamekuja na wazo lamaudhui huria (open content). Katika mfumo wa maudhui huria, waandishi wanampa kila mtu ruhusa ya kunakili, kubadilisha, kutoa au kuuza kazi zao, mradi tu watafuata masharti fulani. Masharti hayo yanaelezwa katikaleseni ya maudhui huria. Baadhi ya masharti ya maudhui huria ni:

  1. Ikiwa mtu anabadilisha maudhui huria, au mtu akiunda kazi mpya kutona nayo, lazima amtaje mwandishi wa kwanza.
  2. Ikiwa mtu atachapisha sehemu ya kazi iliyobadilishwa au inayopatikana, lazima awakubali wengine wazitumie chini ya leseni hiyohiyo ya maudhui huria.
  3. Chini ya leseni kadhaa, mtu hawezi kuuza sehemu ya kazi au kuitumia kupatapesa.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. [https://www.wipo.int/treaties/en/text.jsp?file_id=283698#P127_22000 Art 7, Berne Convention for the Protection of Literary and Artistic Works]
  2. Nchini Tanzania sheria ni "The Copyright and Neighbouring Rights Act", 1999, inayofuata Mapatano ya Bern
  3. "Publication Right, Database Right"(PDF).

Viungo vya Nje

[hariri |hariri chanzo]
Makala hii kuhusu mambo ya sheria bado nimbegu.
Je, unajua kitu kuhusuHakimiliki kama historia yake au uhusiano wake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Hakimiliki&oldid=1140451"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp