Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Haiti

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jamhuri ya Haiti
République d'Haïti (Kifaransa), Repiblik d Ayiti (Krioli ya Kihaiti)
Kaulimbiu: "Liberté, égalité, fraternité" (fr)
"Libète, Egalite, Fratènite" (Krioli)
"L'union fait la force" (Kifaransa)
"Inite se fòs" (Krioli)
Wimbo wa taifa: La Dessalinienne (Kifaransa), Desalinyèn (Krioli ya Kihaiti)
Mahali pa HaitiMahali pa Haiti
Lugha rasmiKifaransa, Krioli ya Kihaiti
Kabila
Dini (2020)
  Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Rais
Fritz Jean
 Waziri Mkuu (Halisi)
Alix Didier Fils-Aimé
Uhuru kutoka Ufaransa
  Tangazo la Uhuru
1 Januari 1804
  Kutambuliwa kwa uhuru
17 Aprili 1825
  Dola ya Kwanza ya Kihaiti
22 Septemba 1804
  Katiba ya sasa
29 Machi 1987
Eneo
  Jumlakm2 27,750(ya 143)
  Maji (asilimia)0.7%
Idadi ya watu
  Kadirio la 202311,470,261
  Msongamano382/km2
PLT (PPP)Kadirio la 2023
  Jumla$38.952 bilioni
  Kwa kila mtu$3,185
PLT (Kawaida)Kadirio la 2023
  Jumla$25.986 bilioni(ya 139)
  Kwa kila mtu$2,125
HDI (2023)decrease 0.554
-kati
Gini (2023)41
SarafuGourde ya Haiti (HTG)
Majira ya saaUTC−05:00
Msimbo wa simu+509
Jina la kikoa.ht
Ramani ya Haiti

Haiti, rasmi kamaJamhuri ya Haiti, ni nchi iliyoko katika Karibi, inayochukua theluthi ya magharibi ya kisiwa chaHispaniola. Inapakana naBahari ya Karibi naBahari ya Atlantiki, na inapakana naJamhuri ya Dominika. Ina idadi ya watu takriban milioni 11.7, ikiwa ya 81 duniani. Mji mkuu na jiji kubwa zaidi niPort-au-Prince. Haiti imegawanyika katika mikoa 10 ya kiutawala. Inajulikana kwa kuwa nchi ya kwanza ya watu weusi kupata uhuru mwaka 1804 baada ya mapinduzi dhidi ya utawala waKifaransa, na kwahistoria yake tajiri yakiutamaduni, pamoja na changamoto zakisiasa na za majanga ya asili kama vile matetemeko ya ardhi.

Haiti inahistoria ya kipekee inayohusisha mapambano ya muda mrefu yauhuru,ukoloni, na mabadiliko yakijamii. Baada ya kuongoza mapinduzi ya watumwa yaliyofanikiwa dhidi yaUfaransa, Haiti ikawataifa la kwanza lawatu weusi kujitawala, jambo lililokuwa na athari kubwaduniani kote. Hata hivyo, tangu wakati huo nchi imekumbwa na mfululizo wa matatizo yakisiasa, mapinduzi ya kijeshi, na ukosefu wa uthabiti waserikali, hali ambayo imeathiri maendeleo yakijamii nakiuchumi.

Katikakarne ya 21, Haiti imekumbwa na majanga kadhaa ya asili, ikiwa ni pamoja na tetemeko kubwa la ardhi la mwaka 2010 lililosababishavifo vya zaidi ya watu 200,000 na kuacha mamilioni bila makazi. Mifumo yaafya,elimu namiundombinu imeendelea kuwa dhaifu, hukuuchumi ukitegemea misaada ya kimataifa, uhamishaji wa fedha kutoka kwa watu waishio nje ya nchi, na sekta ndogo yakilimo. Licha ya hayo, watu wa Haiti wanaonyesha uthabiti mkubwa, wakihifadhi tamaduni zao tajiri,muziki,sanaa, na lugha yao yaKrioli ya Haiti.

Jiografia

[hariri |hariri chanzo]

Jina la "Haiti" lina asili katikalugha yaKitaino ya wakazi asilia; linamaanisha "nchi ya milima", na kwelikisiwa kinamilima mingi.

Nchi imegawanywa katikawilaya kumi.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Mwanzo na ukoloni wa Hispania

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi asilia walikuwaWaindioWaarawak.

Baada ya kufika kwaKristoforo Kolumbus nautawala waHispaniaidadi yao ilipungua haraka kutokana namagonjwa yaUlaya ambayo hawakuzoea na kukosakinga dhidi yake, lakini pia kutokana na kutendwa kwa unyama na mabwana wapya.

Wahispania walianzishamashamba kwa kutegemea kazi yawatumwa kutokaAfrika.

Mnamomwaka1600 Waindio wachache tu walibaki kutoka malakhi wakati wa Kolumbus wakapotea kabisa kwa njia ya kuoa au kuolewa naWazungu naWaafrika.

Ukoloni wa Ufaransa

[hariri |hariri chanzo]

Katikakarne ya 17Wafaransa walifikakisiwani wakanunuatheluthi moja ya kisiwa wakaiita "Saint-Domingue" kilichokuwa baadaye Haiti. Wafaransa walileta watumwa wengi kutoka Afrika na kujengauchumi wa mashamba makubwa, hasa yamiwa.Koloni la Saint-Domingue lilikuwa koloni tajiri la Ufaransa katikaAmerika.

Mapinduzi ya Ufaransa

[hariri |hariri chanzo]

Wakati wamapinduzi ya Ufaransa ya mwaka1789 koloni lilikuwa na wakazi wa aina nne:

  • Wazungu, hasa Wafaransa, waliokuwa mabwana lakini walikuwa na tofauti kubwa kati yao: wenginetajiri sana wenginemaskini - jumla takriban watu 32,000
  • machotara na Weusi huru ambao walikuwaraia wa daraja ya pili; wengine walikuwa matajiri na mabwana wa mashamba na pia wa watumwa - jumla watu 28,000
  • watumwa wenye asili ya Kiafrika - jumla watu 500,000
  • Wamaroni walikuwa watumwawakimbizi walioishimlimani katikapori - idadi yao haijulikani lakini hawakuwa wengi.

Mapinduzi ya Ufaransa na kutangaziwa kwahaki za kibinadamu vilisababisha matumaini ya machotara wenyemali ya kukubaliwa kama raia kamili wenyehaki ya kupiga kura. Wenyewe hawakutegemea kumaliza utumwa uliokuwa msingi wa uchumi. Lakini matumaini yao yalishindikana wakakataliwa na watawala kisiwani.

Toussaint L'Ouverture kiongozi wa uhuru wa Haiti

Mapinduzi ya Haiti

[hariri |hariri chanzo]

Sehemu ya matajiri kati ya Wazungu walitaka kujitenga na Ufaransa kwa msaada waUingereza na Hispania wakichukiamapinduzi katika Ufaransa. Watumwa na Weusi huru wenyeelimu walifuata habari hizi wakaogopa ya kwamba utawala wa mabwana hao bilasheria za Ufaransa utakuwa mbaya kuliko hali jinsi ilivyokuwa wakaanza mapinduzi.

Kiongozi wao alikuwaToussaint L'Ouverture aliyefaulu kushikaserikali ya koloni tangu mwaka1798. Awali alipiganiajeshi la Ufaransa; baada yabunge laParis kutangaza mwisho wa utumwa alishirikiana na Ufaransa dhidi ya jeshi la mabwana wenye mashamba waliotaka kuendeleza utumwa katika nchi ya kujitegemea.

Toussaint L'Ouverture alishinda piaWaingereza waliotaka kuwasaidia wapinzani Wafaransa waParis na mwaka1801 akatekakaskazini mwa kisiwa iliyokuwa eneo la Kihispania na kutawalaHispaniola yote akitangaza kote mwisho wa utumwa.

Lakini mnamo mwaka1802siasa ya Paris ilibadilika na mtawalaNapoleon Bonaparte aliamua kurudisha Hispaniola katika hali ya awali akatuma jeshi kubwa laaskari 40,000. L'Ouverture alikamatwa alipokubali kushauriana najenerali Mfaransa akapelekwa kama mfungwa Ulaya. Lakinimakamu wake Jean-Jacques Dessalines aliposikia kuhusu mipango ya Ufaransa ya kurudisha utumwa alianzavita upya. Katika vita vikali Wafaransa walishindwa na Dessalines alitangazauhuru wa koloni tarehe1 Januari1804 kwajina la "Haiti" kama "Jamhuri ya watu weusi".

Wilaya za Haiti

[hariri |hariri chanzo]
Wilaya za Haiti
MINUSTAH kazini wakati wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2006.
  1. Artibonite (Gonaïves)
  2. Centre (Hinche)
  3. Grand'Anse (Jérémie)
  4. Nippes (Miragoâne)
  5. Nord (Cap-Haïtien)
  6. Nord-Est (Fort-Liberté)
  7. Nord-Ouest (Port-de-Paix)
  8. Ouest (Port-au-Prince)
  9. Sud-Est (Jacmel)
  10. Sud (Les Cayes)

Watu

[hariri |hariri chanzo]

Wakazi ni 11,439.646 (2018), lakini wananchi wengine wengi wamehama kutokana naufukara. Karibu 900,000 wakoMarekani, 800,000 wakoDominikana na 300,000Kuba, halafuKanada,Ufaransa,Bahamas.

Uchunguzi waDNA umeonyesha kwambaAfrikaKusini kwa Sahara imeichangia 95.5% na Ulaya 4.3%.

Kunalugha rasmi mbili: moja niKifaransa (42%) na nyingine niKihaiti ("Kreyol") inayotokana nacho (karibu 100%).

Wakazi wengi ni wafuasi waYesu Kristo (86.4%) (katikaKanisa Katoliki 56.8% namadhehebu yaKiprotestanti 29.6%) lakini wengi hufuata vileviledini yavudu inayotokana nadini za jadi kutokaAfrika ya Magharibi.

Tazama pia

[hariri |hariri chanzo]

Viungo vya nje

[hariri |hariri chanzo]
WikiMedia Commons
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi huru
Kamili
Sehemu
Maeneo chini ya nchi nyingine
Udani
Ufaransa
Uholanzi
Ufalme wa Muungano
Marekani
Makala hii kuhusu maeneo yaBahari ya Karibi bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusuHaiti kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuongeza habari.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Haiti&oldid=1425509"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp