Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Eurasia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Eneo la Eurasia
Namna mbalimbali za kuchora mpaka kati ya Ulaya na Asia.

Eurasia nijina linalotumika kutaja kwa pamoja nchi zote zaAsia naUlaya. Jina hilo linaunganisha maneno "Europa" na "Asia".

Hali halisimabara ya Ulaya na Asia yako pamoja kama nchi kavu mfululizo na hakunabahari inayoyatenganisha. Kwa hiyo Ulaya na Asia haziitwi mabara kwa sababu zakijiografia bali kwa sababu zakihistoria na zakiutamaduni tu.

Desturi hii inatokana naWagiriki wa Kale waliokuwa watu wa kwanza wa kugawadunia katika sehemutatu tofauti (Ulaya, Asia naAfrika) na hivyo kuweka msingi wa ugawaji wa dunia kwa mabara.

Wataalamu wengi wa jiografia wanaona ya kwambamasi ya nchi kavu inayojumlisha Ulaya na Asia inatabia zote zabara moja na hivyo hutumia jina la "Eurasia". Karibu eneo lote liko juu yabamba la gandunia lilelile, yaaniBamba la Ulaya-Asia.

Tangu kale suala la mpaka kati ya Ulaya na Asia lilikuwa tata na kuna majibu mbalimbali. Wengi hukubaliana ya kwamba mstari unafuatamilangobahari yaDardaneli naBosporus (nchiniUturuki),mwambao waBahari Nyeusi naBahari Kaspi halafusafu ya milima yaUral hadiBahari Aktiki. Lakini kati ya Bahari Nyeusi na Kaspi katika eneo laKaukasus mawazo hutofautiana sehemu gani ni za Asia na zipi za Ulaya.

Makala hii kuhusu eneo fulani bado nimbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwakuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.

Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Eurasia&oldid=995583"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp