Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Eneo tegemezi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Eneo tegemezi ni lolote lile ambalo si sehemu kamili yanchi huru lakini halijapatamamlaka kamili ya kujitawala, bali linategemeadola mlezi kwa viwango tofautitofauti. Hivyo, eneo tegemezi ni tofauti najimbo aumkoa wa nchi huru kwa sababu si sehemu kamili ya nchi ile. Katika uhusiano na dola mlezi linauhuru zaidi kuliko majimbo au mikoa yake.

Mara nyingi maeneo tegemezi ni madogo aumaskini mno ili kuchukuamajukumu yote ya nchi huru pamoja na kujilinda kijeshi na kuwa namabalozi katika nchi za nje.

Asili

[hariri |hariri chanzo]

Mara nyingi maeneo tegemezi ni mabaki yamakoloni ya awali ambayo wananchi wao hawakupenda kuwa nchi huru wala kuwa sehemu kamili ya nchi tawala ya awali.

Ramani ya maeneo tegemezi duniani
     AUS     CHI     DAN     FRA     NZL     NOR     GBR     USA

Kwa mfanoGreenland ilikuwa koloni laDenmark lakini tangukura ya wananchimwaka2009 ni eneo tegemezi la Denmark. Kunabunge naserikali ya pekee.Ulinzi umo mikononi mwa Denmark, pamoja na sehemu kubwa yasiasa ya nje; Greenland iliamua kutoshiriki katikaUmoja wa Ulaya kama ilivyofanya nchi mlezi wake. Inahaki ya kuachana kabisa na Denmark. Hadi sasa sehemu kubwa ya makisio ya serikali yake inatolewa na Denmark.

Mfano mwingine ni eneo dogo laGibraltar karibu naHispania ambalo limetawaliwa naUingereza tangu miaka 300 iliyopita. Eneo lote nikilomita za mraba 6.7 pekee lenye wakazi 32,000. Hispania inadai Gibraltar kuwa sehemu yake lakini watu wake wamepiga kura mara kadhaa kwaasilimia zaidi ya 90 kuwa wanataka kukaa chini ya ulezi waUfalme wa Muungano.

Orodha ya maeneo tegemezi

[hariri |hariri chanzo]

Kuna maeneo tegemezi katikaAntaktiki yasiyotambuliwa kimataifa, na haya yanatajwa kwaherufi italiki.

Tazama pia:Eneo la ng'ambo la Marekani

Marekani ina maeneo tegemezi 11 na madai juu ya maeneo 2.Atolli ya Palmyra katikaPasifiki ni sehemu kamili ya Marekani ila hutawaliwa kama eneo tegemezi kwa sababu haina wakazi.[1]

BenderaFunguvisiwa
au kisiwa
Eneo la nchi kavu
(km²)
Hori la ndani
(km²)
Kifupi cha
ISO 3166-1
Puerto Rico8.959--PR
Visiwa vya Virgin vya Marekani349--VI
Navassa5,4--

Kituo cha kijeshi chaGuantanamo kipo pia katikaKaribi: ni eneo laKuba lililokodishwa kwa Marekani.

Visiwa katika Bahari ya Pasifiki

[hariri |hariri chanzo]
BenderaFunguvisiwa
au kisiwa
Eneo la nchi kavu
(km²)
Hori la ndani
(km²)
Kifupi cha
ISO 3166-1
Guam549--GU
Visiwa vya Mariana ya Kaskazini477--MP
Samoa ya Marekani199--AS
Visiwa vidogo vya nje vya Marekani5,4--UM
Kisiwa cha Baker1,64--
Kisiwa cha Howland1,85--
Kisiwa cha Jarvis4,50--
Atolli ya Johnston2,67130
Atolli ya Kingman0,01100
Atolli ya Midway6,2040
Atolli ya Palmyra3,98
Atolli ya Wake6,506

New Zealand

[hariri |hariri chanzo]

New Zealand ina eneo moja tegemezi (Tokelau) na eneo moja ambalo inadai kulitawala hukoAntaktiki. Ina pia maeneo mawili (Cook Islands naNiue) yanayojitawala yakiunganishwa nayo kamamadola shirikishi.

Norwei ina eneo tegemezi moja pamoja na madai juu ya maeneo mawili mengine.

Ufalme wa Muungano

[hariri |hariri chanzo]
Tazama piaEneo la ng’ambo la Uingereza

Visiwa vya mfereji wa Kiingereza (Jersey,Guernsey) naIsle of Man si sehemu zaUfalme wa Muungano bali hutazamwa kuwa "maeneo chini yataji la Uingereza", si chini ya Ufalme wa Muungano.

Ufalme wa Muungano huwa na maeneo tegemezi 13: 10 ya kujitawala, 1 ya kijeshi, 1 bila watu. Kuna pia eneo moja bila watu katika Antaktiki ambako Ufalme wa Muungano unadai ulezi.

Tazama pia:Eneo la ng'ambo la Ufaransa

Ufaransa ilikuwa na makoloni mengi kote duniani. Hadi leo kuna maeneo yaliyo mbali na Ulaya lakini ama yamekuwa sehemu kamili za nchi hiyo au zinasimamiwa kama maeneo tegemezi yaliyopewa hadhi ya “jumuiya ya ng’ambo ya bahari” (collectivite d’outre mer) katikakatiba ya Ufaransa ya mwaka 2003.

Maaeneo yote yana wawakilishi katika bunge la Ufaransa na pia katikaBunge la Ulaya. Katika Bunge la Ulaya kuna wawakilishi watatu, mmoja-mmoja kwa maeneo katika Atlantiki, Pasifiki na Bahari Hindi.

Mikoa ya Ng'ambo (Département d'outre-mer) au Jimbo la Ng'ambo (Région d'outre-mer)

[hariri |hariri chanzo]

Maeneo yafuatayo yanapatikana nje ya Ulaya, yalikuwa makoloni ya Ufaransa lakini wakazi wake walipiga kura kuwa sehemu kamili za Ufaransa zikiwa na hadhi ya mikoa ya ng’ambo au majimbo ya ng’ambo ya Ufaransa. Yote ni pia sehemu kamili zaUmoja wa Ulaya.

Hayo ni:Guadeloupe (tangu1946 -Bahari ya Karibi),Martinique (tangu1946 -Bahari ya Karibi),Guyana ya Kifaransa (tangu1946 -Amerika ya Kusini),Réunion (tangu1946 -Bahari Hindi) naMayotte katikaBahari Hindi karibu naKomori; mwaka2011 wakazi walipiga kura wakaamua kuendelea kama Mkoa wa Ng'ambo.

Jumuiya za Kujitawala za Ng'ambo (Collectivité d'outre-mer)

[hariri |hariri chanzo]

Jumuiya hizo zilianzishwa kwa mabadiliko ya katiba ya Ufaransa mwaka 2003. Kila jumuiya imeundwa kwa sheria ya pekee.

Nouvelle-Calédonie auKaledonia Mpya

[hariri |hariri chanzo]
  • Kaledonia Mpya (katikaPasifiki ya kusini) ni eneo la pekee; wakazi walijadili uhuru lakini waliamua kwa kura ya mwaka 2018 kubaki kama jumuiya chini ya Ufaransa.

Visiwa visivyokaliwa na watu

[hariri |hariri chanzo]

Ufaransa hutawala au kudai utawala juu ya visiwa vidogovidogo bila wakazi:

Visiwa vya kusini na eneo la Antaktiki (Terres australes et antarctiques françaises)

[hariri |hariri chanzo]

Maeneo hayo yanatawaliwa kutoka Réunion. Hakuna wakazi wa kudumu, hivyo ni maeneo ya pekee yasiyo na haki za kisiasa: kuna visiwa vya Amsterdam, Saint-Paul, Crozet, Kerguelen na eneo la Adélieland kwenye Antaktiki, halafu Îles Éparses.

Visiwa hivyo hudaiwa pia naMadagaska na Tromelin inadaiwa naShelisheli.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. "Definitions of Insular Area Political Organizations". U.S. Department of the Interior. Iliwekwa mnamo6 Aprili 2019.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Eneo_tegemezi&oldid=1085491"
Jamii:
Jamii iliofichwa:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp