Movatterモバイル変換


[0]ホーム

URL:


Nenda kwa yaliyomo
WikipediaKamusi elezo ya maandishi huru
Tafuta

Elamu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Ramani inayoonyesha eneo la Milki ya Elamu (katika nyekundu) na maeneo ya jirani.

Elamu ilikuwaustaarabu wa kalemashariki mwaMesopotamia. Elam ilienea katikamagharibi nakusini-magharibi mwaIran ya sasa, pamoja na sehemu ndogo ya kusini mwaIraki.[1]

Mji muhimu zaidi ulikuwaShushani; kwakarne kadhaamji mkuu ulikuwaDur-Untashkilomita 40 kusini mwa Shushani.

Historia

[hariri |hariri chanzo]

Historia ya Elamu inajulikana kwa sehemu tu. Ilidumu zaidi yamilenia 2.Wataalamu hugawa historia hiyo kwa vipindi vifuatavyo:

  • Proto-Elamu: mnamo3200 KK -2700 KK (mjini Shushani maandishi na michoro vinapatikana ambavyo ni tofauti naUruk)
  • Elamu ya Kale: 2700 KK -1600 KK (nchi ilivamiwa mara kadhaa na watawala kutoka Mesopotamia, mara chache ilijitawala na hata kudhibiti sehemu za Mesopotamia)
  • Elamu ya Kati:1500 KK -1100 KK (watawala wa Elamu hupanua utawala juu ya sehemu kubwa zaidi za Mesopotamia; hatimaye mtawala wa Babeli alivamia Shushani)
  • Kipindi cha Neo-Elamu: 1100 KK -539 KK (mapambano dhidi ya milki mpya ya Ashuru, hatimaye kuvamiwa na kuharibika na Ashuru)

Rekodi zilizoandikwa huanza kutoka karibu3000 KK katika kipindi cha Waelami wa Kale (Zama za Shaba ya Kati). KatikaMilki ya Waakhamenilugha yaKielamu ilikuwa miongoni mwa lugha zilizotumika rasmi. Lugha ya Kielamu haina uhusiano unaoeleweka na nyingine yoyote.

Waelamu waliita nchi yao "Haltamti", lakiniWasumeri naWaakadia waliiita Elamu, na ndivyo ilivyoitwa pia katikaBiblia ya Kiebrania.

Ustaarabu wa Elamu ulianza karibu 2700 BC, na hatimaye walishindwa naWaakhameni mnamo640 KK. Kibao kilichopatikana mwaka wa1848 kina mfalme waAshuruAshurbanipal akijigamba juu yaushindi wake:

  • Picha ya mwanamke aliyepeperushwa na mhudumu. Anashikilia kifaa cha kusokota. Mezani iko bakuli iliyo na samaki mzima.
    Picha ya mwanamke aliyepeperushwa na mhudumu. Anashikilia kifaa cha kusokota. Mezani iko bakuli iliyo na samaki mzima.
  • Kikombe cha fedha kutoka Izeh, Khuzestan, Iran, chenye maandishi ya Kielami. Mwishoni mwa Milenia ya 3 KK. Makumbusho ya Taifa ya Iran.
    Kikombe cha fedha kutoka Izeh, Khuzestan,Iran, chenye maandishi ya Kielami. Mwishoni mwa Milenia ya 3 KK. Makumbusho ya Taifa ya Iran.
  • Kiumbe mwenye 'pembe mbili' kikishindana na nyoka.
    Kiumbe mwenye 'pembe mbili' kikishindana na nyoka.

Marejeo

[hariri |hariri chanzo]
  1. Potts D.T. 1999.The Archaeology of Elam: formation and transformation of an ancient Iranian state. Cambridge World Archaeology.
Rudishwa kutoka "https://sw.wikipedia.org/w/index.php?title=Elamu&oldid=1245093"
Jamii:

[8]ページ先頭

©2009-2025 Movatter.jp